Saturday, March 1, 2014

YANGA YAITANDIKA AL AHLY BAO 1 - 0 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR LEO

 Kikosi cha Yanga 
 Kikosi cha Al Ahly
 Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Mrisho Ngassa akiondoka na mpira huku Beki wa Timu ya Al Ahly ya Misri akitafuta namna ya kumzuia katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
 Kiungo mchezeshaji wa Yanga,Haroun Niyonzima akitafuta namna ya kuwatoka mabeki wa Timu ya Al Ahly ya Misri katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
 Kiungo mchezeshaji wa Yanga,Haroun Niyonzima akizuiwa na Beki wa Timu ya Al Ahly ya Misri,Ramy Abdel Aziz katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
Kipa wa timu ya Al Ahly ya Misri,Sherif Ekramy Ahmed akida moja ya hatari iliyokuwa ikielekeshwa langoni kwake na Mshambuliaji wa Yanga,Hamis Kiiza.
 Heka heka ya kuwania mpira wa Kichwa.
 Mshambuliaji Machachari wa timu ya Yanga,Emmanuel Okwi akiwachachafya mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri katika mchezo wao uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wa kuwania tiketi ya kusheza 16 bora ya Klabu Bingwa Barani Afrika.katika mchezo huo,Yanga imeifunga timu ya Al Ahly bao 1 - 0. 
 Emmanuel Okwi wa Yanga akichezewa faulo na mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri.
 Heka heka langoni mwa timu ya Al Ahly.
Mshambuliaji Emmanuel Okwi wa Yanga leo ndio alikuwa mwiba kwa timu ya Al Ahly,maana alikuwa akikabwa na Mabeki wawili wawili........
 Kipa wa timu ya Al Ahly ya Misri,Sherif Ekramy Ahmed akiruka mithili ya nyani wakati akiokoa moja ya hatari zilizokuwa zikielekezwa langoni kwake.
 Okwi anatafuta namna ya kuchia shuti.
 Mshambuliaji wa Yanga,Didier Kavumbagu akiwania mpira na Mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri.
 Ulinzi maridhawa kabisa ulitawala Uwanjani hapa.
 Ilikuwa ni nyomi la hatari.
Wachezajiwa timu ya Yanga wakishangilia ushindi wao sambamba na Mashabiki wao lukuki waliofurika uwanjani hapa.

Mfungaji wa bao pekee la Yanga,Nadir Haroub akirejea uwanjani baada ya kutoka kushangilia pamoja na washabiki wao.
 Benchi la ufundi la Al Ahly ya Misri.
 Benchi la Yanga.
 Mashabiki wa Al Ahly wakishangiliwa mwanzo mwisho,wakisaidiwa na Mashabiki wa timu ya Simba. 
 Okwiiiiiiii.......
Kocha wa Al Ahly akihaha kutoa maelekezo kwa Wachezaji wake. 
 Mabeki wa timu ya Yanga,Nadir Haroub pamoja na Kelvin Yondani wakiwa wamejipanga vyema kuuzuia mpira wa Mshambuliaji wa timu ya Al Ahly,Moussa Yedan.
 "Poa tu mwana,hii ni fea pleii tuuuuu......" 
 Ni shangwe tupu kwa Mashabiki wa timu ya Yanga uwanjani hapa hii leo. 
Mashabiki wa timu ya Al Ahly wakifungasha virago vyao baada ya kulala kwa bao 1 - 0.
 Kocha wa Yanga akisema na wachezaji wake mara baada ya kipenga cha mwisho kulia.
 Kufungwa kubaya jamaniiiiii....
 Mara baada ya Yanga kupata Goli la kwanza na la pekee,Mashabiki wa Simba walianza tena kunyoa viti na kuwarushia mashabiki wa timu ya Yanga waliokuwa wakishangilia ushindi wao huo. 
 Wazee wa feva wakiwatuliza washabiki hapo wa Simba.
Cheki mapengo ya kung'olewa kwa viti uwanjani hapa.Hali hii ni nani anatakiwa kuidhibiti???

ukishangaa ya mussa....

Yes, that is cash piled on the table in the background!
Just a small collection of guns - these people are not really dangerous at all; not.
Yes, that is real gold on these guns!
Gold and Titanium 45 Caliber semi automatic pistols - they found 16 of these!
Go and kill in the name of the Lord my son was etched!  There was a matched pair of these found.
357 Magnum semi automatic with solid gold grips.
This guy had a better gun collection then most legitimate museums do.
Just a quaint little villa in the hills - Drug money bought it all!
Man made cave and hot tub inside the home.
A collection of exotic animals - which were cared for in the grandest fashion by the way.
8 Lions were on the property.
A very rare Tiger!
The back yard pool.
Exotic art collection -  some of which was illegal to own - some stolen.
More guns than you could ever imagine!
This pile of cash before it was counted was estimated to be approximately 18 Billion Dollars!  After it was counted it turned out to be a little more than 22 Billion Dollars!
22 Billion Dollars from another angle.
Guns and more cash hidden all over the house, along with ample ammo, just in case of trouble.
Additional stacks of cash were found in every nook and cranny!
This case is filled with 100 dollar Bills estimated to be and additional 1/2 a million dollars and no doubt headed out to make another drug by perhaps from the Columbians.
Additional 18 plastic bins filled with 100 dollar bills were discovered!
Another cabinet stack tight with cash - all 100 dollar bills.
Even more 100 dollar bills!
Each of these stacks of 100 dollar bills holds $250,000 (a quarter of a million dollars)!  They also had millions in Columbian money and Mexico Pesos although they preferred American dollars for the most part.
Folks, there were even stacks of Chinese Yen found in one closet!
More Gold machine guns and pistols -  more were never fired, just held for collection value.
They just burned it all down!
The money and valuables found in this one house alone, would be enough to pay for health insurance for every man, women and child in the USA for 12 years!
There are believed to be approximately 27 more of these houses in Mexico alone not to mention the ones in other countries who are enriching themselves in the illicit drug trade.  
These people have so much money, they make the great Arab oil sheiks look like welfare recipients.  Their money can buy the best politicians, some cops, the best judges, or whatever they need they just throw down stacks of cash and it is theirs! 
This is why the drug problem is so difficult to fight.

MAMBO 6 YANAYOMFANYA MTU AWE KIONGOZI BORA NA SIO BORA KIONGOZI

Tukiacha mbali picha ambayo mara nyingi au kwa miaka mingi imekuwa ikijengwa  vichwani mwa wengi wanapoona na kudhani kwamba fulani ni kiongozi bora [pengine kwa muonekano tu], au kwa sababu anashuka kutoka kwenye gari kwa mbwembwe, tabasamu baada ya kufunguliwa mlango na mkanda na kisha kupokelewa briefcase yake, yapo mambo kadhaa ambayo yanamfanya mtu awe kiongozi bora na sio bora kiongozi. Na kadri siku zinavyokwenda, taswira ya kiongozi kwa muonekano tu inazidi kupotea. Vitendo,maadili,mafanikio, uvumbuzi na maendeleo vinachukua mstari wa mbele.

Tofauti na miaka ile ambayo picha ya kiongozi bora ilikuwa kama hiyo hapo juu, siku hizi viongozi bora wapo na wanajitokeza katika hali tofauti tofauti kabisa. Anaweza kuwa asiyevaa suti kama Dalai Lama na akawa kiongozi bora. Au asiyevaa suti bali t-shirt na jeans tu kama alivyokuwa Steve Jobs wa Apple au Mark Zuckerberg boss wa Facebook. Mifano ya viongozi hawa ipo mingi.

Kituo cha utafiti na mafunzo ya uongozi cha Dale Carnegie cha jijini New York nchini Marekani kinasema katika utafiti wao wamegundua kwamba kinachomfanya mtu awe kiongozi bora sio suti, briefcase, tabasamu[ hususani lile la uongo] bali uwezo na nia ya dhati katika kuamsha ari, kuwawezesha unaowaongoza, kuwafanya wajiamini na kuwapa motisha watu unaowaongoza.

Pamoja na hayo, na kutokana na ukweli kwamba leo hii tuna kila aina ya viongozi, yapo baadhi ya mambo yanayowatofautisha viongozi bora na bora viongozi. Haya hapa ni baadhi yake;
  • Aweze Kuyakabili Matatizo au Changamoto
Kiongozi bora ni yule ambaye ana ujasiri wa kutosha wa kukabiliana na kila aina ya changamoto au matatizo ambayo yanaweza kujitokeza iwe aliyatarajia au hakuyatarajia.

Dunia ya leo imejaa changamoto za kila aina. Kila kukicha kuna jipya na gumu zaidi. Uchumi umeporomoka, fedha haina thamani tena, kimbunga kikali kimekuja na kuipindua juu chini shule ya kijiji. Kiongozi bora anafanyaje? Anapotelea mjini kwa kisingizio cha kuwa “bize” au anakuwepo bega kwa bega kutatua tatizo?

Jibu lipo wazi. Kiongozi bora atakuwepo na kuwasiliana na kila mtu anayemuongoza iwe ni ofisini au jimboni kuhusu ukweli halisi na ukubwa wa tatizo na jinsi ambavyo yeye kama kiongozi analishughulikia [kwa kushirikiana na kila mtu wakiwemo anaowaongoza] tatizo au changamoto husika.
  • Awe Muaminifu
Kiongozi bora lazima awe muaminifu. Uaminifu unaanzia kwenye kuwa mkweli. Anaposema atafanya hili au lile, alifanye. Asipolifanya, awe muwazi na kuwaeleza wale anaowaongoza ukweli wa sababu zilizofanya asitimize ahadi yake na jitihada anazofanya kutimiza ahadi yake.

Kwa mfano wananchi wanapomchangua “kiongozi” kutokana na sera na ahadi za kutatua tatizo la ukosefu wa maji safi jimboni kwao kisha miaka mitano baadae ahadi hiyo ikawa haijatimia, ni wazi kwamba imani kwa kiongozi huyu itafifia kama sio kupotea kabisa. Mbaya zaidi pale atakapokuja na sababu ambazo hazina mashiko huku kila mtu akiona wazi kwamba ahadi yake ilikuwa ahadi hewa au ya kisiasa.

Onyesha kwamba unawajali na kuwathamini unaowaongoza. Yaelewe matatizo na changamoto za unaowaongoza. Shirikiana nao bega kwa bega kuyatatua. Usiwe kiongozi wa ofisini tu bali nenda kule walipo. Na usiende kwa nia ya kupigwa picha tu. Ili wakuamini ni muhimu wakaona kwamba wewe sio “mwizi” tu wa fursa.
  • Kuwa Halisi [Asiwe Feki]
Mojawapo ya mambo ambayo sio tu yanamfanya mtu awe bora kiongozi bali apoteze kabisa hata nafasi ya kuongoza ni pamoja na kuwa “feki”. Ni rahisi sana kwa mtu/watu kutambua kwamba huyu si yeye. Anajifanya kuwa mtu ambaye siye.

Kwa bahati mbaya hakuna mtu anayependa “feki”. Viongozi wanasiasa huanguka sana kwenye mtego huu. Wengi wanadhani wananchi hupenda kusikia mashairi na ngonjera tamu tamu pekee. La. Labda zamani. Siku hizi ukiwa kitimbakwila utajulikana kirahisi na utakuwa nje ya ulingo. Wenzetu wanasema Walk The Walk and Talk The Talk.

Hata kama wewe ni kiongozi wa ofisi au mfanyabiashara, pindi tu utakapokuwa “feki” wateja wako watajua. Watakukimbia. Watahisi hata vitu unavyouza ni “feki” kwa sababu wewe mwenyewe unaonekana feki au unajibeduisha kuwa sivyo. Kuwa orijino. Unapenda kucheka au kuchekesha? Cheka. Wachekeshe unaowaongoza. Unapenda muziki? Usihofu kuonyesha wazi kwamba unapenda muziki. Tumia vitu unavyovipenda au maarifa unayoyamudu zaidi kutengeneza aina yako ya uongozi.
  • Ajiheshimu
Kiongozi bora lazima ajiheshimu. Na dhana ya kujiheshimu ni pana. Kuna kujiheshimu katika nyumba na mahusiano yako iwe na wanao, mkeo, wazazi wako, ndugu, jamaa na hata marafiki. Kuna kuiheshimu ofisi yako na watu unaowaongoza. Kiongozi ambaye kila siku anakabiliwa na tuhuma za ulaji rushwa, uongo, umalaya ni wazi kwamba hajiheshimu na hivyo ni ngumu kuwafanya watu wengine wamheshimu. Nawajua baadhi ya “bora viongozi” ambao wametumbukia huko kutokana na tabia zao za ufuska ambazo ingawa wanahisi watu hawajui, kwa kiasi kikubwa zimewapotezea heshima ya uongozi na hususani uongozi bora.

Unapojiheshimu, inakuwa rahisi kuongoza wengine. Hakuna mtu anayependa kujishirikisha na mtu asiyejiheshimu. Watu hujisikia faraja kuhusiana au kufanya biashara na watu wanaojiheshimu. Pia hata kama unaongoza ofisi au biashara tu,wateja wenye akili timamu wanataka kutumia hela zao mahali ambapo ofisi au biashara inaheshimu na kutimiza ahadi zao kufuatana na misingi. Ukisema kwamba ninyi ndio duka lenye bei chee zaidi na bidhaa halisi, basi iwe ni kweli. Vinginevyo inaashiria kwamba hamjiheshimu. Ni waongo. Uongo ni sehemu ya kutojiheshimu.
  • Jifunze/ Taka Kujua Zaidi/ Nenda Na Wakati
Kiongozi bora ni yule ambaye anataka kujifunza zaidi na ni mtafiti. Mwisho wa darasa sio mwisho wa kujifunza kwa kiongozi bora. Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini aliwahi kunieleza katika mahojiano yangu naye jinsi ambavyo alishangaa wakati fulani kusafiri na viongozi fulani kutoka Tanzania mpaka Ujerumani na asione wakisoma hata vipeperushi vinavyokuwa kwenye viti achilia mbali vitabu,magazeti nk.Viongozi bora wanauliza maswali. Wanauliza maswali kwa nia ya kujifunza, kupata maarifa na taarifa. Ni wasikivu na wapo tayari kufundishwa.

Kwa bahati nzuri dunia ya leo ina kila nafasi na uwezekano wa kujifunza. Hizi ni zama za sayansi na tekinolojia. Kiongozi bora atataka kujua…hicho kitu kinachoitwa Twitter ni nini? Kinafanyaje kazi? Atajiunga. Atataka kujua jinsi watu wanavyowasiliana siku hizi. Atataka kujua jinsi nchi za wenzetu wanavyofanikiwa katika masuala mbalimbali. Atajitahidi na kuchunguza mpaka mwisho kuona kama sayansi hiyo au maarifa hayo yanaweza pia kutumika nchini kwake,jimboni kwake, ofisini kwake nk. Kiongozi bora atasoma vitabu,majarida,magazeti, nk kwa nia ya kujifunza zaidi.
  • Kuwa Mtendaji
Yote niliyoyataja hapo juu yanakamilishwa au kuhusishwa moja kwa moja na utendaji. Kiongozi bora haishii kwenye kuongea tu huku akijizungusha kwenye kiti na kuagiza chai. La.Anatenda. Ananyanyuka, kwenda na kutenda kama mfano. Tunapomkumbuka Mwalimu Nyerere kama kiongozi bora aliyewahi kutokea ni kwa sababu alikuwa mtendaji. 

Aliongea,kuelekeza,kuonya lakini mwisho wa siku alikuwa mtendaji.
Nyanyuka na enenda ukaifanye kazi. Onyesho kwa vitendo kwamba wewe ni kiongozi bora na sio bora kiongozi.
Jeff Msangi ni mwandishi, mchunguzi wa masuala mbalimbali na mmiliki wa mtandao wa www.bongocelebrity.com. Unaweza kuwasiliana naye kupitia jeffmsangi at gmail dot com