Monday, February 12, 2018

MAMA SALMA, BASHE, MSUKUMA, LUSINDE WAMUOMBEA KURA MTULIA KINONDONI

Na Said Mwishehe, Glogu ya jamii

WABUNGE kutoka majimbo mbalimbali nchini kupitia Chama ChaMapinduzi (CCM), wamewaomba wananchi wa jimbo la Kinondoni jijiniDar es Salaam kuhakikisha Februari 17, mwaka huu wanamchaguamgombea ubunge wa chama hicho, Abdallah Mtulia katika uchaguzi
mdogo jimboni humo.

Wamesema Mtulia ndio chaguo sahihi kwa wananchi wa Kinondoni nakwamba akiwa mbunge watashirikiana naye katika kufanikishachangamoto za wananchi zinapata ufumbuzi wake.Pia wameeleza namna ambavyo wabunge wa CCM  wamekuwa wamojabungeni katika kupigania maendeleo ya wananchi tofauti na wabungewa upinzani ambao kila kitu wao ni kupinga hata liwe jambo lamaendeleo.

Wakizungumza kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika wanja wa People Kigogo wilayani Kinondoni jijini, wabunge hao waCCM wamewaomba wananchi kutofanya makosa kwenye uchaguzi huohuku wakitoa sababu mbalimbali za kwanini Mtulia anastahili kuwa mbunge wa jimbo hilo.

Mgeni rasmi  kwenye kampeni hizo ambaye pia ni Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM) amewaomba wananchikumchagua Mtulia kwani ndio mgombea sahihi na wanaamini akiwambunge watashirikiana naye kutatua kero za wananchi.
 
"Nimekuja kuzungumza na ninyi kuwaomba tarehe 17,siku yaJumamosi wote mkamchague Mtulia, lakini si tu kumchagua lazimatuseme kwanini mumchague Mtulia.Ndio mgombea mwenye sifa zoteza kuwa mbunge wa Kinondoni,"amesema Bashe.

Pia amesema kwenye kampeni hizo wapo wanaotoa hoja kuwa Serikali ya CCM haitaki mfumo wa vyama vingi, ambapo amefafanua hoja hiyo haina maana yoyote kwani mwaka 1992 licha ya watanzania wengi kutaka mfumo wa chama kimoja uendelee lakini uamuzi ulitolewa wa kuingia mfumo vyama vingi.

"Mwaka 1992, watanzania walipata fursa ya kuchagua tuingie kwenye mfumo wa vyama vingi au laa.Waliotaka vyama vingi walikuwa asilimia 20 na waliosema chama kimoja kiendelee walikuwa asilimia 80."Mwaka 1995 tukafanya uchaguzi wa vyama vingi na CCM ikashinda, hivyo CCM hatuna hofu na mfumo wa vyama vingi na ndio maana tumeendelea kushinda katika kila chaguzi.

"Pia wapo wanaotoa hoja CCM hakuna demokrasia hili nalo halina ukweli.CCM demokrasia ipo tena ya kutosha.Ndani ya CCM tunaweza kutofautiana kimtazamo, tunaweza kutofautiana kwa hoja na wakati mwingine tukashikana mashati lakini ukweli utabaki tunafanya hayo yote kwasababu ya demokrasia tuliyonayo,"amesema Bashe.

Kuhusu hoja uchaguzi ni gharama, Bashe amesema wanaona ni gharama wanayo fursa ya kupeleka muswada wa sheria bungeni ili kubadilisha sheria ambayo itaelekeza hakuna uchaguzi mdogo hata mbunge anapoamua kuondoka chama kimoja na kujiunga na chama kingine.Pia njia nyingine ni kubadilishwa kwa sheria ili kurudi kwenye mfumowa chama kimoja ambao hautakuwa na gharama.
 
"Kuna hoja nyingine hazina maana mbunge akitoka upinzani kwendaCCM wanasema kanunuliwa ila akitoka CCM kwenda upinzani huyohajanunuliwa.Hii hoja haina mantiki yoyote.

Bashe amesema Mtulia ameamua kujiunga CCM ili aweze kuleta maendeleo ya wananchi kwani alikokuwa hakuko salama."Mtulia mwaka 2015 alikuwa kwenye gari ya Ukawa na sasaameamua kuwa kwenye gari la CCM.Tatizo liko wapi hasa kwakuzingatia kule alikokuwa hakuko salama.CUF imegawanyika vipande viwili kwani Katibu Mkuu wao, Maalim Seif Sharif Hamad anafanya 

kazi kivyake na Mwenyekiti Lipumba naye yupo kivyake."Mtulia alikuwa anapata posho bungeni, analipwa mshahara lakini ameamua kujiuzulu kutokana na hali iliyopo kwenye chama chake kwani hakuwa anapata muda wa kutosha kushughulikia changamoto za jimbo lake.Akaona ni bora ajiuzulu kule na kisha aje huku,"amesema Bashe.

Mke wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Lindi, Salma Kikwete amewaomba wananchi wa Kinondoni kumchagua Mtulia ili washirikiane naye kutatua changamoto za wananchi wa Tanzania wakiwamo wa Kinondoni.Amesema Rais ,Dk. John Magufuli anafanya kazi nzuri ya kuleta maendeleo ya wananchi ,hivyo ni vema Kinondoni wakamchagua 

Mtulia ili awe sehemu ya kiunganishi kati ya Rais na wananchi."Kazi iliyopo mbele yenu ni kumchagua Mtulia ili awe mbunge wa Kinondoni. Wabunge na viongozi wa ngazi mbalimbali ndio maana wapo hapa kumuombea kura Mtulia awe mbunge kwani wanaamini atashirikiana nanyi katika kupigania mamboyanayowahusu,"amesisitiza Mama Salma. 

Kwa upande wake Mbunge Geita Vijijini, Joseph Kasheku mbali ya kumuombea kura Mtulia ametumia nafasi hiyo kuwaeleza baadhi ya viongozi wa Chadema kuwa hawana tofauti na watu matapeli.Amemtolea mfano Frederick Sumaye ambaye amekuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 lakini hakuna hata siku moja ambayo amekwenda kuhutubia wananchi wa Kigogo lakini baada ya kuona kuna uchaguzi wa ubunge ndio anakwenda.

"Sumaye amekuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 lakini hajawahi kufika kuhutubia wananchi na leo maisha yamempiga ndio anakuja kwenu.Wananchi msihangaike ikifika siku ya uchaguzi Februari 17 
nendeni mkamchague Mtulia aje bungeni."Tena akifika bungeni nitamwambia akamuombe Spika wa Bungetuwe tunakaa karibu ili niwe namuelekeza ... mimi ni darasa la saba lakini mambo yasiyokuwa na tija kwa wananchi hayana nafasi,"amesema.

Pia amesema upinzani wanazungunzia namna ambavyo viongozi wa CCM wanapiga magoti wakati wa kumuombea kura Mtulia na kueleza hiyo ni ishara ya heshima na ndio sifa ya wanaCCM ya kuheshimu wananchi.Wakati huo huo, Mbunge wa Mtela, Livingston Lusinde naye ameendelea kumuombea kura Mtulia huku akitumia nafasi hiyokuwapiga  vijembe wapinzani kutokana na hoja mbalimbali wanazozitoa kwenye kampeni hizo.

CCM kwenye kampeni hizo wamekuwa wakitumia wabunge wake mbalimbali pamoja na viongozi ambao wamekuwa wakimuombea kura  Mtulia na kwa kampeni za leo zilizofanyika Kigogo wabunge zaidi ya10 wamemuombea kura mgombea wao.

No comments: