
Mkuu wa Wilaya ya Chato Shabani Ntarambe (aliyesimama) akimweleza jambo Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia) wakati wa mkutano wa hadhara kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, ambapo Waziri ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.Kulia ni Diwani wa kata ya Kasenda Muganza Mwita.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia katikati) akiwa kwenye moja ya boti inayotumika kwa Uvuvi wa samaki kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chato Bathromeo Christiani, Kushoto ni Diwani wa kata ya Kasenda Muganza Mwita. (Picha na John Mapepele)

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia) akiwahutubia wananchi kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. (Picha na John Mapepele)

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye kofia) akikagua ofisi za soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi bi Mwanaidi Mlolwa. Nyumba niYohana Mikumbe Mtekinolojia wa samaki katika soko la Kasenda. . (Picha na John Mapepele)

Umati wa wananchi waliohudhuria mkutano wa Waziri Luhaga Mpina kwenye soko la kimataifa la samaki la Kasenda wilayani Chato leo, ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. (Picha na John Mapepele)
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameamuru kufanyika ukaguzi mpya wa hesabu za fedha kwenye masoko yote ya kimataifa ya samaki na mazao yake yaliyoko katika Ziwa Victoria ili kuhakiki uhalali wa mapato ya Serikali yaliyokusanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Masoko hayo yatakayohusika na ukaguzi huo ni pamoja na Kirumba Mwanza, Nyakalilo Buchosa Mwanza ,Kasenda Chato Geita, Magalini Muleba Kagera, Kemondo Bukoba Kagera na Mwigobero Musoma Mara ambapo wafanyabiashara watakaobainika walihusika kufanya udanganyifu wa mapato watatakiwa kurejesha fedha hizo walizoiibia Serikali kwa kipindi hicho ambapo Watumishi wa Umma nao waliohusika kuhujumu mapato hayo watasakwa popote walipo na kufikishwa kwenye vyombo vya dola kukabiliana na mashtaka ya kuhujumu wa rasimali za nchi .
Hatua hiyo ya Waziri Mpina imekuja kufuatia kubaini kuwepo udanganyifu mkubwa katika biashara ya samaki, dagaa,mabondo, na mapanki akibainisha kuwepo tabia ya kupunguza uzito na idadi ya magunia,kubadilisha matumizi ya vibali,kuchanganya mizigo ya ndani na nje ya nchi kwenye malori, kuanzishwa kwa masoko ya kimataifa yasiyo rasmi na wafanyabiashara wakubwa wa mazao ya uvuvi kutolipa kodi za mapato kutoka TRA.
Pia Waziri Mpina ameamuru kufutwa kwa masoko yote yasiyo rasmi yaliyopewa hadhi ya kimataifa ikiwemo soko la Nyakalilo na Magalini ambapo amemuagiza Katibu Mkuu Uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Yohana Budeba kuwaondoa na kuwapangia vituo vingine vya kazi watumishi waliokuwepo kwenye masoko hayo.
Waziri Mpina ametolea mfano udanganyifu mkubwa uliofanywa na wafanyabiashara na watumishi wa umma wasio waaminifu likiwemo tukio la Disemba 16 mwaka jana ambapo mfanyabiashara mmoja (jina tunalo)huku akitumia gari lenye usajili ya nchi ya Rwanda lenye namba za usajili RB 9591 alipewa kibali cha kusafirisha magunia 258 kwenda Ngara mkoani Kagera na badala yake aliyapeleka nchini Rwanda na kuisababishia Serikali hasara ya sh. Milioni 3.
Pia kupunguza uzito na idadi ya magunia ili kulipia kidogo mapato ya Serikali akitolea mfano mfanyabiashara mwingine (jina tunalo) ambapo Disemba 2 , 2017 kutoka soko la Kasenda alisafirisha magunia 300 ya dagaa lakini yaliyolipiwa mrabaha wa Serikali ni magunia 200 tu huku Serikali ikipoteza mapato ya magunia 100 .
Waziri Mpina amesema matukio hayo ya udanganyifu aliyotolea mfano ni ya siku moja tu huku wafanyabiashara hao wakiwa na utamaduni wa kusafirisha zaidi ya safari nane kwa mwezi ambapo Serikali hupoteza mabilioni ya fedha za mapato kwa mwaka ambapo Samaki, dagaa, kayabo, mabondo, mapanki,furu wamekuwa wakiroroshwa kupitia mipakani na njia ya panya kwenda nchi za Rwanda, Burundi, DRC, Zambia, Malawi, Uganda na Kenya.
Amesema wafanyabiashara waliopewa leseni za kusafirisha mazao ya uvuvi nje ya nchi wamekuwa mawakala wa raia wa kigeni ambapo kazi ya kununua, kukusanya na kusafirisha hufanywa na wageni jambo ambalo ni kinyume cha Sheria ya Uvuvi namba 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009 kifungu cha 13 (14).
Kuhusu kasi ya Uvuvi haramu katika Wilaya ya Chato Waziri Mpina amesema taarifa zinaonesha kwa kipindi cha Januari hadi Disemba mwaka 2017 zana haramu zikiwemo Timba, Kokoro,Katuri,Mitumbwi, yenye thamani ya sh milioni 525,207,000 vilikamatwa, kutaifishwa na kuteketezwa.
Ametumia nafasi hiyo kuwasihi wananchi kuacha uvuvi haramu huku akieleza kusikitishwa na namna watanzania hao wazawa walivyopoteza mitaji yao lakini akatangaza msimamo mzito.
“Nimesononeshwa sana na taarifa ya kuteketezwa kwa mitaji ya wafanyabiashara hao wazawa kwa sababu ya kujihusisha na uvuvi haramu lakini nataka kuwakikishia kuwa vita dhidi ya uvuvi haramu haina suluhu na kwamba sitamuonea haya wala huruma mtu yoyote atakayejihusisha na uvuvi haramu tutawashughulikia wote bila huruma kwani Serikali ya awamu ya tano imejidhatiti kukabiliana na uvuvi haramu kwa nguvu zote na bila kuchoka”alisema.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mwanaidi Mlolwa alisema jukumu la kulinda rasilimali za nchi liko kikatiba hivyo kila mwananchi ana wajibu wa kusaidia kulinda rasilimali hizo zisitoroshwe kwa manufaa ya nchi ya nyingine.
Amesema Sheria ya Uvuvi namba 22 ya mwaka 2003 kifungu cha 37(a) (ii) na (iii) na kanuni zake za mwaka 2009 zinawapa mamlaka wasimamizi wa Sheria hiyo kumkamata mtu yeyote anayekutwa na samaki na mazao yake waliovuliwa kwa njia haramu na kutaifisha mali zote ikiwemo samaki, boti, mitumbwi na magari yaliyobeba samaki hao.
Mkuu wa Wilaya ya Chato, Shabani Ntarambe amesema katika kukabiliana na uvuvi haramu wilaya kwa kipindi cha Januari hadi Disemba mwaka 2017 imefanikiwa kukamata ,kutaifisha na kuteketeza zana haramu za uvuvi zikiwemo Timba, Kokoro,Katuri,Mitumbwi, yenye thamani ya sh. milioni 525.2 na kumhakikishia Waziri Mpina kuwa mapambano bado yanaendelea kukomesha kabisa uvuvi haramu
2 comments:
Ushuhuda
Nilivunjika moyo kabisa uhusiano wangu ulipoisha. Niliamini kweli kwamba nilikuwa nimepoteza mpenzi wa maisha yangu milele. Kisha nikampata Dkt. Dawn, na kila kitu kikabadilika.
Kwa wema, hekima, na mwongozo wenye nguvu, alirudisha upendo niliodhani ulikuwa umetoweka. Leo, tuna furaha zaidi kuliko hapo awali!
Dkt. Dawn aligeuza machozi yangu kuwa furaha kweli.
Dkt. Dawn Anaweza Kukusaidia Kwa:
✅ Uchawi wa Mapenzi
✅ Uchawi wa Mimba
✅ Kurejesha Ndoa / Uhusiano
✅ Tiba za Mimea kwa VVU, Ugonjwa wa Figo, Matatizo ya Moyo, Maambukizi, na zaidi
📧 Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com
📞 Simu/WhatsApp: +2349046229159
Usiteseke kimya kimya. Dkt. Dawn anaweza kurudisha furaha maishani mwako!
🌹 Ushuhuda Wangu Kuhusu Dkt. Dawn – Mtu Aliyerejesha Nyumba Yangu na Furaha Yangu
Nataka kushiriki ushuhuda wangu wa dhati kuhusu jinsi Dkt. Dawn alivyobadilisha maisha yangu kabisa.
Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na alikuwa ameenda kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.
Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwangu — na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.
Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.
Lakini si hayo tu — Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyokuwa ikizunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.
Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote — huzuni, bahati mbaya, au mkanganyiko — usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.
Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com
Post a Comment