Wednesday, January 2, 2019

NAIBU WAZIRI SHONZA AWATAKA WASANII KUJIJENGEA TABIA YA KUJIWEKEA AKIBA


Naibu waziri wa Habari, sanaa utamaduni na michezo, Juliana Shonza akizungumza katika tamasha Tukuza Festival Genesis one katika hotem ya Corido Spring Jijini Arusha. Picha/habari na Vero Ignatus.
Rais wa Mtandao wa wasanii wa Injili na Maadili Tanzana Dkt. Godwin Maimu
Naibu Waziri wa Habari, sanaa, Utamaduni na michezo Juliana Shonza akipeana mikono na Rais wa Tagoane Dkt. Godwin Maimu mara baada ya kuzindua mfuko wa Tagoane Loan Fund Jijini Arusha.
Afisa michezo wa Jiji la Arusha Benson Maneno akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika Hotel ya Corido Spring Jijini Arusha
Naibu waziri wa habari sanaa, utamaduni na michezo Mhe. Juliana Shonza akizungumza katika uzinduzi wa Mfuko wa Tagoane Loan Fund jijini Arusha.
Rais wa Mtandao wa wasanii wa Injili na Maadili Tanzania Dkt. Godwin Maimu akizungumza na wasanii mbalimbali waliohudhuria katika tamasha la Tukuza festival Genesis one Jijini Arusha.
Naibu waziri wa Habari sanaa utamaduni na michezo Juliana Shonza akisalimiana na Mkurugenzi wa Newlife Band Fortunatus Mabondo(Hondo)
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na michezo Juliana Shonza akivishwa skafu na mmoja wa Skauti Jijini Arusha
Mkurugenzi wa Newlife Band Fortunatus Mabondo(Hondo) Mabondo akipeana mkono wa pongezi na Rais wa Mtandao wa wasanii wa Injili na Maadili Tanzana Dkt. Godwin Maimu
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, utamaduni na michezo akipokelewa na kikundi cha ngoma cha jamii ya wamasai cha Meserani Jijini Arusha
Picha ya pamoja Naibu Waziri wa habari, sanaa, utamaduni na michezo Juliana Shonza, Rais wa Tagoane Tanzania Dkt. Godwin Maimu, Katibu mkuu mtendaji wa Tagoane Taifa Silvanus Mumba, Afisa michezo Jiji la Arusha Maneno.
Picha Naibu Waziri wa Habari, sanaa, utamaduni na michezo Juliana Shonza akiwa na wasanii mbalimbali pamoja na viongozi wa Tagoane.


Na Vero Ignatus, Arusha

Naibu waziri wa Habarui, sanaa utamaduni na michezo Mhe. Juliana Shonza amewataka wasanii wa Injili kjijengea tabia ya kujiwekea akiba ili punde wapatapo matatizo waweze kuyatatua kwa urahisi.

Ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akizindua mfuko wa Tagoane LoanFund Jijini Arusha ambapo amepongeza uongozi wa Tagoane kufikia hatua hiyo. Ameyataka mashirikisho yote ya muziki wa Injili nchini Tanzania kuiga mfano nzuri wa Tagoane ili waweze kuwa na mashirikisho ambayo ni hai na yanayoleta mshindo kwenye jamii.

Amesema yeye kama mlezi wa wasanii wote nchi amewaomba waamke wachangamkie fursa na wasiwe wavivu kujifunza kutoka kwa wenzao waliofanikiwa .Amewataka wasanii kukaa kwa pamoja Kuonyeshe Uzalendo kwa nchi yao wajadili changamoto mbalimbali wanazozipitia na kutafuta namna ya kutazua changamoto zinazowakabili.

Kwa upande wake Rais wa Tagoane Taifa Dkt. Godwin Maimu amesema kuwa wanedhamiria kuanzisha mfuko wao wa Tagoane Loan Fund ambapo mpaka sasa umekuwa na wanachama ambao wameshachangia akiba zao zipatazo shilingi milioni kumi.Amesema mfuko huo unatarajiwa kuanza kutoa mikopo kwa wanachama wavhqngiaji kuanzia 2 januari 2019

maendeleo kama vijana hayawezi kuendelea ukiwa na jitihada za mtu mmoja mmoja bali balintunapounganisha nguvu zetu kwa pamoja mwisho wa siku tunapata kitu cha kuweza kutusaidia. Alisema Dkt Maimu

Amesema lengo la mfuko huo ni kuwakwamua wasanii watakaokuwa na miradi ya uwekezaji, makampuni makubwa, na watakaoweza kutoa fursa na ajira kwa vijana hapa nchini na kulipa kodi kama wananchi wengine

Aidha tamasha hilo lililoshorikisha wasanii mbalimbali wakiwemo wajasiriamali, wachoraji, wachongaji, sanaa za ubunifu ni fursa ambayo Tagoane wameileta na kuwataka wasanii waitumie kwaajili ya kujikwamua kiuchumi na kuoata maendeleo katia jamii nzima

Tamasha hilo la Tukuza festival lilizinduliwa rasmi mwaka 2017 likiwa linafanyika kwa mara ya pili limebeba kauli mbiu isemayo toto yatima haihitaji chakula a mavazi peke yake ila awezeshwe nyenzo za kutimiza malengo yake. 

No comments: