Sunday, September 30, 2018

“TAA KUIFUNGUA TANZANIA KWA ULIMWENGU”

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (kushoto) akiongea na waandishi kuhusiana na viwanja vya ndege kuchagiza uingiaji wa watalii nchini. Kulia na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Prof. Audax Mabula.



Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), imejipanga kupitia kaulimbiu yake kuifungua Tanzania kwa ulimwengu kupitia sekta ya Utalii nchini, kwa kuimarisha usafiri wa anga ili kuhakikisha watalii wote wanafikia vivutio vyote vya utalii kwa haraka zaidi.

Hayo yamebainishwa juzi na Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw. Richard Mayongela alipokuwa akizumgumza na waandishi wa habari siku ya ushiriki wa Mamlaka katika Tamasha la Urithi Wetu linaloanza leo Jumatatu (Oktoba Mosi, 2018) kwa Mkoa wa Dar es Salaam.

“Viwanja vyetu vya ndege ndio milango mikuu wa watalii kupita, hivyo tupo hapa kuwaambia wananchi, wadau pamoja na Jumuiya za Kimataifa kwamba sasa kuna fursa ya kutanganza vivutio vya kitalii kupitia viwanja vyetu vya ndege kwa kuwa vinatumika kwa usafiri wa anga lakini pia tunaweza kuvitumia kibiashara kwa kutangaza vivutio vyetu” alisema Bw. Mayongela.

Bw Mayongela pia amewapa wito Watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii kutangaza vivutio vilivyopo kupitia Viwanja vya ndege lakini pia kuwaeleza wadau kwa njia mbalimbali zilizopo Tanzania ili watalii wanapowasili waweze kupata picha halisi ya maeneo ya kutembelea akiwa nchini.

Aidha Bw. Mayongela ameongeza kwamba Mamlaka ina mtandao mkubwa na inasimamia viwanja 58 vilivyopo chini ya serikali, ambavyo vipo kila sehemu penye vivutio vya utalii na wamejiimarisha kuhakikisha huduma bora ya usafiri wa anga.

“Sehemu ya Kaskazini mwa nchi yetu ambapo ndio kuna vivutio vingi, vipo viwanja vya ndege vya kutosha, tuna Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA), Kiwanja cha Lake Manyara ambacho kimejengwa kwa mkakati wa kutumika kwa watalii na kinafanya vizuri sana kwa kuingiza watalii wengi, vilevile tuna mpango wa kujenga kiwanja kipya katika Mkoa wa Manyara,” alibainisha Bw. Mayongela.

Akizungumzia miundombinu ya Viwanja vya Ndege kwa Kanda ya Kusini ameeleza kwamba serikali imejitoa kufanya maboresho ya kiwanja cha Mtwara kwa lengo moja kuu la kuvutia watalii wengi zaidi ili waweze kushuhudia vivutio vya utalii vilivyopo maeneo hayo.

“Serikali inaboresha kwa kufanya upanuzi na ukarabati mkubwa wa Kiwanja Cha Ndege cha Mtwara, pamoja na sababu za kiuchumi lakini pia lengo ni kuvutia watalii wengi zaidi ili waweze kushuhudia vivutio vilivyopo, sio hivyo tu lakini pia Kilwa masoko tuna kiwanja, Lindi tuna kiwanja, Nachingwea mpaka Masasi kote tuna viwanja” Alisema Bw. Mayongela.

Akizungumzia upande wa nyanda za juu Kusini Bw. Mayongela amebainisha kwamba baada ya ukarabati mkubwa kukamilika kutakuwa na kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Songwe, Njombe mpaka Iringa kutakuwa na viwanja vizuri vya ndege ili kuhakikisha kwamba vivutio vilivyopo Tanzania vinafikika kwa urahisi.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Prof Audax Mabula ameeleza kwamba Tamasha la Urithi Wetu lililobuniwa na Wizara ya Maliasili na Utalii lina madhumuni makuu mawili ikiwemo ya kuwezesha kuonyesha fursa zote zinazoizunguka tasnia hii.

“Madhumuni makuu ni kuendeleza, kutambua na kuhifadhi urithi wetu wa utamaduni kwa ajili ya kizazi kilichopo na kinacho kuja lakini pili ni kubadili urithi wetu wa utamaduni kuwa zao la utalii hayo ndio malengo makuu mawili” alisema Prof Mabula.

TAA wametoa msaada wa fulana 100 kwa ajili ya washiriki wa tamasha la Urithi Wetu, ambalo litafikia tamati Oktoba 6, 2018 kwa kufungwa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa.
a Iringa wakati akifanya majumuisho ya ziara yake mkoani humo inayokwenda kwa jina la "Iringa Mpya" ambapo watedaji kutoka wilaya zote na wataalam walijumuika pamoja katika mkutano huo.

No comments: