Binti mwenye umri chini yaa miaka 18 akiwa amembeba motto wake mdogo baada ya kukatishwa ndoto zake za kupata masomo na kijana.
baadhi ya wananchi waliohudhuria kwenye uzinduzi wa semina ya mapambano dhidi ya ndoa za utotoni uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki,mjini Singida.
baadhi ya wananchi waliohudhuria kwenye uzinduzi wa semina ya mapambano dhidi ya ndoa za utotoni uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki,mjini Singida.
Meneja wa World Vision Tanzania (WVT) Kanda ya kati,Faraja Kulangwa akiwasilisha mada juu ya madhumuni ya semina hiyo kwa wananchi waliohudhuria kwenye ukumbi wa mikutano wa Kanisa Katoliki,mjini Singida.
Mkuu wa wilaya ya Singida,Eliasi Tarimo alipokuwa akizindua mpango wa mapambano dhidi ya ndoa za utotoni kwenye ukumbi wa Kanis Katoliki,mjini Singida.(Picha zote Na Jumbe Ismailly).
Na,Jumbe Ismailly SINGIDA
TATIZO la ndoa za utotoni katika Tanzania na nchi za Afrika Mashariki limeonekana ni tatizo kubwa sana katika maeneo hayo ambapo kitakwimu inaonyesha kuwa kati ya mikoa kumi bora Mkoa wa Shinyanga unaongoza kwa kuwa na asilimia 59 na Mkoa wa Singida umeshika nafasi ya nane kwa kuwa na asilimia 42.
Meneja wa Shirika la kidini lisilokuwa la kiserikali la World Vision Tanzania (WVT) Kanda ya kati,Faraja kulanga aliyasema hayo kwenye uzinduzi wa mpango wa kutokomeza mimba za utotoni uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kanisa Katoliki,mjini Singida.
Alifafanua kwamba kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Tanzania Demokratic Health Survey ya mwaka 2010 inaonyesha kitakwimu kwamba tatizo la ndoa za utotoni,Mkoa unaoongoza ni Mkoa wa Shinyanga wenye asilimia 59 huku Mkoa wa Singida ukiwa na assilimia 42 na hivyo kushika nafasi ya nane katika mikoa hiyo kumi bora.
“Kwa maana kwamba ule utafiti huwa unakwenda kuuliza kila nyumba na wakiuliza katika kila nyumba mama alipata ujauzito katika umri gani,wale waliopata mimba katika umri chini ya miaka 18 ilikuwa ni asilimia 59.”alifafanua Kulanga.
Kwa mujibu wa Meneja huyo katika asilimia 42 ya familia zilizoulizwa kina mama kwamba alipata ujauzito akiwa na umri chini ya miaka 18,asilimia 42 wakaonekana ilikuwepo na kwamba shirika hilo lilifanya utafiti katika Kanda saba kwenye maeneo wanayofanya kazi.
Aidha Meneja huyo aliweka bayana kwamba kanda hiyo ina jumla ya kanda saba ambazo ni pamoja na Kanda ya Pwani ambayo ndiyo inayoongoza ikifuatiwa na kanda ya kati ambayo ni pamoja na Mkoa wa Singida ambapo kitakwimu inaonyesha kuwa kuna tatizo kubwa la ndoa za utotoni.
Kwa upande wake Afisa wa dawati la jinsia na Watoto kutoka jeshi la polisi wilaya ya Singida,Amina Fakih Abdallah alibainisha kuwa kinachochangia kwa namna moja au nyingine kuwepo kwa ongezeko la mimba za utotoni ni ukinzani wa sheria zinazosimamia mimba za utotoni.
Hata hivyo afisa huyo wa dawati la jinsia na watoto alisisitiza pia kwamba katika sheria zinazosimamia ndoa hizo za utotoni,hakuna sheria iliyosimama na inayolinda mimba za utotoni kutokana na moja ya sheria hizo kuruhusu mtoto aolewe akiwa na umri wa miaka 14 huku sheria ya jinai inakataza motto mwenye umri wa miaka 18 kuolewa.
“Sasa kama inalinda mimba za utotoni kuna sheria inaruhusu mtoto wa kike aolewe akiwa na umri wa miaka 14,sasa hii sheria inaporuhusu mtoto aolewe akiwa na umri wa miaka 14,we huku kwenye sheria ya jinai unasema kwamba huyu mtoto aliye chini ya miaka 18 haruhusiwi kuolewa”alifafanua.
Naye Mkuu wa wilaya ya Singida,Eliasi Tarimo akizindua Mpango wa mapambano dhidi ya kutokomeza ndoa za utotoni za mradi wa Mtinko ADP uliopo wilaya ya Singida alisisitiza pia juu ya kuondoa mapungufu yaliyopo katika sheria zinazosimamia mimba za utotoni ili ziweze kufanana badala ya kuendelea kukinzani.
Kwa mujibu wa Tarimo ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama katika wilaya hiyo sheria zote hizo hazina budi kutamka bayana kwamba umri wa motto usizidi miaka 18,ikiwemo sheria ya ndoa,sheria ya motto mwenyewe na kipengere kinachotamka kuwa motto anaweza kuolewa kwa kibali cha wazazi.
1 comment:
Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.
Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.
Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.
Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.
Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.
Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com
Post a Comment