Sunday, May 6, 2018

TULIA AWASHUKURU WADHAMINI KWA KUFANIKISHA MBIO ZA 'MBEYA TULIA MARATHON 2018'.

SE3
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Dk. Tulia Ackson akizungumza mara baada ya kukamilika kwa mbio za Mbeya Tulia Marathon 2018 zilizofanyika kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya leo, Mbio hizo Zimeshirikisha wanariadha mbalimbali wakiwemo wakenya na watanzania pamoja na viongozi mbalimbali na wananchi wa mkoa wa Mbeya , kumekuwepo na washiriki wa mbio mbalimbali zikiwemo za Kilomita 41, kilomita 21, Kilomita 5, Kilomita 2, Mita 100, Mita 400 na Mita 800.
Dk. Tulia Akson Naibu Spika wa Bunge amewashukuru wadhamini mbalimbali ambao wamewezesha kufanyika kwa mbio hizo kwa mafanikio makubwa mbali ya changamoto ndogondogo ambazo zitaendelea kuboreshwa katika maandalizi ya mbio zingine zitakazofanyika mwakani jijini Mbeya.
SE4
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Dk. Tulia Ackson akihojiwa na Mtangazaji wa Kituo Cha Luninga cha Clouds TV Hassan Ngoma kuhusu mafanikio ya mbio hizo za Mbeya Tulia Marathon 2018.
SE5
Mmoja wa wananchi waliohudhuria ili kushuhudia mbio hizo akisoma kipeperushi cha Bahati nasibu ya Mzuka huku akifurahia jambo katika kipeperushi hicho.
1
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Dk. Tulia Ackson akianzisha Mbio za mita 100 katika mashindano ya Mbeya Tulia Marathon 2018 zilizowahusisha viongozi wa serikali , Wabunge na Madiwani kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya leo,
2
Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mbeya Ndg Wilson Nkambaku pamoja na baadhi ya wabunge wakishiriki mbio za mita 100 kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya wakati wa mashindano ya Mbeya Tulia Marathon 2018 jijini Mbeya.
3
Watoto wakishiriki mbio za mita 1500.
4
Baadhi ya wananchi wakifuatilia matukio hayo.
5
Washiriki wa mbio za Baiskeli Kilomita 150 wakiingia uwanja wa Sokoine mara baada ya kumaliza mbio hizo.
7
Wananchi wakifuatilia matukio.
SE1
Afisa Mkuu wa Masoko, wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya mabalozi wa Tatu Mzuka na maofisa wa Tatu Mzuka Kulia ni Barbara Hassan Matangazaji wa Clouds Radio na Mwanamuziki wa Bongo Fleva Fid Q.
8
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Dk. Tulia Ackson akicheza Muziki wa Kwaito pamoja na baadhi ya wabunge na viongozi wa Serikali.
9
Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice Tanzania Bw. Maharage Chande akikabidhi king'amuzi na Dishi kwa washindi mbio za Kilomita 21. wanawake.
12
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Dk. Tulia Ackson akifurahia jambo wakati Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice Tanzania Bw. Maharage Chande akizungumza kwenye uwanja wa Sokoine mara baada ya kumalizika kwa mbio hizo.
13
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Dk. Tulia Ackson akifurahia jambo wakati Afisa Mkuu wa Masoko, wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga akizungumza kwenye uwanja wa Sokoine mara baada ya kumalizika kwa mbio hizo.
14
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Dk. Tulia Ackson akisikiliza wakati Mkuu wa Mkoa wa Simiyu na Rais wa Chama cha Riadha Tanzania RT Mh. Anthony Mtaka akizungumza .
15
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh. Amos Makala akielezea jambo wakati alipokuwa akisifu umakini wa Naibu Spika Tulia Akson na kazi kubwa anayoifanya kusaidia jamii kupitia mfuko wa Dk. Tulia Trust.
16
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh. Amos Makala na Naibu Spika Dk.Tulia Akson wakipiga picha ya pamoja na washindi wa mbio za kilomita 21.
17
Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice Tanzania Bw. Maharage Chande akiwavisha medali washindi wa mbio za kilomita 41.
18
Mkurugenzi Mtendaji wa Multchoice Tanzania Bw. Maharage Chande na Naibu Spika Dk. Tulia Akson pamoja na Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makala wakipiga picha ya pamoja na washindi mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao.
19
Baadhi ya washindi wa mbio hizo wakipiga picha huku wakiwa wameshika zawadi zao za ving'amuzi.

No comments: