Wednesday, November 2, 2016

MATUKIO BUNGENI DODOMA LEO

 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangala (kulia) akisalimiana na matabibu wa dawa za asili mjini Dodoma. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA; KAMANDA WA MATUKIO BLOG

 Wabunge wa Kambi ya Upinzani wakijadiliana jambo bungeni Dodoma
 Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Rukwa, Bupe Mwakang'ata akiwa makini kusikiliza hoja bungeni
 Mbunge wa jimbo la Pangani, Jumaa Aweso (kushoto) akijadiliana jambo na mbunge mwenzie

 Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Bulembo (CCM), akichangia hoja kuhusu mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2016/2017 bungeni Dodoma, hasa jinsi ya kuwawezesha vijana nchini
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akijibu maswali ya wabunge

 Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya kupitia Chadema, Sophia Mwakagenda (kulia) akijadliana jambo na mbunge mwenzie
 Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lisu (Chadema), akichangia hoja bungeni, ambapo alihoji watu wasio husika kuwaweka kwenye makumbusho ya mashujaa nchini.
 Mbunge wa Jimbo la Kilindi, Omary Kitua akichangia hoja wakati wa majadiliano ya mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2016/17

 Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT), akichangia hoja bungeni Dodoma , katika mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2016/17.
 Wabunge wakiingia bungeni Dodoma jioni hii
 Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga akichangia mpango huo


 Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini,  Charles Msigwa akichangia mpango huo

Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema akijadiliana jambo na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

Usalama, Faragha na Imani katika matumizi Changamoto kwenye TEHAMA Changamoto kubwa katika TEHAMA


Mkurugenzi Mkuu, Mh. James Kilaba
Na Mwandishi Maalum, Hammamet, Tunisia.

PAMOJA na maendeleo na faida mbalimbali za Tekinolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), masuala ya Usalama, faragha na imani katika matumizi bado yameendelea kuwa masuala ya kuwekwa maanani katika ngazi za kitaifa na kimataifa.

Akihutubia kikao cha Mkutano wa Dunia wa Masuala ya Viwango Katika Mawasiliano (World Telecommunication Standardization Assembly – WTSA-16) mjini Jasmine Hammamet, nchini Tunisia hivi karibuni, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Eng. James Kilaba amesema tekinolojia mpya ndani ya TEHAMA zina mchango mkubwa katika usalama (wa mitandao,mifumo, vifaa, data na wa watumiaji); faragha ( katika data na watumiaji) na Imani (kwenye mitandao,mifumo, vifaa, data na kwa watumiaji). 

“Katika vikao kama hivi vya majadiliano kuhusu TEHAMA, wakati mwingi hatusahau kuzungumzia masuala ya huduma, vifaa na ukuaji wa watumiaji, mtandao na hata mapato. Leo tunazungumzia mchango wa teknolojia mpya katika usalama, faragha na Imani katika matumizi ya TEHAMA”, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA aliuambia mkutano huo.

Eng. Kilaba ailisema kumekuwepo na mabadiliko ya teknolojia kutoka zilizotawaliwa kwa kiasi kikubwa na kuendeshwa kwenye mfumo wa intaneti kwa kutumia kompyuta binafsi zilizounganishwa kwa mfumo wa waya hadi tekinolojia zinazotumia vifaa ya mkononi vilivyounganishwa bila kutumia waya. Amesema hii imewezesha na kufanikisha mawasiliano zaidi na kwa kupitia mfumo wa intaneti kuifikia dunia iliyounganishwa na mfumo wa kompyuta.

Eng Kilaba aliongeza kwamba mada kuu ya majadioiano katika mkutano huo ilikuwa ni huduma, vifaa, kukua na kuongezeka kwa watumiaji na kupanuka na kwa mifumo ya mawasiliano ambayo inawafika mbali zaidi na kuwafikia watu wengi zaidi.

“Wasimamizi wa mawasiliano duniano kote wanayo changamoto ya kukabiliana na mahitaji ya watumiaji na kubadilika kwa vifaa, bila kujali kuwa vimefungwa wapi au kutumiwa vipi ili mradi vinaimarisha usalama, faragha na Imani ya watumiaji. Kwa hiyo kimsingi ni watu ambao wanaishi kwenye utamaduni tofauti na katika maeneo tofauti ya kijiografia”, amesema Mkurugenzi Mku wa TCRA.

Ameeleza kwamba Tanzania, kama nchi inayoendelea imefanya mengi katika sekta ya usalama wa mitandao ya kompyuta zinazotumika kwa mawasiliano. Aliongeza kwamba Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inao mfumo wa Usalama wa Matumizi ya Usalama Mtandaoni ambao umewekwa kwa kushirikisha wadau mbalimbali.

Amesema Tanzania imeanzisha mfumo wa kitaifa wa kushughilikia dharua zinazohusiana na matumizi ya kompyuta za mawasiliano (TZ- CERT) ambao unatumika kutoa elimu kuhusu masuala ya usalama wa mitandao, taarifa na ujuzi kwa wadau na watumiaji ili kuwawezesha kuwa na kiwango cha kuridhisha cha utaalamu unaohitajika katika kushughulikia masuala makubwa yanayohusiana na matumiai ya mitandao ya inayotumia mifumo ya kompyuta kwa mawasiliano.

Hali kadhalika, aliongeza kuwa Tanzania ina kituo cha kitaifa kinachohifadhi data. Vilevile aliuambia mkutanio huo kwamba Tanzania imeanzisha utaratibu wa kuzuia matumizi mabaya ya data au taarifa kutoka kwenye simu za mkononi zilizoibwa nchini Tanzania.Eng. Kilaba alisema kwamba vitengo vya kushughulikia dharua za mifumo ya mawasiliano inayotumia kompyuta imeanzishwa katika nchi nne na kwa kiasi kikubwa nchi hizo zinabadilishana na kulinganisha taarifa kuhusu masuala ya usalama wa mitandao.

Kupitia umoja wa taasisi za Mawasiliano Afrika Mashariki ambao unajulikana kama EACO, nchi wanachama zinakutana na kujadili masuala mbalimbali kuhusu usalama wa mitandao. Aliongeza kwamba changamoto zilizojitokeza kuhusiana na usalama, faragha na Imani katika matumizi ya TEHAMA zinaweza kuainishwa katika maeneo matano ambao ni viwango hafifu, sera, sheria na mikakati.

“Viwango, Sheria na Mikakati vinahitajika ili kuinua kiwango cha ulinzi wa nchi katika masuala ya ulinzi wa mitandao. Kwa kuwa masuala ya usalama wa mitandao hayaishii ndani ya mipaka ya ncchi moja, viwango vilivyowekwa, sheria zilizowekwa na Kanuni zilizopo znahitajika kuhuishwa ili zitumike katika maeneo ya nchi zaidi ya moja na pia ulimwenguni pote. Inaaminika kwamba kuna wataalamu wachache wa masuala ya usalama wa mitandao wenye hadhi ya kimataifa wanaoweza kushughulikia kikamilifu ulinzi na makosa yanayohusiana na mitandao” alileza Mhandisi Kilaba.

Alisisitiza kwamba kuna umuhimu wa kuwa na mikakati ya kitaifa kuhusu masuala ya usalama wa mitandaoo ambayo itawezesha kueneza elimu, ufahamu na ujuzi wa watumiaji na wadau wengine na watumiaji wengine ili kuwawezesha kushughulikia kikamilifu matukio ya usalama wa mitandao. Alisema kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na mfumo wa kuthibiti usalama wa mitandao ndani na nje ya mipaka ya nchi husika.

“Baadhi ya nchi zinazoendelea hazina mifumo ya kuthibiti usalama wa mitandao ya kompyuta za mawasiliano. Mifumo hii ikiwekwa na kutumika inawezesha uratibu, uchambuzi na uchukuaji wa hatua za kuimarisha mifumo na kubadilishana taarifa kuhusu usalama na tishio kwa mifumo ya kompyuta za mawasiliano’, Eng. Kilaba aliuambia mkutano huo.Mkutano wa WTSA unafanyika kila baada ya miaka minne. Mkutano wa wa mwaka huu ulianza 25 Oktoba hadi Novemba 3. Ulitanguliwa na Mkutano wa Dunia wa masuala ya viwango uliofanyika 25 Oktoba 2016.

Asilimia 85 ya Ardhi nchini haijapimwa,Watu wengi wanaendelea kuishi katika makazi holela-Waziri Lukuvi


Hayo ameyasema leo Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi wakati akifungua Mkutano Mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi uliofanyika jijini Dar es Salaam, amesema kuwa wataalam wafanye kazi ya kupima ardhi ili kuweza kuondokana na makazi holela.

Amesema kuwa serikali inapoteza mapato kutokana na kuwa na sehemu kubwa ya ardhi kutopimwa.Lukuvi amesema wapimaji wa sekta binafsi wamekuwa wakifanya vizuri kuliko wale ambao wameajiliwa na serikali.

Amesema lazima kuondokana na mfumo wa hati kwenye karatasi na kuingia katika mfumo wa kieletroniki katika kusaidia wananchi kudhulumiwa ardhi kwa kushirikiana na watumishi wasio waaminifu.

Waziri Lukuvi amesema ni marufuku kwa wapimaji ardhi walioajiliwa na serikali kuwa kampuni za upimaji wa ardhi ili kuondokana na mgongano wa kimasilahi. Amesema katika miaka 10 ijayo kuwa kila mtu kuwa hati na kiwanja au shamba kiwe kimepimwa.Lukuvi amesema katika kuondoa migogoro ya wafugaji ni kuondokana na uchungaji wa mifugo.

Amesema kufika mwishoni mwa mwaka huu wawe wamepima ardhi viwanja 400.Nae Rais IST, Martins Chodata amesema kuwa watashirikiana na serikali katika masuala ya upimaji ardhi.Amesema wapo baadhi ya wapimaji ardhi hawana maadili na kusababisha kuwepo migogoro. 
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akifungua mkutano mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi linalofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia leo Novemva 2-3, 2016.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akionyeshwa moja ya vifaa vinavyotumika katika upimaji wa Ardhi mapema leo katika Mkutano mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi unaofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akipewa maelezo jinsi mambo yalivyobadirika katika mfumo wa Kidigitali.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akiwa amebeba moja ya kifaa kinachotumika katika upimaji.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akionyeshwa kifaa cha kisasa kinachotumika katika upimaji.
Wapimaji wa Ardhi wakiwa katika mkutano Mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi.
Wapimaji wa Ardhi wakiwa katika mkutano Mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akitoa cheti cha shukrani kwa makampuni yaliweza kusaidia kufanikisha mkutano Mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi. Pembeni kushoto ni Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani, Bw. Justo Lyamuya.
 

KIOTA KIPYA CHA MARAHA NA BENDI MPYA YA MJENGONI VYAZINDULIWA RASMI JIJINI ARUSHA


Mkurugenzi wa mjengoni Klabu pamoja na mjengoni Bendi John Mdeme akiongea na waandishi wa habari katika usiku wa uzinduzi huo
wadau waliojitokeza katika uzinduzi wa mjengoni kabu pamoja na mjengoni band wakiwa wanaagiza nyama kwa ajili ya kula(habari pich na Woinde Shizza).
Bendi mpya inayojulikana kama Mjengoni bandi ikiwa inatumbuiza wageni waalikwa , washabiki pamoja na wananchi waliouthuria katika uzinduzi huo
mashabiki na wapenzi wa bendi ya mjengoni wakiwa wanasakata rumba hatariii

Msaniii wa bendi ya Fm Academia Kingombe Blaise na aliuthuria katika uzinduzi huu wa bandi ya mjengoni pamoja na klabu mpya matata ya Mjengoni.
Mmiliki wa blog ya libenee la kaskazini Woinde Shizza wa kwanza kulia nyuma yake ni mmiliki wa blog ya Jamii blog Pamela mollel ,wakanza kushoto ni dada Fatuma wa Stax Tv pamoja na Veronica Ignatus wote tulibahatika kuhuthuria na kushuhudia uzinduzi rasmi wa bendi ya mjengoni pamoja na klabu ya mjengoni .
Jiji la Arusha kwa nyama ni penyewe na pia klabu ya mjengoni kwa kuchoma nyama nzuri ndio pamonaongoza wadau wengi walionekana kuvutiwa na nyama ilikuwa imechoma na wataaalam wa klabu hiyo.
Rais wa bendi Robert Mukongya (Digital) akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari waliouthuria uzinduzi huo
Burudani ikiendelea kutoka kwa bendi ya mjengoni





mmiliki wa jamii blog Pamela mollel akiwa anafafanua jambo kuhusiana na kiota iki kipya kilichozinduliwa rasmi jijini Arusha ambapo alitumia muda huo kuwa sihi wakazi wa mkoa wa Arusha pamoja na wale wageni ambao wanauthuria katika mkoa huu kutoacha kufika mjengoni klabu kwa ajili ya kujipatia nyama choma safi na freshi pamoja na muziki muzuri kutoka katiak bendi ya mjengoni

Habari picha na Woinde Shizza,wa libeneke la kaskazini blog

Bendi mpya ya mziki wa dance ijulikanayo kwa jina la Mjengoni Bandi imezinduliwa rasmi mkoani Arusha huku ikiwaaidi mema wakazi wa jiji la Arusha pamoja na wageni wanaoingia ndani ya jiji hilo

Akiongea na waandishi wa habari katika usiku wa uzinduzi rasmi wa bendi hiyo Rais wa bendi Robert Mukongya (Digital) alisema kuwa wamejipanga kufanya mkoa wa Arusha kuwa na bendi kubwa inayotoa burudani ya nguvu kama zilivyo bandi zingine za jiji la Dar es salaam akatolea mfano FM Academia na malaika bendi.

Alisema kuwa wakazi wa mikoani wamekuwa wakitegemea bendi kutoka jijini dar lakini kwa sasa ivi wamesogezewa burudani karibu kabisa na itakuwa kila siku za wekendi

Aidha alibaiisha kuwa bendi hiyo anayoisimania inawanamziki wengi ambao wanauwezo wa hali ya juu pamoja na uzoefu wakutosha ivyo anaamini wapenzi wa mziki wa dance wataipenda bendi hiyo na kuikubali

Alisema adi sasa bendi na inanyimbo zake na wanajipanga kwa ajili ya kurekodi ili wapenzi ,wadau na wananchi waweze kupata mziki na kuhusikia katika maredio na hata wanapokuwa majumbani.

Alimalizia kwakusema kuwa bendi hiyo ya mjengoni itakuwa inatoa burudani kila wekendi hivyo wakazi wa jiji la Arusha pamoja na wageni wanaoingia wajitokeze kuja kupata burudani ya nguvu inayotoka kwa wanamuziki wa bendi hiyo.Kwa upande wake wa mkurugenzi wa mjengoni Klabu pamoja na mjengoni Bendi John mdeme alisema kuwa ameamua kufungua kiota ichikipya ili wakazi wa jiji la arusha wawez e kupata sehemu ya kistaarabu ya kupata chakula ,nyama choma nzuri pamoja na mziki mzuri wa live bandi

Alisema kuwa kimepita kipindi kirefu wakazi wa jiji la Arusha wamekuwa wanakosa sehemu ya kwenda kupata burudani nzuri ya mziki wa bakurutu pamoja na live bendi inayoeleweka tangu hotel ya sabasaba ifungwe ivyo ameamua kuileta burudani hiyo ili wananchi wa Arusha waweze kupata sehemu ya kustarehe.


Alimewakaribisha wageni kutoka mikoani pindi wanapofika jijini Arusha kutoaacha kuja mjengoni kujipatia burudani ya nguvu kutoka katika bendi ya mjengoni pamoja na nyama choma nzuri na freshi inayotengenezwa na wachoma nyama waliobobea katika sekta hiyo.













watu wakila bata



huyu ndio mpiga kinanda

















Rais wa Bendi ya Mjengoni akiimba kwa hisia