Sunday, July 9, 2017

KIJANA MJASILIAMALI AIOMBA SERIKALI IZITAMBUE BIDHAA ZA MBAO ILI APATE KIWANDA

Na Karama Kenyunko-Globu ya Jamii

, Mjasiliamali anayejihusisha na utengenezaji wa extension za Umeme kwa kutumia mbao, anaiomba Serikali izitambue bidhaa za mbao ili apate kiwanda kikubwa ambacho kitamuwezesha kutoa ajira kwa vijana na bidhaa hizo kufika hadi nje ya nchi.

Charles Antoni Sanga, ambaye ni mwafrica wa kwaza kugundua ujuzi wa kupitisha umeme kwenye mbao, ameongea hayo katika maonyesho ya 41 ya biashara (Sabasaba) yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Amesema, upitishaji wa Umeme kwenye mbao ni bora na siyo rahisi kusababisha shoti ya Umeme, pia ujuzi huo unatoa fursa kwa kuwainua wajasiliamali wanaochaji simu vibandani.

"Ninahamasidha kauli mbiu ya Mh.Rais kuwa Tanzania ya viwanda inawezekana sababu kuna vitu tunavyobuni watanzania ambayo ni imara kuliko vile vya kutoka nje ya nchi".

Aidha ameiomba Serikali na wadau mbali mbali wanaopenda bidhaa hizo za mbao kujitokeza na kumuinua kwani anafanya kazi katika mazingira magumu kwani hata TBS walimuagiza kuwa awe na karakana na machine Au hata jengo lakini hana chochote kwani hana fedha za kumuwezesha kuwa na vifaa hivyo.

Akielezea safari yake ya iliyomfikisha hapo anasema, alikuwa akiishi bila ya kipato chochote ndipo akaamua kubuni kitu ambacho hajawahi kukiona mahali popote ndipo akaja na wazo la extension ya mbao.

Anasema, alipokamilisha moja, watu wengi walivutiwa nayo ndipo akaamua kutengeneza kwa oda hiyo ilikuwa mwaka 2012 ambapo baadae alishiri maonyesho ya SIDO nyanda za juu kusini, huko alikutana na viongozi kutoka nchi mbali mbali wakiwemo TBS ambao walishangaa ubunifu huo ambao hawakuwa wameuona mahali popote duniani.

Sanga anaongeza, TBS walimshauri kwenda Tume ya Sayansi yabTeknolojia ili wachunguze kama bidhaa hiyo ipo mahali popote duniani lakibi haikuonekana mahala popote na kumfanya awe Mwafrica wa kwanza kupitisha umeme kwenye mbao.

Anasema, baada ya uchunguzi alifanikiwa kupata cheti cha ugunduzi (Patent) kwenda kwa mwanasheria Mkuu wa ugunduzi ambaye alisubiri pingamizi kwa muda wa miaka miwili lakini hakukuwa na pingamizi.

Sanga anawaomba wadau wajitokeze na kumuunga mkono ili aweze kutoa ajira kwa vijana hali kadhalik serikali imsaidie kuwezesha jambo hilo.
 Mgunduzi wa Soketi ya Mbao Charles Sanga akieleza Kwa Makini jinsi alivoweza kutengeneza Soketi hizo
 Charles Sanga akionesha moja ya Soketi aliyoitengeneza

No comments: