Monday, July 10, 2017

BENKI YA CRDB YASAIDIA UJENZI WA NYUMBA YA WALIMU KATIKA SHULE YA SEKONDARI LAIKALA KONGWA DODOMA

Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Kongwa, akisalimiana na Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB Dodoma, Bi. Rehema Hamisi wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa mifuko 200 ya Saruji iliyotolewa na Benki ya CRDB kwa ajili ya kusaidia Ujenzi wa Nyumba ya Walimu wa shule hiyo iliyopo jimboni kwake Kongwa mkoani wa Dodoma.
Spika wa Bunge, Job Ndugai, akisalimiana na Meneja wa Kituo cha Huduma kwa Wateja Njia ya Simu (Call Center), Ena Mwangama, wakati alipowasili katika Shule yua Sekondari ya Laikala.
Spika wa Bunge, Job Ndugai na Mkurugenzi wa Tawi la Benki ya CRDB Dodoma, Rehema Hamisi wakielekea shuleni hapo.
Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Tawi la Dodoma, Rehema Hamisi (wa pili kushoto), akipiga ngoma sambamba na wasanii wa kikundi cha Matumaini kilichokuwa kikitumbuiza katika hafla hiyo.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Laikala, Msafiri  Simon, akisoma historia fupi ya shule hiyo.
Mkurugenzi waBenki ya CRDB  Tawi la Dodoma, Bi. Rehema Hamisi, akisoma hotuba katika hafla ya kukabidhi msaada wa mifuko 200 ya Saruji iliyotolewa na Benki ya CRDB kwa ajili ya Kusaidia Ujenzi wa Nyumba ya Walimu katika Shule ya Sekondari Laikala. 
 Baadhi ya walimu na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Laikala wakisikiliza hotuba ya Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Tawi la Dodoma, Rehema Hamisi.
Spika wa Bunge, Job Ndugai, akizungumza katika hafla ya Benki ya CRDB kukabidhi mifuko 200 ya saruji.
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Laikala wakimsikiliza Spika wa Bunge na mbunge wa Jimbo la Kongwa, Job Ndugai wakati shule hiyo ilipopokea msaada wa Sh. Milioni 15 kutoka Benki ya CRDB kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya shule hiyo. 
Spika wa Bunge, Job Ndugai, ambaye pia ni mbunge wa Kongwa, akipokea mfano wa hundi  ya Sh. Milion 15 kutoka kwa Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Tawi laDodoma, Rehema Hamisi kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa nyumba ya walimu katika Shule ya Sekondari Laikala iliyopo wilayani Kongwa. Kulia ni Diwani wa Kata ya Sagala, Simon Kamando, akishuhudia.
Spika wa Bunge, Job Ndugai (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya CRDB Tawi la Dodoma pamoja na viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo.
 Wanafunzi wakifurahia mfano wa hundi iliyotolewa na Benki ya CRDB. 
  Sehemu ya mifuko ya sarui iliyokabidhiwa na Benki ya CRDB kwa Shule ya Sekondari Laikala. 
Spika wa Bunge, Job Ndugai, akitoa shukrani zake kwa Benki ya CRDB baada ya kupokea mifuko 200 ya saruji pamoja na hundi ya Sh. Milioni 15.
 Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya makabidhiano ya hundi ya Sh. Milioni 15 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa nyunba ya walimu pamoja na kuboresha miundombinu katika Shule ya Sekondari Laikala.
 Baadhi ya maofisa wa Benki ya CRDB.
 Baadhi ya wananchi wakifuatilia hafla ya makabidhiano ya mifuko ya saruji.
Baadhi ya maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika hafla hiyo.

No comments: