Monday, August 6, 2018

JASINTA MBONEKO AKIAPISHWA KUWA MKUU WA WILAYA YA SHINYANGA

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Zainab Telack amemuapisha Jasinta Venant Mboneko kuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga leo Jumatatu Agosti 6,2018.


Na Kadama Malunde – Malunde1 blog
Hafla fupi ya kuapishwa kwa mkuu huyo mpya wa wilaya ya Shinyanga imefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali,vyama vya siasa,taasisi na wadau mbalimbali.
Akizungumza baada kula kiapo,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,mheshimiwa Jasinta Venant Mboneko alisema amekuja wilayani humo kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na kusimamia Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

“Namshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuniamini kuwa na mimi kuwatumikia wananchi wa Shinyanga,nipo tayari kuwatumikia wananchi na nitaendelea kuisimamia ilani ya uchaguzi ya CCM na kuhakikisha tunaifanya wilaya ya Shinyanga kuwa salama”,alisema Mboneko.
“Nimekuja Shinyanga kufanya kazina tumeelekezwa kuwatumikia wananchi,kazi hii sitaifanya peke yangu,wapo watu wataniwezesha ikiwemo kamati ya ulinzi na usalama lakini pia viongozi wa Chama Cha Mapinduzi ,viongozi wa dini pamoja na wananchi,naomba mwenyezi Mungu anisaidie sana na aniwezeshe”,aliongeza.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack alimtaka mkuu huyo wa wilaya na viongozi wengine kufanyia kazi malalamiko ya wananchi na kuepuka urafiki katika kazi.

“Mwananchi akilalamika msikilize,hakikisha unafanyia kazi kila jambo linalokuja mbele yako,Shinyanga iko salama,naomba tushirikiane kufanya kazi”,alisema Telack.

“Najua utapata watu wengi wa kukukaribisha,kuwa makini na watu wanaokukaribisha,hizi kazi zetu hazina urafiki,nikumbushe tu kwamba mishahara mnayopewa na serikali inatosha msikubali kupewa rushwa”,aliongeza.
Kulia ni Jasinta Venant Mboneko akila kiapo kuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga leo Jumatatu Agosti 6,2018 - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Jasinta Venant Mboneko akila kiapo kuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akisaini hati ya kiapo
Kushoto Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akishikana mkono na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Venant Mboneko baada ya kumkabidhi katiba ya nchi,ilani ya CCM na kanuni ya maadili ya utumishi wa umma.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Venant Mboneko akiwa na wazazi wake
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Venant Mboneko akizungumza baada ya kula kiapo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Venant Mboneko akiomba ushirikiano kutoka kwa viongozi na wananchi wilayani Shinyanga
Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Venant Mboneko 
Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga Albert Msovela akizungumza ukumbini
Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha,akifuatiwa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Venant Mboneko,Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack na Mkuu wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Talaba wakiwa ukumbini
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akizungumza baada kumuapisha Jasinta Mboneko kuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga
Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Shinyanga Bakari Mohamed Kasinyo na Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi (kushoto) wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea ukumbini
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akizungumza ukumbini
Askofu David Mabushi akitoa neno ukumbini
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Charles Sangura akitoa neno
Mkuu wa wilaya ya Kahama, Anamringi Macha akizungumza ukumbini
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Talaba akizungumza ukumbini
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack,Katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya za Kahama,Shinyanga na Kishapu
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack,Katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Shinyanga
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa,katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Shinyanga
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa,katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na wazazi wa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa,katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na kamati ya ulinzi na familia ya Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa,katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na kamati ya ulinzi na viongozi wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa, katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na kamati ya ulinzi na viongozi wa dini
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa,katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na sekretarieti ya mkoa wa Shinyanga
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa,katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na viongozi wa taasisi mbalimbali
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa,katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na viongozi wa taasisi mbalimbali
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa,katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na waandishi wa habari
Picha ya pamoja mkuu wa mkoa,katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya na waandishi wa habari
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Venant Mboneko akiteta jambo na ndugu yake

ANGALIA PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI UKUMBINI


Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

No comments: