Wednesday, December 19, 2018

NMB YATOA MABATI 229 KUPIGA TAFU UJENZI WA WODI YA WAKINA MAMA HOSPITALI YA WILAYA YA MUHEZA

  Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel kushoto akimkabidhi mabati 229 Katibu wa UWT Mkoani Tanga Sophia Nkupe kwa ajili ya ujenzi wa wodi wakina mama hospitali ya wilaya ya Muheza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo
 Katibu wa UWT Mkoani Tanga Sophia Nkupe kulia akimkabidhi 229 Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo mabati 229 kwa ajili ya ujenzi wa wodi wakina mama hospitali ya wilaya ya Muheza kushoto ni Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel
 Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akimkabidhi mabati 229 Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza kwa ajili ya ujenzi wa wodi wakina mama hospitali ya wilaya ya Muheza kushoto ni Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel
  Katibu wa UWT Mkoani Tanga Sophia Nkupe akizungumza katika halfa hiyo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo
  Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel akizungumza katika halfa hiyo
Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza katika halfa hiyo kushoto ni Katibu wa UWT Mkoa wa Tanga Sophia Nkupe na kulia ni Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel
 Meneja wa NMB Tawi la Muheza akizungumza katika halfa hiyo.
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza akizungumza katika Halfa hiyo kushoto ni Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel
 Sehemu ya watumishi wa benki ya NMB wilaya Muheza wakiwa kwenye halfa hiyo
 Sehemu ya wananchi wilaya Muheza wakishuhudia makabidhiano hayo



NA MWANDISHI WETU, MUHEZA.

BENKI ya NMB nchini imetoa mabati 229 kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wakima mama katika hospitali ya wilaya ya Muheza ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt John Magufuli kuhakikisha wananchi wanaondokana na changamoto za afya kwenye maeneo yao.

Halfa ya makabidhiano hayo yalifanyika mjini Muheza na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo akiwemo Katibu wa UWT Mkoani Tanga Sophia Nkupe na Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo.

Akizungumza baada ya kupokea mabati hayo Katibu wa UWT huyo aliishukuru na kuwapongeza benki ya NMB kwa kuwakubalia ombi lao la kuwasaidia mabati kwa sababu wamekuiwa mstari wa mbele kusaidia lakini wanafanya hivyo kuunga mkono juhudui za Rais katika dhamirta yake ya kuhakikisha huduma za afya zinakuwa bora,.

Nkupe alisema pia wana mpongeza Rais Dkt John Magufuli kwa juhudi kubwa anazofanya kuhakikisha wananchi wanaondokana na changamoto mbalimbali ikiwemo za huduma ya afya na nyenginevyo

“Lakini pia nikushukuru Mh DC Mhandisi Mwanasha Tumbo kwa juhudi zako unazozifanya kuhakikisha wilaya ya Muheza inapata maendeleo makubwa pia niwaombe NMB mtusaidie wakina mama kwa sababu tunateseka sana wanachombezwa na taasisi mbalimbali za mikopo yenye riba kubwa”Alisema Katibu huyo wa UWT.

Awali akizungumza wakati akikabidhi msaada huo wa mabati Kaimu Meneja ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel Sadat alisema wameona watoe msaada huo kutokana na ushirikiano mkubwa ambao wamekuwa wakiupata hauna kifani huku wakiupongeza uongozi wa wilaya na Mganga Mkuu wa wilaya hiyo.

Alisema kwa sababu wakati DMO alipoona uwepo wa changamoto hiyo ya jengo la wakima mama hawakuwaza mbali nao na walijua kwamba mkombozi wao ni NMB na hivyo kupeleka maombi yao ambayo yalifanyiwa kazi kwa uhakika hatua iliyowawezesha kunufaika na msaada huo ambao utakuwa chachu kwao .

“Asanteni sana kwa kutupa dhamana hii,mliona mnawadau wa uhakika wa kupeleka kilio chenu,tunatambua juhudi kubwa za serikali hasa ya awamu ya tano zimekuwa na nguvu kuhakikisha watanzania wa kawaida wanaishi maisha ya neema”Alisema Kaimu Meneja huyo

Aidha alisema kwamba benki hiyo haiwezi kuiacha serikali bila kuisaidia wao wapo nao bega kwa bega na jamii popote pale nchini kuhakikisha inapata afya iliyo bora na elimu iliyobora ili neema ya watanzania wote tuweze kuionja.

Naye kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo alisifu juhudi kubwa zinazofanywa na benki hiyo kwa kuwapatia msaada huo na kuwaomba wasiwachoke waendelee kushirikiana nao ili kuhakikisha huduma za afya wilaya humo zinaweza kupatikana kwa urahisi ili kila mmoja anapotaka kupata aweze kufika kwa urahisi na kuweza kuendelea shghuli zao kwa wakati na kuchochea kasi ya maendeleo.    

No comments: