Friday, February 16, 2018

Waziri Mwakyembe Akutana Na Wajumbe Wa Bodi Ya Filamu Na kutembelea Studio Zinazoandaa Kazi Za Filamu Na Muziki

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Bw. Silvester Sengerema (kulia) moja ya kompyuta mpakato kuashiria makabidhiano ya vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa kwa ajili ya kuimarisha majukumu ya Bodi ya Filamu alipofanya ziara katika ofisi za Bodi na kukutana na wajumbe wa Bodi ya Filamu jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kulia) akimsikiliza Mkurugenzi wa Jasons Televisheni (JTV) Bw. Sanstus Mtsimbe (kulia) alipotembelea studio za televisheni hiyo kuangalia namna kazi za filamu zinavyoandaliwa jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo na wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Bw. Silvester Sengerema
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kushoto) akiangalia moja studio za Starline Films zilizopo Mikocheni alipotembelea studio hiyo kuangalia namna kazi za filamu zinavyoandaliwa jana Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Bw. Silvester Sengerema na kushoto ni meneja wa studio za Starline Films Bw. Silver Oddo
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo (kulia) akifafanua jambo alipokua akizungumza na wafanyakazi wa Studio za Starline Films (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) kutembelea Studio zinazojishughulisha na uandaaji wa kazi za filamu na muziki jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Bw. Silvester Sengerema
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (waliokaa kulia) akimsikiliza Mkurugenzi wa Studio za Wanene Bw. Darsh Pandit (wapili kushoto) baada ya kuangalia baadhi ya kazi zilizoandaliwa na studio hizo wakati wa ziara yake kutembelea studio mbalimbali zinazojishughulisha na uandaaji wa kazi za filamu na muziki jana Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) kiandika maoni yake katika kitabu cha wageni baada ya kutemblea studio za Wanene zilizopo Mwenge wakati wa ziara yake kutembelea studio mbalimbali zinazojishughulisha na uandaaji wa kazi za filamu na muziki jana Jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo na kushoto ni Mkurugenzi wa Studio za Wanene Bw. Darsh Pandit
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo (kulia) akitoa taarifa fupi ya majukumu ya bodi ya filamu kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) alipofanya ziara katika ofisi za Bodi na kukutana na wajumbe wa Bodi ya Filamu jana Jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Bw. Silvester Sengerema (kulia) akizungumza wakati wa kikao cha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kulia) alipofanya ziara katika ofisi za Bodi na kukutana na wajumbe wa Bodi ya Filamu jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo na wapili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Sanaa Bibi. Leah Kihimbi
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Filamu (hawapo pichani) alipofanya ziara katika ofisi za Bodi na kukutana na wajumbe hao jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo
Baadhi ya watumishi wa Bodi ya Filamu na wajumbe wa kamati ya maudhui ya filamu wakifuatilia maagizo ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) alipofanya ziara katika ofisi za Bodi na kukutana na wajumbe wa Bodi ya Filamu jana Jijini Dar es Salaam.Picha na: Genofeva Matemu – WHUSM

No comments: