Sunday, February 11, 2018

RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AFUNGUA MKUTANO MKUU WA CHAMA CHA WALIMU ZANZIBAR LEO

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Katibu Mkuu wa ZATU Mussa Omar Tafurwa, alipowasili katika viwanja vya Wizara habari kuhudhuria ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Walimu wakati wa hafla ya Mkutano Mkuu wa Sita wa Chama cha Walimu Zanzibar uliofanyika katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Zanzibar wakati wa ufunguzi huo
BAADHI ya Walimu wa Chama cha Walimu Zanzibar wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akifungua mkutano wa Sita uliofanyika katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi kikwajuni Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa viongozi wa meza kuu wakiimba wimbo wa wafanyakazi wa solidariti foreva wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Sita wa Chama cha Walimu Zanzibar uliofanyika katika ukumbi wa zamani wa baraza la wawakilishi kikwajuni Zanzibar
WANAFUNZI wa Skuli ya Msingi Kisiwandui wakicheza ngoma ya mwanandege wakati wa ufunguzi huo wa mkutano mkuu wa chama cha walimu Zanzibar.
RAIS w Chama cha Walimu Zanzibar Seif Mohammed akisoma risala ya Chama hicho wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Sita wa Chama hicho wakati wa ufunguzi huo uliofanyika katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar
BAADHI ya Wanachama wa Chama cha Walimu Zanzibar wakifuatilia hutuba ya ufunguzi ya ufungunguzi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, wakati wa ufunguzi wa mkutano huo leo uliofanyika katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Zanzibar.
KAIMU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali pia ni Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Zanzibar kabla ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, kuufungua mkutano huo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akionesha picha ya sura yake aliokabidhiwa zawadi na Chama cha Walimu Zanzibar wakati wa hafla ya Mkutano Mkuu wa Sita wa Chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi kikwajuni Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Chama cha Walimu Zanzibar baada ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Sita wa Chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa zamani wa baraza la wawakilishi kikwajuni.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Rais wa Chama cha Walimu Tanzania Bara. Leiya Ulaya, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwnyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Walimu Uganda Tumuhimbise Zadock, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Zanzibar uliofanyika katika ukumbi wa zamani wa baraza la wawakilishi kikwajuni
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mwakilishi wa Chama cha Walimu kutoka (DLF) Flemming Sorrensen, baada ya hafla ya uzinduzi wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Walimu Zanzibar.Picha na Ikulu

No comments: