Saturday, April 21, 2018

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWEKA JIWE LA MSINGI LA MRADI WA UJENZI WA MAGHALA NA VIHENGE VYA KISASA MJINI DODOMA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na balozi wa Poland nchini, Mhe. Krzysztof Buzalski wakati alipowasili kwenye viwanja vya magahla ya Wakala wa Hifadhi yaTaifa ya Chakula chino (NFRA) kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa magahala na vihenge vya kisasa, eneo la Kizota mjini Dodoma Aprili 21, 2018. Wapili kushoto ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba , kushoto ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt, Mary Mwanjelwa na kulia ni Mjumbe wa bodi ya kampuni ya Freerum ya Poland, Bw. Piotr Wielesik.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na balozi wa Poland nchini, Mhe Krzysztof Buzalski wakati alipoweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa maghala na vihenge vya kisasa katika eneo la Kizota mjini Dodoma Aprili 21, 2018.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwemo wabunge na Wakuu wa Mikoa wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati aliopozungumza kabla ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa magahala na vihenge vya kisasa kwenye eneo la Kizota mjini Dodoma Aprili 21, 2018.
Spika wa Bunge, Mhe.Job Ndugai akizungumza Katika sherehe ya uwekaji jiwe la msingi la maghala na vihenge vya kisasa kwenye eneo la Kizota mjini Dodoma, Aprili 21, 2018. Mgeni rasmi alikuwa ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipoweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa magahala na vihenge vya kisasa katika eneo la Kizota mjini Dodoma Aprili 21, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwaongoza viongozi kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa maghala na vihenge vya kisasa kwenye eneo la Kizota mjini Dodoma Aprili 21, 2018. Kutoka kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, Spika wa Bunge, Job Ndugai, Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Dodoma, Godwin Mkanwa, Balozi wa Poland nchini, Mhe. Krzystof Buzalski na kulia Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi walioshiriki kwenye sherehe ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa maghala na vihenge vya kisasa kwenye eneo la Kizota mjini Dodoma, Aprili 21, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na balozi wa Poland nchini, Mhe Krzysztof Buzalski baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa magahala na vihenge vya kisasa katika eneo la Kizota mjini Dodoma Aprili 21, 2018. Watatu kulia ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba , kushoto ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt, Mary Mwanjelwa na wapili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bilinith Mahenge.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments: