Tuesday, July 18, 2017

Mtanzania "Sensei Fundi Rumadha ( 4th Dan) Yondan" Apandishwa cheo na baraza la Karate Duniani

 

Sensei Kinjo, Gima, Yoshihiro Kancho Miyazato, sensei Fundi Rumadha na Sensei Rony Kluger toka Israel. Katika where za kupandiswa ngazi walimu kadhaa.
Masensei toka Ujerumani, Ureno, Uingereza, Japan, na Tanzania katika semina "Gasshuku" wakiwa na furaha nyingi.


Masters au walimu wakuu wa Okinawa Goju Ryu Jundokan So Honbu Karate-Do chini ya usimamizi wa mwenye kiti wake mkuu duniani, aliwafanyia mitihani ya mikanda myeusi zaidi ya walimu 15 toka nga ya pili" Nidan" hadi ngazi ya saba "Nanadan". Ngazi hizi zote kwa uramaduni wa mtindo huu wa Okinawa Goju Ryu huchukua miaka mingi sana kupandiswa ngazi kulinganusha na mitindo mingine.

Kongamano la Karate mtindo wa Goju Ryu katika chama cha Jundokan So Honbu hufanyika kila mwaka nchi za ulaya kwa kutembelewa na wakuu wake toka katika visiwa vya Okinawa kuwasahihisha mbinu za mafunzo na mikakati mipya ya chama na hatimae sasa kuwaalika walimu toka nje ya bara la ulaya kwa muda wa miaka zaidi ya miwili sasa ikiwemo Tanzania na Angola.

Mwaka huu, wakuu wapatao watano chini ya mwenye kiti sensei Yoshihiro "Kancho" Miyazato, Tetsu Gima sensei, Tsuneo Kinjo sensei na Miyazaki sensei na mjumbe mwingine pia. Wakuu wa Okinawa Goju, wametilia mkazo na msisitizo mkubwa sana kwa kuzimudu mbinu kwa kina na matuzi yake, na pia watoto wadogo kwani ndio walimu wa kesho.

Mengi juu la misafara hii nikuwajumuisha masensei wote wa chama cha Jundokan So Honbu, kuwasahihisha na kuwafundisha ngazi kwa wana Swahili kufanyiwa hivyo, kulikoni kufanya gharama za kwenda Okinawa, Japan kimafunzo.

Sensei Fundi Rumadha aliweza kufanya mitihani wake toka Dan ya tatu "Sandan" kwenda ngazi ya nne "Yondan" na kufauli vizuri chini ya waamuzi masters toka Okinawa chini
ya Miyazato sensei. Sensei Fundi Rumadha amepewa mamlaka kuwasaidia wanafunzi wake wa Tanzania, kuwafanyia mitihani na kuwapa "Dan" hadi ngazi ya pili " Nidan" sababu chama chake kuanzia Dan ya 3 hutolewa na Master Miyazato pekee hadi leo hii.

Nimatumai yetu wanachama wa Jundokan So Honbu Tanzania kujiwajibisha kimafunzo, na kuimarisha umadhubuti wa mbinu" Techniques" kulikoni kulenga sana ngazi bila msingi mazuri kimafunzo, hasa katika kufanya "Kata" na "Bunkai".

Sensei Fundi Rumadha ingawa sasa anashikilia ngazi ya daraja la nne "Yondan", na umahili wake wa Karate kwa zaidi ya miaka 38, alitoa Shukran zake kwa mlezi wake wa mafunzi tokea utotoni, mwalimu "Sensei Magoma N. Sarya chini ya uongozi wake "Bomani Brigade" kama ilivyojilikana "BB" na mwanzilishi hayati Nantambu Camara Bomani sensei, mwanzilishi wa Okinawa Goju Ryu Tanzania 1973.

Tanzania na Angola zinatarajia kuhudhuria maadhimisho ya miaka 65 tangu kuanzishwa kwa chama cha "Jundokan" na Master Eiichi Miyazato sensei huko Naha City, Okinawa mwezi wa Novemba 1918, kwa sasa kinaongozwa na mwanae Yoshihiro Kancho Miyazato.


https://www.facebook.com/fundi.romi
www.instagram.com/fundi_romi

No comments: