Sunday, December 31, 2017

NAIBU WAZIRI ULEGA AAGIZA WATENDAJI WA VIJIJI NA WENYEVITI KUWASOMEA MAPATO NA MATUMIZI WANANCHI

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizingumza na wananchi wa kijiji cha Kiziko alipofanya ziara katika jimbo la Mkuranga.
Mwenyekiti wa Halmshauri ya Mkuranga, Juma Abeid akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kiziko juu ya mikakati ya Halmashauri katika uboreshaji wa sekta mbalimbali.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akiwasili katika kijiji cha cha Kitonga katika ziara ya vijiji jimbo la Mkuranga. 


Na Chalila Kibuda,Globu ya jamii.

NAIBU waziri wa Mifugo na Uvuvi (Mbunge) wa Jimbo la Mkuranga mkoani Pwani Abdalla Ulega ametoa agizo kwa Watendaji wa vijiji na Wenyeviti kuwasomea mapato na matumizi wananchi wao ili kuepuka kurudisha nyumba uchangiaji wa shughili za maendeleo.

Naibu waziri huyo ametoa agizo hilo wilayani humo akiwa katika mwendelezo wa ziara za vijijini ambapo akiwa katika kijiji cha Kiziko, kilichopo Kata ya Mwarusembe baada ya kupokea malalamiko ya wananchi juu ya viongozi wao ngazi ya kijiji kushindwa kusoma taarifa ya mapato na matumizi.

Alisema kushindwa kusoma taarifa za mapato na matumizi kunachangia kwa asilimia kubwa wananchi kushindwa kuchangia maendeleo katika maeneo hayo hivyo lazima wananchi wajulishe kinachoingia na kinavyotumika.

"Natoa agizo hili kwa watendaji na wenyeviti kusoma mapato na mapato na matumizi na hapa naagizi mtendaji wa Kata ya Mwarusembe kuhakikisha hadi kufika Januari 2 ,2018 niwe nimepata taarifa za kushindwa kusoma mapato na matumizi katika kijiji hiki cha kiziko. "alisema Ulega

Alisema wananchi wanatamani kujitolea kwa lengo la kuchangia maendeleo lakni wanavunjwa moyo viongozi hao huku akisisitiza kupewa ifika January 2 awe amepata taarifa nakuhaidi kulifuatilia jambo hilo kwa ukaribu zaidi.

Pia akiwa katika kijiji hicho cha alitoa mifuko 50 ya saruji pamoja na shilingi laki tano kwa ajili kuchangia ujenzi ya serikali ya kijiji hicho ikiwa pamoja na matundu ya vyoo katika shule ya msingi kiziko huku akitoa ahadi ya shilingi tisa. Kwa ajili ya kuchangia vikundi tisa vya Vikoba.

Awali wakitoa kero zao kwa Mbunge huyo walisama wamakerwa sana na kukithiri kwa mifugo aina ya ng'ombe hali inayosababisha umasikini na njaa kwa wananchi hao kutokana na mazao yao.Pia walilalamikia kukosekana kwa barabara, inayounganisha kijiji hicho cha kiziko na vijiji vingine pamoja na Daraja linalounganisha vitongoji vya Gwanzo, Chakande vyenye wakazi wengi zaidi.

"kwakweli tuna kero nyingi mno hapa kijijini kwetu kwani mbali na barabara na Daraja lakini pia tunakero ya kukosa Daktari kwenye Zahanati hii yetu hali inayosababisha wananchi kukosa kupatiwa huduma stahiki. "alisisitiza Mojamed Ally mjumbe wa serikali ya kijiji.

Naye Ofisa Kilimo wa Kijiji hicho... Alisema wananchi hao ambao waliowengi ni wakulima lakini wanakosa dhana za kisasa za kilimo pamoja na ukosefu wa gereta ili kusikuma maji kwenye kisima cha maji kilichopo shule ya msingi kiziko ili wanafunzi na raia wengine wapate maji.

Mbali na kijiji hicho pia Naibu waziri Ulega aliendelea na ziara katika kijiji cha Kitonga kata hiyo ya Mwarusembe ambapo pia alipokea kero ya kuvamiwa na ng'ombe kwenye mashamba ya wananchi huku wakimtaka kumaliza kero hiyo.

Wakati huohuo wananchi hao walilalamika kwa Kiongozi wao huyo juu ya kutoridhishwa na huduma zinazotolewa katika Hospitali ya wilaya hiyo nakudai kwamba wakinana mama wanapohitaji kujifungua kuambiwa wabebe vifaa vya uzazi mbali Serikali kusema huduma hiyo bure.

"Naibu waziri kwakweli wananchi wako sisi tunaumia. Pale Hospitali ya Wilaya ya mkuranga ni tatizo bado panafigisu na kona kona nyingi tunaomba tusaidie. "alisema mmoja wa wananchi katika mkutano huo.

No comments: