Wednesday, July 5, 2017

RAIS DKT. MAGUFULI ALIPOZUNGUMZA NA WANANCHI WA MKOA WA GEITA WAKATI AKIELEKEA CHATO JANA JIONI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpungia mkono Mama mmoja mlemavu mkazi wa Buseresere mara baada ya kumaliza kuhutubia mamia ya wakazi wa Katoro na Buseresere waliojitokeza pembezoni mwa barabara katika eneo hilo kumsalimia wakati akielekea Chato Mkoani Geita jana jioni.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Bwanga njia panda ya kuelekea Makao makuu ya Wilaya ya Chato jana jioni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Katoro na Buseresere mara baada ya kusimama wakati akielekea Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Geita mjini wakati akielekea Chato.
Wananchi wa Geita waliokuwa na Shauku ya kumuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakiwa wamepanda juu ya magari pembezoni mwa barabara ya Usagara- Sengerema-Geita jana jioni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Mama Rosemary Lucas ambaye alikuwa akiwasilisha kero yake ya kuvunjiwa nyumba Sengerema mkoani Mwanza.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela akichukua maelezo ya mama huyo Rosemary Lucas aliyevunjiwa nyumba yake Sengerema mkoani Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kada wa zamani wa CHADEMA Hamis Tabasamu ambaye alikuwa akionesha Kadi yake mpya ya CCM mara baada ya kuhamia. Kadi hiyo alikabidhiwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza katika Wilaya ya Sengerema. PICHA NA IKULU.

No comments: