Sunday, December 31, 2017

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA AMEHUTUBIA BARAZA LA KUFUNGA MWAKA 2017 NA KUUKARIBISHA MWAKA MPYA 2018 JIJINI MBEYA

Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiongoza Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018. Baraza hilo limehudhuriwa na Maafisa na Askari kutoka vituo mbalimbali vya Magereza Mkoani Mbeya, Chuo cha Magereza Kiwira na Chuo cha Ufundi Mbeya ambapo Baraza hilo limefanyika leo Desemba 31, 2017 katika Viwanja vya Magereza Mkoani Mbeya.
Baadhi ya Askari wa kike wa Jeshi la Magereza kutoka vituo mbalimbali vya Magereza ya Mkoa wa Mbeya wakisikiliza hotuba ya Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(hayupo pichani) katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018.
Wakuu wa Magereza yaliyopo Mkoani Mbeya wakifuatilia kwa umakini mkubwa maelekezo ya Kamishna Jenerali wa Magereza aliyoyatoa katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018.
Mkuu wa Magereza Mkoani Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Kijida Mwakingi akitoa taarifa fupi ya Mkoa wake katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018.
Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila akitoa ufafanuzi wa masuala yahusuyo Divisheni ya Huduma za Urekebishaji mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa pili kulia) katika Baraza la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018 (wa kwanza kushoto) ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mbaraka Semwanza. Baraza hilo limefanyika katika Viwanja vya Magereza Mkoani Mbeya.
Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu katika Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Chacha Binna akitolea ufafanuzi kuhusiana na masuala ya madeni ya watumishi yaliyoulizwa na Maafisa na Askari wa Jeshi hilo Mkoani Mbeya(hawapo pichani) katika Baraza hilo.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akipokea salaam ya heshima kutoka kwa gwaride maalum alipowasili katika Viwanja vya Magereza Mkoani Mbeya kabla ya kuhutubia Baraza la Maalum la Maafisa na Askari kutoka vituo mbalimbali vya Magereza Mkoani Mbeya, Chuo cha Magereza Kiwira na Chuo cha Ufundi Mbeya ambapo Baraza hilo limefanyika Desemba 31, 2017.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akikagua gwaride la Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza kabla ya kuhutubia Baraza Maalum la Maafisa na Askari wa Jeshi hilo lililofanyika katika Viwanja vya Magereza Mkoani Mbeya leo Desemba 31, 2017(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments: