Tuesday, October 3, 2017

DC WA KIBAHA AWAASA WANAWAKE KUTODHARAU KAZI

Na.Vero Ignatus ,Mlandizi

Mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumtha mshana amewaasa wanawake kutokudharau kazi hata kama ni ndogo kwani kwenye hiyo ndogo ndipo nyingine kubwa itafuata.

Ameyasema hayo Katika Kanisa la RGC lililopo Mlandizi ambapo alikuwa mgeni rasmi katika Kongamano la wanawake lililoambatana na Changizo kwa ajili ya kununua eneo la kiwanja cha kujenga kanisa

Mkuu huyo wa wilaya ambaye pia ni mchungaji alipata nafasi ya kuhubiri katika kongamano hilo, ambapo amewataka wanawake kujiamini na kuaajibika kwani hata neno la Mungu linasema asiyefanya kazi na asili.

"Nyumba ambayo mwanamke ni legelege nyumba hiyo haitaendelea kamwe,wanawake changamkeni wajibikeni nyie ndiyo nguzo ya familia hutamchosha mume wako" alisema

Kwa upande wake Mchungaji Kiongozi Kambi ya Waebrania Mlandizi Mercy Adam Mwakimomyile amesema kuwa Kongamano hilo limebeba kaulibiu isemayo Nguvu ndani ya Mwanamke(Power in Woman)ambapo imewafanya wanawake wajisikie wanaweza

"Kutokana na uwezo uliopo ndani ya mwanamke basi leo tumeamua kuwa tunaweza kumjengea Mungu madhabahu kupitia kongamano hili" alisema

Amesema katika kanisa hilo wato watoto zaidi ya elfu moja ambao wanafundishwa maadili kupitia neno la Mungu kuibua vipawa  mbalimbali vilivyopo ndani yao na kuviibua
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumta Mshama .Picha na Vero Ignatus Blog.
Mkuu wa wilaya akiweka saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika kanisa la GRC kambi ya Waebrania Mlandizi àliyepo kulia kwake ni mchungaji kiongozi wa kanisa hilo la Mlandizi.Picha na Vero Ignatus Blog.
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe.Assumtha Mshama akiwa anaonyeshwa mipaka ya eneo la kiwanja cha Kanisa la GRC Kambi ya Warbrania Mlandizi aliyepo nae ni Mchungaji kiongozi wa Kanisa hilo  Mercy Adam Mwakimomyile.Picha na Vero Igbatus Blog.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha Mhe.Assumta Mshama akiwa anaongoza maombi mara baada kuona eneo ambalo linatarajiwa kujengwa kanisa .Picha na Vero Ignatus Blog.Kuna Mama Mtume Deo Rwetaka 

Mhe.Assumtha Mshama akihubiri neno la Mungu katika kanisa hilo la GRC lililopo Mlandizi.Picha na Vero Ignatus Blog
 Wa kwanza kulia ni Mchungaji Kiongozi wa RGC Kambi ya Waebrania Mercy Adam Mwakimomyile Mama Mtume Deo Rwetaka wa Kwanza kushoto,Mama Askofu Amon Lukama wa RGC Tanzania na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe.Assumtha mshana
Baadhi ya waumini walioshiriki katika ibada hiyo ya Kongamano la Wanawake RGC Mlandizi.Picha na Vero Ignatus Blog.
Baadhi ya watoto wanaolelewa kanisani hapo wakiimba wimbo maalumu wa kuliombea Taifa la Tanzania pamoja na Rais wa nchi.Picha na Vero Ignatus Blog.
Ibada ya ikiendelra katika kanisa hilo la GRC Kibaha Mlandizi .Picha na Vero Ignatus Blog.








No comments: