Monday, July 3, 2017

NIDA YAIBUKA MSHINDI WA KWANZA KATIKA KUNDI LA BANDA BORA KWA WIZARA NA TAASISI ZA SERIKALI

 Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA ndugu Alphonce Malibiche akipokea tuzo toka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. John Pombe Joseph Magufuli wakati wa sherehe za ufunguzi rasmi wa maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Sabasaba yaliyofanyika hivi karibuni. NIDA ilikuwa mshindi wa kwanza katika kundi la banda bora kwa Wizara na Taasisi za Serikali.
 Wananchi wakijaza fomu za maombi ya Vitambulisho vya Taifa na huduma kwenye Banda la NIDA wakati wa maonyesho ya 41 ya Kimataifa ya Sabasaba. 
 Wananchi wakipata huduma kwenye banda la NIDA, ambapo huduma ya Usajili na Utambuzi inatolewa, kuchukua alama za kibaiolijia pamoja na utoaji Vitambulisho kwa wale watakaokidhi vigezo. 
 Baadhi ya Watumishi wa NIDA walioshiriki kufanikisha Maonyesho hayo wakiwa na nyuso za furaha baada ya kupokea Tuzo ya ushindi. Kutoka kulia ni Edna Wanna, akifuatiwa na Agnes Gerrald, Raymondn Sengate na Sarah Mashalla.
 Katikati ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na mratibu wa Banda la Maonyesho la NIDA akiwa ameshikiliwa Tuzo ya Ushindi pamoja na Ndugu Alphonce Malibiche Kaimu Mkuu wa Idara ya Uzalishaji Vitambulisho (kushoto) na kulia ni Ndugu Jamal Kaoneka wa Idara ya Uhamiaji wadau wakuu wa NIDA katika kufanikisha Usajili wa Vitambulisho.
Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa TRL ndugu Masanja Kadogosa akiwa kwenye picha ya pamoja na maafisa wa NIDA baada ya kutembelea Banda la NIDA na kuwapongeza kwa ushindi wa kishindo. Wengine katika picha kushoto ni ndugu Gideon Ndalu Mkurugenzi wa Mifumo ya Tehama NIDA na katikati ni Ndugu Alphonce Malibiche Kaimu Mkuu wa Idara ya Uzalishaji Vitambulisho.

No comments: