Thursday, September 20, 2018

VIJANA 4200 NCHINI KUNUFAIKA MRADI WA KILIMO KUPITIA KITALU NYUMBA

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Bunge, Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe. Anthony Mavunde akimwagilia bustani ya kijana Matogolo Samwel wa Kijiji cha Mwamanyili wilayani Busega, wakati wa Ziara ya kukagua maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa vitalu nyumba mkoani Simiyu.

Na Stella Kalinga, Simiyu

Vijana takribani 4200 hapa nchini wanatarajia kunuafaika na kilimo kupitia mradi wa kitalu nyumba(green house), ambao utaanza kutekelezwa katika mikoa sita ambayo imekuwa kinara kwa kutenga maeneo kwa ajili ya shughuli za vijana, ukiwemo mkoa wa Simiyu na Halmashauri zake zote sita. Hayo yamesemwa na Naibu Waziri , Ofisi ya Waziri Mkuu,  Sera, Bunge,  Kazi ,Vijana Ajira  na Walemavu Mhe. Anthony Mavunde hiyo wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu yenye lengo la kukagua maeneo ya ujenzi wa vitalu nyumba na uwepo wa maji yatakayotumika katika  kilimo cha umwagiliaji.

Mvunde amesema katika kutekeleza mradi huo vijana watawezeshwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ili iwe sehemu ya ajira yao, ambapo vijana watafundishwa kulima kwa tija kupitia kitalu nyumba na kujua namna ya kutengeneza vitalu nyumba na wananchi wengine wanapohitaji kujifunza namna ya kutengeneza vitalu nyumba wajifunze kwao.

“Tutaleta green house (Kitalu nyumba) ambayo itafungwa hapa na vijana wataelekezwa kulima kupitia huko, lakini pia tutawaunganisha na chama cha Wauza mboga Tanzania kwa ajili ya kutengeneza masoko ya uhakika ili green house (kitalu nyumba) hizo ziwe na tija” alisema Naibu Waziri Mavunde
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Bunge, Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe. Anthony Mavunde akikagua eneo litakalotumika kujenga vitalu nyumba Halmashauri ya Mji wa Bariadi katika Viwanja vya Nanenane Nyakabindi, wakati wa ziara yake ya kukagua maeneo hayo mkoani Simiyu.

Akiwa katika ziara yake Naibu Waziri huyo amekutana na baadhi ya vijana ambao watatekeleza mradi huo na kuwapongeza kwa uamuzi waliochukua na akatoa rai kwa vijana wote nchini kuachana kukaa vijiweni na badala yake wajishughulishe na teknolojia hiyo ili waondokane na umasikini. Akiwa wilayani Busega, Bariadi na Itilima Mavunde ameeleza kuridhishwa kwake na maeneo yaliyotengwa na akatoa wito kwa viongozi wote kuwalea vijana wote watakaoanza kutekeleza mradi huo ili mradi huo uweze kuwa endelevu na uweze kuwaletea tija.

Mkuu wa Mkoa wa Mhe. Anthony Mtaka  ameishukuru Serikali kwa mpango huo ambao utawasaidia vijana kujiajiri kupitia vitalu nyumba na akamhakikishia Naibu Waziri kuwa mkoa wa Simiyu utahakikisha vijana wanafanya vizuri katika mradi huo

Mkuu wa wilaya ya Itilima amesema pamoja na vijana wilayani humo kujiandaa na mradi wa kilimo kwa kutumia kitalu nyumba Wilaya hiyo pia imeweka mpango wa kutoa mafunzo ya ujasiriamali na ufundi stadi yatakayowawezesha kupata maarifa ya namna ya kufanya shughuli za ujasiriamali na ufundi kama ajira zao.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Mhandisi. Mohammed Ali akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Bunge, Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe. Anthony Mavunde(mwenye miwani) juu ya eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Kitalu nyumba lililopo Mwamanyili, wakati akiwa katika zi ara ya kukagua maeneo hayo mkoani Simiyu.

Kwa upande wao vijana watakaofaidika na mradi wa kitalu nyumba wamesema wanaupokea mradi huo kwa mikono miwili na wakaomba Serikali iwasaidie kupata mikopo ili waweze kununua vifaa vya kisasa hususani mashine na zana za kilimo zitakazowawezesha kutekeleza mradi huo.

“Mradi huu sisi vijana tunaupokea kwa mikono miwili ombi letu kwa serikali tusaidiwe mikopo itakayotuwezesha kupata mtaji utakatufanya vijana tunufaike na kilimo, tupate vifaa bora kama mashine za kumwagilia na zana nyingine za kilimo ili tuweze kulima kisasa” alisema Matogolo Samwel kutoka Mwanyili wilayani Busega.

Katika ziara hiyo Mavunde ametembelea Halmashauri ya wilaya ya Busega, Halmashauri ya Mji wa Bariadi katika  viwanja vya nane nane Nyakabindi na Halmashauri ya Wilaya ya Itilima makao makuu ya Wilaya Lagangabilili.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Bunge, Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe. Anthony Mavunde( wa pili kulia mbele) akizungumza na viongozi na baadhi ya Vijana wa Itilima, alipotembelea eneo la ujenzi wa Vitalu Nyumba Lagangabilili akiwa katika ziara ya kukagua maeneo hayo mkoani Simiyu.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Bunge, Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe. Anthony Mavunde akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu(baadhi hawapo pichani) mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi kwa ajili ya ziara ya kukagua maeneo yaliyotengwa kujenga vitalu nyumba mkoani humo, (kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza wakati ziara ya Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Bunge, Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe. Anthony Mavunde, aliyofanya mkoani humo kwa ajili ya kukagua maeneo ya kujenga vitalu nyumba.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Bunge, Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe. Anthony Mavunde(mwenye miwani), Mbunge wa Itilima, Mhe. Njalu Silanga(katikati) na Mkuu wa Wilaya ya  Itilima, Mhe. Benson Kilangi(kulia) wakifurahia pamoja na wanafunzi wa Shule ya sekondari Kanadi na baadhi ya viongozi wa Mkoani Simiyu wakati Naibu Waziri Mavunde akiwa katika ziara ya kukagua maeneo ya kujenga vitalu nyumba mkoani Simiyu.

No comments: