Sunday, June 1, 2014

DIAMOND AWEKA HISTORIA NEW JERSEY

 All Star Club Elizabeth New Jersey Diamond akikamua licha ya show kuchelewa kuanza na wapenzi wa Diamond kushikwa na jazba wakitaka aendelee lakini ikashindika kutokana na muda wa kufunga club kufika. 
 AJ nae akifanya yake baada ya kupewa nafasi ya ufunguzi katika show hiyo iliyofanyika New Jersey.
AJ Ubao na Dirty Hary wakishambulia jukwaa kwenye show ya kufubgua pazia iliyoanyika New Jersey na baadae Prezidaa wa Wasafi, Diamond Plutnumz kuwapagawisha mashabiki wake wa ukanda wa pwani ya mashariki.
Ni Rais wa Wasafi akishambulia jukwaa akiwa na madancer wake kwenye show ya kukata na shoka iliyofanyika New Jersey na kuvuta mashabiki kutoka kila kona ya pwani ya mashariki ambayo ni DC, PA, NJ, NY, CT, MA na kwingineko
Diamond mwanamuziki wa kizazi kipya anayekimbiza vibaya mno kwenye anga za Bongo Flava akipagawisha mashabiki wake New Jersey nchini Marekani.
Diamond na madancer wake wakijaribu kukata kiu ya mashabiki wake wa pwani ya mashariki.
 Wapenzi wa Diamond wakipagawa na show ya Diamond iliyofanyika All Star Club Elezabeth NJ.

Shabiki akidata na show ya pezidaa wa wasafi.

Shabiki akidatishwa na moja ya wimbo wa Diamond na kushindwa kujizuia kupanda jukwaani.

Mashabiki wa Diamond wakipagawa huku wengine wakipata taswira za hapa na pale.
kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Picha zote na Vijimambo Blog

Marehemu Amina-Zahara Shabani Mtengeti azikwa leo Kisutu, Dar es salaam

 Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Ghalib Bilali, Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na viongozi wengine na waombolezaji wakiwa katika mazishi ya marehemu Amina-Zahara Shabani Mtengeti katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam jioni hii. Marehemu, ambaye ni mdogo wa Hajat Mwantumu Malale, Dkt. Asha-Rose Migiro, Balozi Radhia Msuya, alifariki jana
 Shughuli za mazishi zikiendelea
 Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Ghalib Bilali akiweka udongo kaburini
 Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi akiweka udongo kaburini
 Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim akiweka udongo kaburini
 Jaji Mkuu Mhe. Mohamed Chande Othman akiweka mchanga kaburini
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Said Mecky Sadick akiweka mchanga kaburini
 Viongozi, ndugu, jamaa na marafiki wakiweka udongo kaburini
 Balozi Juma Mwapachu akiweka udongo kaburini
 Makamu Mwenyekiti wa CCM Mhe Philip Mangula akiweka udongo kaburini
Ndugu, jamaa na marafiki wakiweka udongo kaburini.
Picha na Sultani Kipingo wa Globu ya Jamii


Kili music tour yavunja rekodi Mwanza

 Wakaazi wa Mwanza wakiwa wamefurika kwa maelfu huku wakishangilia wakati kundi la Weusi likitumbuiza  katika show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.

 Msanii wa Bongo flava, Ben Pol akitumbuiza maelfu ya wakazi wa Mwanza wakati wa show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
 Msani wa muziki wa dance, Christian Bella akikonga nyoyo za wakazi wa Mwanza katika show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
 Msanii wa bongo flava, Fid Q akizungumza na wakazi wa Mwanza wakati akitumbuiza katika show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
 Vanessa Mdee na Ommy Dimpoz wakimakinika katika show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Rich Mavoko akipagawisha wakazi wa Mwanza katika show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
 Wakazi wa Mwanza wakiwa wamefurika kwa maelfu huku wakishangilia wakati kundi la Weusi likitumbuiza  katika show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
 Msanii wa miondoko ya Bongo flava, Young Killer akimtambulisha mama yake mzazi wakati wa show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
 Vanessa Mdee na Fid Q wakishirikiana kutoa burudani wakati wa show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.
Msanii wa Bongo Flava Izzo Biznez akifanya vitu vyake wakati wa show ya Kilimanjaro Music Tour iliyofanyika katika Uwanja wa Kirumba na kuwavutia maelfu ya mashabiki. Ziara hii inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager.

WAHARIRI NA WANAHABARI WATEMBELEA HIFADHI YA KISIWA CHA SAANANE JIJINI MWANZA

Baadhi ya Wahariri wa habari na Waandishi waandamizi toka vyombo mbalimbali vya habari wakitoka katika lango la ofisi za Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Saanane tayari kuelekea kisiwani.
Baadhi ya Wahariri wa habari na Waandishi waandamizi toka vyombo mbalimbali vya habariwakiwa katika boti wakielekea Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Saanane.
Mwandishi wa Habari wa kituo cha  TBC 1,Ben Mwaipaja akiwa ameshika jembe lake tayari kwa ajili ya kuchukua matukio.
Safari ilikuwa ni ya takribani dakika 15 hadi 20.
Hatimaye Watalii hao wa ndani wakafika katika Kisiwa cha Saanane.
Baadhi ya Wahariri wa habari na Waandishi waandamizi toka vyombo mbalimbali vya habari wakikaribishwa na Mwongoza Watalii katika Hifadhi ya Taifa ya Saanane Patricia Mtenga.
Safari ya kuelekea katika eneo la kuanzia ziara ya kitalii katika Hifadhi hiyo ikaanza.
Baadae Wahariri wa habari na Waandishi waandamizi toka vyombo mbalimbali vya habari wakapata historia ya Hifadhi hiyo kutoka kwa Muongoza Watalii Fua Hamis.
Baadhi ya Wahariri wa habari na Waandishi waandamizi toka vyombo mbalimbali vya habari wakisikiliza kwa makini maelezo ya mhifadhi Fua Hamis(Hayupo Pichani)
Safar ya kutembelea maeneo mbalimbali katika hifadhi hiyo ikaanza.
Moja ya eneo ambalo liliwavutia Wahariri hao ni eneo hili ambalo unatazama Taswira ya Ziwa Victoria vyema.
Safari iliendelea.
Eneo hili linajulikana kama Jiwe la Kuruka na hapa Mkuu wa Idara ya Ikolojia na Ulinzi katika HIfadhi hiyo Donates Bayona namna ambavyo watalii wa ndani wamekuwa wakifurahia kupata Taswira za Mawinguni wakiwa katika Jiwe hilo.
Baada ya kupita katika maeneo mbalimbali Safari ya Kurudi ikaanza.
Wakati Safari ya kurudi ikiendelea bahati mbaya Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa TANAPA ,Ibrahim Mussa aliteguka mguu baada ya kukanyaga vibaya jiwe hali iliyopelekea kupatiwa huduma ya kwanza.
Baada ya kufikishwa katika eneo la Mapumziko ndiko kukafanyika taratibu za kupelekwa Hosptali kwa ajili ya matibabu zaidi.
Hatimaye akapelekwa Hosptali.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii aliyekuwa jijini Mwanza.