Tuesday, June 26, 2018

MNADHIMU MKUU WA JWTZ KIHANGAIKO BAGAMOYO PWANI

MNADHIMU Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Yacoub Mohamed amewaonya askari wapya wa jeshi hilo kutojiingiza katika masuala ya siasa.

Aidha hakusita kuwapa tahadhari zaidi kwamba atakayebainika atachuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwano kufukuzwa jeshini.

"Jeshini hakuna siasa, hapa mnaenda kutekeleza Katiba ya nchi, jukumu lenu kubwa ni kulinda mipaka ya nchi, Katiba na maelekezo kutoka kwa viongozi wenu," alisema Luteni Jenerali Mohamed.Mafunzo hayo yalihusisha vijana 2,253 yalifanyika kwa miezi 4 katika Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi (RTS), Kihangaiko iliyopo Bagamoyo Pwani.

Kwa upande Kaimu Mkuu wa Shule hiyo Kanali Sijaona Myala alisema kazi ya jeshi ni kuandikisha askari kwa ajili ya kulinda mipaka ya nchi na vita."Kazi ya jeshi ni kuandikisha askari na si ajira, ikitokea vita hata hawa wote wakifa, tutaandikisha wengine," alisema Kanali Myala.


Mbali ya kufungwa kwa mafunzo hayo, askari waliohitimu walionyesha maonyesho ya ukakamavu, sarakasi na vikwazo.
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Yacoub Mohamed akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufunga mafunzo ya awali ya keshi kwa askari wapya 2253 yaliyokuwa yakifanyika katika Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi (RTS), Kihangaiko iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani. 
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Yacoub Mohamed akikagua gwariide la askari wapya wa JWTZ waliomaliza mafunzo yao ya awali katika Shule ya Kijeshi RTS Kihangaiko iliyopo Bagamoyo, Pwani nyuma mwisho ni Kaimu Mkuu wa Shule hiyo Kanali Sijaona Myala.
Maofisa wa JWTZ wakiongoza Gwaride wakati wa kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa askari wapya 2,253 yaliyofanyika Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi RTS Kihangaiko Bagamoyo mkoani Pwani. 
Kaimu Mkuu wa Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi RTS Kihangaiko Kanali Sijaona Myala akimuongoza Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Yacoub Mohamed kupanda jukwaani mara baada ya kukagua gwaride la askari wapya 2253 waliomaliza mafunzo yao ya wali chuoni hapo. 
Mwalimu wa moja ya michezo ya ukakamavu akionyesha namna ya kupita chini ya moto wakati wa maonyeshi yaliyofanyika chuoni hapo.
Askari wapya wakipimana nguvu kwa kuzichapa mbele ya mgeni rasmi Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Lutena Jenerali Yacoub Mohamed aliyefunga mafunzo ya awai ya askari hao 2,253 yalifanyika Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijesjhi (RTS) Kihangaiko Bagamoyo Pwani. 
Askari wapya wakimsikiliza mgeni rasmi Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Yacoub Mohamed alipokuwa akizungumza nao kabla ya kufunga mafunzo yao ya kundi la 38A/17 lililokuwa na askri 2253. 
Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Yacoub Mohamed katikati akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa jeshi waliopop kazini pamoja na wastaafu wakati wa kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa askari 2253 yaliyofanyika Shule ya Mafunzo ya Aawali ya Kijeshi RTS Kihangaiko Pwani. 
Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Yacoub Mohamed wa kwanza kushoto akijadiliana jambo na maofisa wa JWTZ mara baada ya kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa wanahitimu 2253 yaliyofanyika Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi RTS Kihangaiko Bagamoyo mkoani Pwani

No comments: