Friday, November 30, 2018

WAHITIMU CHUO CHA USTAWI WA JAMII WASHAURIWA KUTUMIA UJUZI ,UWEZO WALIOUPATA KUSAIDIA JAMII

Na Khadija Seif, Globu ya jami
            
TAASISI  ya Ustawi wa Jamii imewatunuku vyeti wahitimu 1,387 katika mahafali ya 42 ya chuo hicho katika ngazi ya astashahada,stashahada, katika fani ya Kazi za jamii kwa Watoto na vijana,Mahusiano kazini na Menejimenti ya sekta ya Umma( Industrial Relations and Public Management).

Akizungumzana leo jijini Dar es Salaam katika mahafali hayo, Katibu Mkuu - Idara Kuu ya Maendeleo ya jamii -Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dk.John Jingu amesema wahitimu wote wamekula kiapo kwa ajili ya kulitumikia Taifa na ujuzi waliopatiwa ni rasilimali kwa ajili ya Taifa kwa ujumla.

Dk.Jingu ameeleza fani ya ustawi wa jamii ni nyeti na muhimu katika jamii na wanapaswa kuwa katika sekta mbalimbali kwani wamefundishwa kujiajiri na kuajiri watu kwenye kazi. Aidha katika nchi zilizoendelea kuna hitajika kuwa na Ofisa Ustawi na chuo kwa sasa kinatakiwa kuweka wigo mpana kwa ajili ya kuendelea kuzalisha wataalam kwa lengo la kusaidia jamii na manufaa ya nchi kwa ujumla.

Akizungumza na wanahabari Kaimu Mkuu wa  Taasisi, Mipango,fedha na utawala wa tasisi ya ustawi wa jamii Dk.Saliel Kanza ameeleza kuwa taasisi hiyo  ina changamoto kadhaa katika kutekeleza majukumu yake makuu matatu ambayo ni mafunzo,utafiti na kutoa ushauri wa weledi na changamoto hizo ni upungufu wa vifaa vya  Tehama katika kufundishia na kujifunza, uchakavu na upungufu wa Miundombinu ya kujifunza na kufundishia ikiwemo ofisi za walimu,vyumba vya semina,vyumba vya mihadhara(lecture theatre) na zahanati.

Dk.Kanza pia amesema pamoja na ufinyu wa mapato,Taasisi imeendelea kuweka mikakati ya kuboresha mazingira bora ya kusomea kwa kubadilisha matumizi kwa baadhi ya Majengo na kuwa vyumba vya mihadhara.Pia ununuzi wa samani za ofisini na kompyuta ili kusaidia wanafunzi na wahadhiri kujifunza na kufundishia,Kufanya ukarabati wa miundombinu ya taasisi kama vile vyumba vya mihadhara kulingana na uwezo wa kifedha uliopo.

Hata hivyo,mbali na kufanya hayo bado Taasisi Haina uwezo wa kutosha kifedha ili kutatua changamoto tajwa.Kwa upande wa Mwenyekiti wa Bodi ya Magavana Sophia Simba amewapongeza wahitimu hao na kuwataka watumie elimu yao na ujuzi ili kusaidia jamii katika usuluhishi wa Migogoro mbalimbali katika jamii zetu.

Simba amewahusia wahitimu katika fani zote kuwa ni kila nyanja katika jamii inauhitaji wa Ofisa ustawi kwani ni watu wenye ufanisi mkubwa sana katika kutatua,kusuluhisha,kusaidia maeneo yote kwa walemavu,makazini hata Mashuleni.
 Wahitimu wa chuo cha Ustawi wa jamii waliotunukiwa tuzo ya uzamili na Dkt John Jingu wakati wa mahafali hayo leo Jijini Dar es Salaam

No comments: