Monday, April 9, 2018

Fursa za Usafirishaji Tanzania Zinaweza Kuendesha Nchi

Imeelezwa kuwa Tanzania ndiyo nchi inayoongoza kwa fursa kubwa za maendeleo ya kiuchumi na biashara kuliko nchi nyingine zote za Afrika Mashariki, na kutolea tuu mfano wa sekta moja ya usafiri na usafirishaji, Tanzania imeelezwa kuwa ni nchi yenye bahati sana, kuzungukwa na nchi 8 ambazo hazina bahari, hivyo fursa tuu za usafirishaji kwa kutumia bandari, reli, maziwa na anga, zikitumiwa vizuri, zinaweza kuipaisha Tanzania kiuchumi na kujiendesha, bila kutegemea sekta nyingine zozote.

Bahati hiyo imeelezwa na Mkurugenzi Mkazi wa Taasisi ya TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, Bw. John Ulanga, wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa ufadhili wa Dola za Marekani Milioni 1.3, ambazo ni karibu na Shilingi Bilini 3 za Kitanzania, kwa Taasisi ya Central Corridor Transport Facilitation Agency, inayoshughulikia mizigo inayopitia Bandari ya Dar es Salaam, kuelekea nchi za Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, kwa kutumia njia ya Ukanda wa Kati.

John Ulanga, amesema Tanzania imepakana na nchi nyingi ambazo hazina bahari kuliko nchi nyingine yoyote ya Afrika Mashariki, hivyo Tanzania ikichangamkia kutumia fursa hii kibiashara, itakuza uchumia sio tuu wa Tanzania pekee, bali hata wan chi za jirani zetu, na kule kote njia hizi zinakupita, maeneo hayo yana fursa za kustawi kiuchumi.

Ulanga amesema, Tanzania imekana na nchi nane ambazo hazina bahari, nchi hizo ni Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidekrasia ya Kongo, Zambia, Malawi na Msumbiji, na kusema kama tutazizatiti na kusafirisha mizigo yote ya nchi hizi, pato la usafirishaji pekee litakuwa kubwa kuweza kuendesha nchi, hata bila kutegemea sekta nyingine.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Central Corridor, Capt. Diodonne Dukundane, ameishukuru TradeMark kwa ufadhili huo na kueleza fedha hizo zitasaidia sana katika kutimiza majukumu ya CCTTFA ikiwemo uhamasishaji wa matumizi ya Bandari ya Dar es Salaam kwa kuelezea faida za Bandari ya Dar es Salaam ukilinganisha na bandari nyingine.

Naibu Mkurugenzi  wa Trademark East Africa, Bi. Monica Hangi amesema, kwa vile lengo la Trademark ni kusaidia kurahisisha biashara, hivyo ufadhili huo utasaidia sana kurahisisha biashara ya usafirishaji watu na mizigo kwa nchi za Uganda, Rwanda, Burundi na DRC.

Mkurugenzi wa Miundombini wa TradeMark East Africa, tawi la Tanzania, Smark Kaombwe, amesema biashara ni ushindani, hivyo ili bandari ya Dar es Salaam iweze kuvutia zaidi nchi majirani waitumie, lazima iboreshe utendaji wake mizigo ichukue muda mfupi kutoka, na pia iwe na gharama nafuu kuliko bandari majirani zetu.

Meneja Mradi wa Uangalizi wa Usafirishaji wa Central Corridor, Eng. Melchior Balentandikye, amesema kabla ya msaada huo, Central Corridor imekuwa ikijihusisha na usafiri wa barabara pekee, lakini sasa msaada huo, utawasaidia kushughulikia usafiri wa barabara, reli na usafiri wa majini na usafiri wa anga.

Meneja wa Fedha na Utawala wa Central Corridor, Costaph Natay, amesema msaada huo utasaidia sana kuboresha ufanisi, hivyo Central Corridor itaboresha ufanisi wa shughuli zake, hivyo kuongeza ufanisi katika usafirisha abiria na mizigo katika ukanda wa kati.

Meneja Mawasiliano wa Central Corridor, Flory Okadju, amesema msaada huo utaisaidia Central Corridor kuboresha mawasiliano na utoaji wa elimu kwa umma katika nchi zote tano za Ukanda wa kati, hivyo kutoa uelewa mkubwa zaidi kuhusu ubora na unafuu wa bandari ya Dar es Salaam, hivyo kuvutia zaidi wafanyabiashara wan chi hizi, kupitishia mizigo yao bandari ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkazi wa Taasisi ya TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, Bw. John Ulanga, akionyesha njia za Ukanda wa Kati, wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa ufadhili wa Dola za Marekani Milioni 1.3, ambazo ni karibu na Shilingi Bilini 3 za Kitanzania, kwa Taasisi ya Central Corridor Transport Facilitation Agency, inayoshughulikia mizigo inayopitia Bandari ya Dar es Salaam, kuelekea nchi za Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, kwa kutumia njia ya Ukanda wa Kati.
Mkurugenzi Mkazi wa Taasisi ya TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, Bw. John Ulanga, kushoto, na a Katibu Mtendaji wa Central Corridor, Capt. Diodonne Dukundane wakitia saini mkataba, wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa ufadhili wa Dola za Marekani Milioni 1.3, ambazo ni karibu na Shilingi Bilini 3 za Kitanzania, kwa Taasisi ya Central Corridor Transport Facilitation Agency, inayoshughulikia mizigo inayopitia Bandari ya Dar es Salaam, kuelekea nchi za Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, kwa kutumia njia ya Ukanda wa Kati.
Mkurugenzi Mkazi wa Taasisi ya TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, Bw. John Ulanga, kushoto, na a Katibu Mtendaji wa Central Corridor, Capt. Diodonne Dukundane wakibadilishana mkataba, wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa ufadhili wa Dola za Marekani Milioni 1.3, ambazo ni karibu na Shilingi Bilini 3 za Kitanzania, kwa Taasisi ya Central Corridor Transport Facilitation Agency, inayoshughulikia mizigo inayopitia Bandari ya Dar es Salaam, kuelekea nchi za Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, kwa kutumia njia ya Ukanda wa Kati.

No comments: