Wednesday, May 22, 2019

MAMA JANETH MAGUFULI ATOA FUTARI KWA AJILI YA FAMILIA ZENYE UHITAJI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, amewasihi Waislamu nchini kuendelea kuliombea Taifa muda wote, hususan katika kipindi hiki cha  Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, na kuendeleza mshikamano bila kujali dini ama kabila tabaka zao.
Mama Magufuli ametoa wito huo leo tarehe 22 Mei, 2019 Jijini Dar es Salaam wakati akitoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji.
Vyakula alivyotoa ni tani 5 za mchele, tani 3 za sukari na tende. Hafla hiyoimehudhuriwa na Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe Nuhu Mruma, Mkurugenzi wa Hijja wa BAKWATA Shekhe Haidary Kambwile na wawakilishi wa vikundi mbali mbali vya wenye uhitaji.
Mama Magufuli pia amemuomba Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema, azikubali funga za Waislamu wote  na kuwalipa malipo stahiki wakati wakitekeleza moja ya nguzo muhimu za Dini ya Kiislamu.
“Kipindu cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni kipindi cha toba. Ni kipindi cha kutenda matendo mema na kujizuia na vitendo viovu” amesema Mama Magufuli.
Mama Magufuli amesema licha ya kwamba Tanzania ina watu wa imani za Dini tofauti lakini siku zote wananchi wake wamekuwa wakishirikiana nyakati za dhiki na za raha bila ubaguzi.
Ametoa mfano kuwa licha ya tofauti za kidini zipo baadhi ya familia ambazo Baba Muislamu na Mama ni Mkristo zinaishi kwa amani na kushirikiana katika masuala yote ya kifamilia na kwamba sifa hii ni moja nguzo muhimu za umoja wa Watanzania.
“Binafsi nakumbuka zamani nikiwa mdogo tulikuwa tunatafuta Mwislamu aje atuchinjie kuku ama mbuzi ama ng’ombe” , alisema na kuongezea: “Ni kutokana na utamaduni huo uliojengeka miongoni mwa Watanzania , leo nimeguswa kutoa sadaka yangu kwa ajili ya ndugu zangu wenye uhitaji…”
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiongea machache wakati wa hafla ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimsiliza Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe  Nuhu Muma akitoa shukurani wakati wa kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019

 Wawakilishi waliohudhuria wakiitikia dua baada ya kupokea msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Wawakilishi waliohudhuria wakiitikia dua baada ya kupokea msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiitikia dua baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe  Nuhu Muma msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi Mkurugenzi wa Hija wa BAKWATA Shekhe Haidary Kambwile  msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi muwakilishi wa watototo msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi muwakilishi wa wazee msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi muwakilishi wa kinamama msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli katika picha ya kumbukumbu na   Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe Nuhu Mruma, Mkurugenzi wa Hijja wa BAKWATA Shekhe Haidary Kambwile pamoja na wawakilishi wa vikundi mbali mbali vya wenye uhitaji baada ya hafla ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji.
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na wawakilishi baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na wawakilishi baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na wawakilishi baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na wawakilishi baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na  Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe Nuhu Mruma, Mkurugenzi wa Hijja wa BAKWATA Shekhe Haidary  baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019

2 comments:

Unknown said...

Did you know there's a 12 word sentence you can communicate to your partner... that will induce deep feelings of love and impulsive attraction for you buried inside his chest?

Because hidden in these 12 words is a "secret signal" that triggers a man's impulse to love, adore and look after you with all his heart...

12 Words Will Trigger A Man's Desire Instinct

This impulse is so built-in to a man's brain that it will make him work better than ever before to build your relationship stronger.

As a matter of fact, triggering this dominant impulse is absolutely binding to achieving the best ever relationship with your man that the instance you send your man one of these "Secret Signals"...

...You'll immediately find him expose his soul and mind for you in such a way he haven't expressed before and he will see you as the only woman in the world who has ever truly fascinated him.

William said...

If you are searching for genuine QuickBooks Customer Service dial QuickBooks Support Phone Number + 1855-550-7546 for immediate help .Our Quickbooks Support Phone Number is available 24*7.