Monday, June 18, 2018

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Yafana Muhimbili

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambako maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanafaniyika kwa siku tatu mfulilizo. Wananchi mbalimbali wamefika kwa wingi katika hospitali hiyo kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali zinazotolewa na hospitali hiyo pamoja na kupima afya bure. Kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Muhimbili, Bw. Juma Muhimbi na Mkurugenzi wa Tiba katika wizara hiyo, Dkt. Doroth Gwajima.
Wananchi mbalimbali wakiwamo wataalamu wa MNH wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu wakati akizungumza kwenye viwanja vya Muhimbili.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Figo, Dkt. Onesmo Kisanga akifafanua jambo kwa Waziri Ummy Mwalimu kuhusu magonjwa ya figo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Prof. Lawrence Museru wakati kulia ni mjumbe wa bodi ya Muhimbili, Bw. Juma Muhimbi.
Bw. Paul Mayengo akipima dawa ya methadone kwa watu wenye tatizo la uraibu wa heroin katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Dawa hiyo inatumiwa na wataalamu wa afya kwa ajili ya kutibu uraibu.
Prisca akimweleza waziri kuhusu maendeleo yake baada ya kupandikizwa figo katika hospitali hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Mahonjwa ya Figo, Dkt. Jacqueline Shoo.
Waziri Ummy Mwalimu akiwa kwenye banda la lishe ambako ampatiwa maelezo kuhusu lishe bora. Kushoto ni mmoja wa watu akipimwa afya baada ya kutembelea banda hilo leo.
Ofisa Ustawi wa Jamii wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), John Mwakyusa akitoa huduma ya ushauri kwa mmoja wa watu waliotembelea banda hilo.
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akimsikiliza Msimamizi wa wodi ya Kangaroo, Cleopatra Mtei jinsi ya kuwabeba watoto wanaozaliwa kabla ya muda (premature).
Mtoto, Mnyaman Omary Mohammed akizungumza na Waziri Ummy Mwalimu leo katika viwanja vya Muhimbili ambako maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yanaendelea.
Mkuu wa Idara ya Afya ya Akili, Dkt. Frank Masao akieleza shughuli mbalimbali za tiba zinazofanywa na idara hiyo.

No comments: