Thursday, April 26, 2018

RAIS WA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA AKUNWA NA KASI YA RAIS MAGUFULI

Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika -AfDB, Dkt. Akinumwi Adesina (katikati) akiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambapo pia anatarajiwa kuhudhuria Maadhimisho ya Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mjini Dodoma. kulia ni mwenyeji wake, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.


Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango (kulia) akiwa na mgeni wake Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika -AfDB, Dkt. Akinumwi Adesina, wakiingia kwenye jengo la watu mashuhuri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya Rais huyo kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kufuatia mwaliko wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambapo pia anatarajiwa kuhudhuria Maadhimisho ya Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, mjini Dodoma 
Sehemu ya ujumbe wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), ukiwa katika chumba cha wageni Mashuhuri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam ukiwa na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika -AfDB, Dkt. Akinumwi Adesina (hayupo pichani) aliyewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambapo pia anatarajiwa kuhudhuria Maadhimisho ya Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mjini Dodoma. 
MKURUGENZI Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro, akizungumza jambo wakati Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika -AfDB, Dkt. Akinumwi Adesina (kushoto) akiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambapo pia anatarajiwa kuhudhuria Maadhimisho ya Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mjini Dodoma. Katikati ni Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb).
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika -AfDB, Dkt. Akinumwi Adesina (kulia) akisisitiza jambo alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam na kupokelewa na mwenyeji wake Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambapo pia anatarajiwa kuhudhuria Maadhimisho ya Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mjini Dodoma. kulia ni mwenyeji wake, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango. 
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika -AfDB, Dkt. Akinumwi Adesina (kulia) na mwenyeji wake Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) wakigonga “tano” wakati wa mazungumzo yao wakati rais huyo alipowasili nchini kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambapo pia anatarajiwa kuhudhuria Maadhimisho ya Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mjini Dodoma.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika -AfDB, Dkt. Akinumwi Adesina (kushoto) na mwenyeji wake Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) wakiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambapo pia anatarajiwa kuhudhuria Maadhimisho ya Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mjini Dodoma. 



Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam

Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, DKT. AKINUMWI ADESINA, ameanza ziara ya kikazi ya siku tatu hapa nchini kwa mwaliko wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kuahidi kuwa benki yake itawekeza zaidi ya dola za Marekani bilioni 1 nukta 5 kwenye sekta mbalimbali katika kipindi cha miaka miwili ijayo,

Dkt. Adesina ameyasema hayo alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, na kupokelewa na mwenyeji wake, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango.

“Tunajivunia uhusiano wetu wa muda mrefu na Tanzania ambayo ni mnufaika anayeongoza miongoni mwa nchi za kiafrika kupata ruzuku na mikopo yenye masharti nafuu kutoka benki yetu ambapo tangu mwaka 1971, Benki imewekeza zaidi ya dola za Marekani bilioni 3.6” alisema Dkt. Adesina

Alisema kuwa miradi inayoendelea hivi sasa nchini Tanzania kupitia ufadhili wa Benki yake imefikia thamani ya zaidi ya dola za Marekani bilioni 2 ambapo uwekezaji mkubwa uko katika sekta za nishati ya umeme, usafiri, miundombinu ya barabara, kilimo, maji na usafi wa mazingira, kusaidia Bajeti Kuu ya Serikali pamoja na uendelezaji wa rasilimali watu.

“Katika miundombinu ya barabara peke yake, Benki yangu imewekeza zaidi ya dola za Marekani bilioni 1.1 na kwamba uwekezaji huo utasaidia kuboresha usafirishaji wa bidhaa na abiria hivyo kuchochea ukuaji na uendelezaji wa uchumi wa viwanda” alisema Dkt. Adesina.

Dkt. Adesina ameutaja mradi mwingine mkubwa wa kusafirisha umeme wenye msogo wa kilovolti 400 wenye njia yenye urefu wa kilometa 670 katika Ukanda wa Kusini na Kusini Magharibi mwa Tanzania, unaohusisha pia ujenzi wa vituo vya kupozea umeme katika mikoa ya Iringa, Dodoma, Singida na Shinyanga, wenye thamani ya dola milioni 220.

“Miradi hii pamoja na ile wa umeme wa kutumia joto ardhi pamoja na maji inayotarajiwa kupatiwa fedha na Benki hiyo, itasaidia sana mkakati wa Mhe. Rais Dkt. John Magufuli, ambaye ammwagia sifa kwa utendaji kazi wake mahili, wa kujenga uchumi wa viwanda kwa kuwa na umeme wa uhakika na wenye gharama nafuu” aliongeza Dkt. Adesina.

Alisema Tanzania imepiga hatua katika viwango vya wananchi kupata huduma ya umeme ambapo awali ilikuwa asilimia 18 lakini hivi sasa kiwango hicho kimepanda hadi kufikia asilimia 38 na kwamba lengo la benki hiyo ni kutaka kiwango hicho kifikie asilimia 82 katika miaka michache ijayo.

Alisema ili kufikia hatua hiyo Benki yake ina mpango wa kuboresha Shirika la Ugavi wa Umeme nchini-TANESCO ili liongeze uzalishaji wa umeme wenye gharama nafuu, kuongeza ufanisi na kutengeneza faida ili kuchochea maendeleo ya viwanda.

Aidha, Rais huyo wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB, ameeleza kuwa benki yake inasiadia kuendeleza kilimo nchini kupitia Mpango wa Kukuza Kilimo katika Ukanda Kusini mwa Tanzania-SAGCOT, kwa kukuza masoko na uongezaji thamani ya mazao ya wakulima yanayozalishwa kupitia mradi huo.

Akizungumzia miradi ya kikanda, Dkt. Adesina alisema kuwa benki yake imewekeza katika miradi ya nishati ya umeme na miundombinu ya barabara ili kuunganisha Tanzania na nchi jirani za Burundi na Kenya ili kurahisisha biashara na kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme katika nchi hizo.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, ameeleza kuwa Benki ya Maendeleo ya Afrika ni mshirika mkubwa wa Maendeleo wa Tanzania kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa katika nyanja mbalimbali.

Alisema kuwa AfDB, licha ya kusaidia kwa kiasi kikubwa kufadhili miradi ya ujenzi wa barabara, nishati na mingine mingi na mfuko mkuu wa Serikali, mwaja jana ilitoa pia mkopo nafuu wa dola za Marekani milioni 50 kwa ajili ya kukuza mtaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini-TADB, zinazotumika kukopesha wakulima.

Dkt. Mpango amesema kuwa Rais huyo akiwa hapa nchini atatembelea mradi wa kituo cha kupooza umeme cha Zuzu kilichoko mkoani Dodoma na ataungana na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuzindua barabara ya Dodoma-Babati hadi Arusha, iliyofadhiliwa na Benki hiyo na washirika wake.

No comments: