Tuesday, October 30, 2018

ROCK CITY MARATHON 2018 ILIVYONOGA: Watanzania, Wakenya wang’ara Rock City Marathon

 Mwanariadha Mourice Masima Kutoka Kenya  akimaliza katika nafasi ya kwanza kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza mwishoni  mwa wiki baada ya kutumia  muda wa saa 2:19:14. Kivutio katika mbio hizo ilikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella ambae licha ya kuzindua mbio hizo, alikimbia kikamilifu mbio za km 42 akiambatana na baadhi ya viongozi  waandamizi  wa serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Magu  Dk. Philemon Sengati .
 Mwanariadha Emmanuel Giniki  kutoka Tanzania akimaliza katika nafasi ya kwanza kwenye mbio za km 21 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza leo baada ya kutumia  muda wa 1:04:09 akifuatiwa na Mkenya Daniel Kayioki alietumia muda wa saa 1:04:47.
 Mshindi wa kwanza  mbio za km 42 kwa upande wa wanawake Naomi Jepngetich kutoka Kenya  aliyetumia muda wa saa 02:44:19 kukamilisha mbio hizo.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  (katikati) akishiriki katika mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  (katikati) akishiriki katika mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
 Baadhi ya washiriki wa mbio za Rock City Marathon wakiwa kazini!
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  akimaliza mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  (katikati) akikabidhi zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 4 kwa mwanariadha Mourice Masima Kutoka Kenya  aliemaliza katika nafasi ya kwanza kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza mwishoni  mwa wiki baada ya kutumia  muda wa saa 2:19:14.
 Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Kuhifadhi Mafuta ya TIPER, Bw Emmanuel Kondi akikabidhi  zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 4 kwa mshindi wa kwanza mbio za km 42 kwa wanawake mwanariadha Naomi Jepngetich kutoka Kenya  aliyetumia muda wa saa 02:44:19 kukamilisha mbio hizo. Kulia  ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw John Mongella. TIPER ni moja ya wadhamini wakubwa wa mbio hizo.
 Mwakilishi kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bi. Flora Ndutta akikabidhi  zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 3 kwa mshindi wa kwanza mbio za km 21 mwanariadha Failuna Matanga kutoka Tanzania.
 Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Mwanza (MWAA) Bw Silas Lucas (kulia) akikabidhi zawadi  kwa mshindi wa kwanza mbio za KM 21 Emmanuel Giniki kutoka Tanzania alietumia saa 1:04:09 akifuatiwa na Mkenya Daniel Kayioki alietumia muda wa saa 1:04:47.
 Baadhi ya washiriki wa mbio za km 5 wakimalizia mbio hizo zilizohitimishwa kwenye viunga vya jengo la Rock City Marathon.
 Mmoja wa washiriki wa mbio za KM 3 mahususi kwa ajili ya wazee akiwa kazini
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi wa mbio za km 42 Rock City Marathon kwa upande wa wanawake. Wengine ni pamoja na Mwenyekiti wa mbio hizo Bw Zenno Ngowi  (wa tatu kulia), Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Kuhifadhi Mafuta ya TIPER, Bw Emmanuel Kondi (Kulia kwa Mkuu wa Mkoa) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Mwanza (MWAA) Bw Silas Lucas.
Mkuu wa Wilaya ya Magu  Dk. Philemon Sengati (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi wa mbio za km 5 kwa upande wa watu wenye ualibino.

Katika mashindano hayo ilishuhudiwa washiriki ambao pia ni wadhamini wa mbio hizo kutoka  makampuni ya Puma Energy Tanzania, Tiper,Rock City Mall,  NSSF, Gold Crest, New Mwanza Hotel,  CF Hospital, Coca Cola, Metro Fm, EF Outdoor,  KK Security, Belmont Fairmount Hotel , Bigie Customs na Global Education Link wakishiriki kikamilifu katika mbio za KM 5 sambamba na watu wenye ulemavu wa ngozi yaani Albino.

1 comment:

William said...

If you are searching for genuine QuickBooksCustomer Service Number dial QuickBooks Number 855-756-1077 for immediate help .Our QuickBooks Number is available 24*7.