Friday, July 6, 2018

NSSF WATOA MSAADA WA ZAIDI YA MILIONI 4.5 MANISPAA YA IRINGA NA HALMASHAURI YA IRINGA

Na Francis Godwin, MichuziBlog Iringa 

MFUKO  wa   hifadhi ya  jamii (NSSF)  umetoa  msaada  wa  mashuka 300 yenye  thamani ya  zaidi ya  shilingi  milioni 4.5  kwa  Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa  na  halmashauri ya  Iringa mkoani  Iringa  kwa ajili ya  kusaidia hospitali  ,zahanati na  vituo  vya afya vyenye upungufu wa mashuka ya  wagonjwa.
Akikabidhi  msaada  huo  leo  meneja  wa  NSSF  mkoa  wa Iringa  Josephat  Komba  alisema  kuwa NSSF  imetoa msaada  huo  ikiwa ni  sehemu ya  utekelezaji  wa maombi yaliyotolewa na  Halmashauri  hizo  kwa  NSSF  kuomba  kusaidiwa msaada wa mashuka.
Komba  alisema kuwa NSSF  kama  mfuko  wa  hifadhi ya jamii  unayojukumu  la kuendelea  kuunga mkono  jitihada  za  Halmashauri  nchini  katika  kutoa  huduma  za  afya na  pia  unaendelea  kuunga  mkono   jitihada  za  serikali ya  awamu ya  tano  chini ya  Rais Dkt  John Magufuli  kuona  sekta ya  afya  inaendelea  kuboreshwa  zaidi.
Kwani  alisema  NSSF pamoja  na majukumu mengine itaendelea  kuwa karibu na  jamii ya kitanzania kwani hatua  ya  waajiri kuwaunganisha  wafanyakazi wao na  NSSF  ni kutaka  kuona  maisha yao  yanaendelea  kuboreshwa  zaidi  hivyo  jukumu lao kuona  NSSF  inaendelea kuunga mkono azima ya  serikali katika  uboreshaji wa  huduma  za afya.
Alisema kuwa NSSF  ilipokea  maombi  kutoka katika  Halmashauri ya  Manispsaa ya  Iringa na Halmashauri ya  Iringa  kuomba kusaidiwa msaada  wa mashuka kwa ajili ya wagonjwa na pasipo kuchelewa  wametimiza maombi hayo.
"  NSSF  imekuwa  ikisaidia   katika  huduma  mbali mbali  za  kijamii pamoja na  kusaidia  Halmashauri  ila pia  wamekuwa  wakisaidia  huduma ya matibabu kwa  wanachama wake  bure  pamoja na familia  zao ili mradi  awe mwanachama wao  ".
Alisema   kuwa  sehemu ya  kuunga  mkono  kasi ya  wanachama  kujiunga nakuwekeza katika  NSSF  ni pamoja na  NSSF  kuunga  mkono  jitihada  zinazofanywa na  Halmashauri  katika  uboreshaji  wa Afya  na  wataendelea  kufanya  hivyo.
Komba alisema kuwa hospitali ya  Manispaa ya Iringa  Frelimo  iliomba  msaada  wa mashuka  200 na  halmashauri ya  Iringa  iliomba mashuka  100  na  NSSF  imetoa mashuka  yote kama  Halmashauri  zilizoomba  japo  itaendelea  kusaidia  mahitahi mengine  kulingana na maombi na  upatikanaji  wa  pesa.
Kwa upande  wake  kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa Omary  Mkangama  alipongeza  msaada  huo  wa NSSF  katika  Hospitali ya  Frelimo na  kuomba  ushirikiano  huo  kuendelea  zaidi .

Alisema  kuwa Hospitali  hiyo  imekuwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ya mashuka  ambayo imetatuliwa na  NSSF  na  ile ya  mashine ya  kufulia  nguo  na  chumba cha  kufulia nguo  iliyotekelezwa na CCM wilaya ya  Iringa mjini.
kaimu mganga mfawidhi  wa hospitali ya  Frelimo Dr Benjamin Mhanga  alisema kuwa  Hospitali  hiyo inakabiliwa na  changamoto mbali mbali  ikiwemo ya  upungufu wa majengo  kama  la kulaza wagonjwa  akina mama ,watoto ,magonjwa ya  kuambukiza ,chumba  cha kuhifadhia maiti  na  jengo la  wanawake pamoja na  vifaa tiba.
Huku  kwa upande  wake mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Robert Masunya mbali ya kupngeza NSSF kwa  kusaidia  msaada wa mashuka bado alisema  Halmashauri  hiyo inahitaji  mashuka  zaidi pamoja na  vitanda kwa  ajili ya vituo  vya  afya ,zahanati na Hospitali ya  wilaya  na kuwa  zaidi ya mashuka .

Kuwa  kuna  vituo  vya  afya  10 ,Hospitali teuli  moja na  zahanati ambapo  hitahji  zima ni shuka zaidi ya 1560 zinahitajika  hivyo  msaada  huo wa  shuka 100  umepunguza sehemu ya  hitaji ya  changamoto  hiyo.

Hivyo  alisema kupitia  mbunge wa  jimbo la  Ismani Wiliam  Lukuvi wameendelea  kutafuta  wahisani  kwa ajili ya  kutatua tatizo  hilo kwa  kutafuta wadau  wakiwemo  NSSF  ambao  wamejitolea  msaada  huo  wa mashuka ambayo yatakwenda Kalenga na  jimbo la  Isimani .

Meneja  wa NSSF  mkoa wa  Iringa Josephat  Komba(kushoto) akimkabidhi msaada wa  shuka  200  kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa Omary  Mkangama  kwa  ajili ya  Hospitali ya  Frelimo 
 Wafanyakazi wa  hospitali ya  Frelimo wakitandika  mashuka  yaliyotolewa na  NSSF 
 Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Iringa Robert Masunya (kulia )  akishukuru kwa msaada wa  NSSF 
 Meneja  wa  NSSF  mkoa wa Iringa Josephat  Komba  akielezea msaada wa  uliotolewa na  NSSF  katika Halmashauri  za  Iringa
  Mashuka  yaliyotolewa na  NSSF 

 Wafanyakazi wa hospitali ya Frelimo  wakifuatilia tukio  hilo 
Meneja  wa NSSF  mkoa wa  Iringa Josephat  Komba  (kushoto ) akimkabidhi msaada  wa mashuka  100 mkurugenzi wa  Halmashauri ya  Iringa Robert Masunya. Picha na Francis Godwin, Michuzi Blog, Iringa

No comments: