Wednesday, August 1, 2018

BALOZI MPYA WA KENYA AKARIBISHWA NCHINI TANZANIA

Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumkaribisha rasmi nchini, iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam Julai 31, 2018. Kulia ni Mke wa Balozi Kazungu, Bi. Mapenzi Kazungu.
Kiongozi wa Mabalozi nchini na Balozi wa Rwanda, Eugene Kayihura akizungumza jambo kwa niaba ya Mabalozi wengine, wakati wakimkaribisha Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu, katika dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumkaribisha rasmi nchini, iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam Julai 31, 2018. 
Kaimu Balozi wa Kenya nchini, Boniface Muhia akizungumza katika dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumkaribisha rasmi nchini Balozi mpya wa Kenya, Dan Kazungu, iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam Julai 31, 2018. 
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu (kushoto) akiwa katika mazungumzo yenye furaha na baadhi ya maafisa wa Ubalozi wa Kenya hapa nchini, wakati hafla fupi ya kumkaribisha Balozi huyo, iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam Julai 31, 2018.

Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akimkaribisha Kiongozi wa Mabalozi nchini na Balozi wa Rwanda, Eugene Kayihura wakati walipowasili kwenye hafla fupi ya kumkaribisha Balozi huyo, iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam Julai 31, 2018. Kulia ni Mke wa Balozi Kazungu, Bi. Mapenzi Kazungu.














No comments: