Thursday, July 27, 2017

BARAZA LA MADIWANI KISHAPU MKOANI SHINYANGA WAPONGEZWA KWA HATUA YA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO KWA UFANISI PAMOJA NA CHANGAMOTO ZA UHABA WA FEDHA


Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu, Boniphace Butondo akizungumza wakati akifungua kikao cha Baraza la Madiwani la kupokea na kujadili tarifa za kata za robo ya nne ya mwaka. Wengine pichani kushoto ni Makamu mwenyekiti wa halmashauri, Edward Shigela na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Stephen Magoiga.

Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga akizungumza wakati wa kikao hicho. Wengine pichani kuanzia kushoto ni Katibu Tawala Wilaya, Shadrack Kangese, Makamu mwenyekiti wa halmshauri, Edward Shigela na Mwenyekiti Boniphace Butondo.

Madiwani na wataalamu kutoka halmashauri hiyo wakifuatilia kikao hicho cha kupokea na kujadili tarifa za maendeleo ya kata.

Katibu Tawala Wilaya ya Kishapu, Shadrack Kangese akizungumza neno wakati wa kikao hicho.

Makamu mwenyekiti wa halmshauri, Edward Shigela akizungumza wakati akifunga kikao hicho.

Madiwani na wataalamu kutoka halmashauri hiyo wakifuatilia kikao hicho cha kupokea na kujadili tarifa za maendeleo ya kata.


………………………………


Na Robert Hokororo

Halmashauri ya wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga imepongezwa kwa hatua yake ya utekelezaji miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ufanisi pamoja na changamoto za uhaba wa fedha.

Pongezi hizo zimetolewa leo na mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Boniphace Butondo wakati akifungua kikao cha Baraza la Madiwani kilichoketi kupokea taarifa za kata kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka.Butondo alisema miradi hiyo imetekelezwa kwa kiwango kizuri pamoja na changamoto ya uhaba wa fedha iliyoikabili halmashauri hiyo kwa kipindi hicho.

Alisema ushirikianoa baina ya madiwani na wataalamu kutoka halmashauri hiyo ndiyo siri ya mafanikio hayo ambayo ni tija kwa wananchi wanaowahudumia.Aidha, aliwapongeza wataalamu hao kutoka idara mbalimbali kwa kuwa na usimamizi mzuri ikiwemo wa fedha na maeneo ambayo miradi hiyo inatekelezwa na kuwataka waendelee kushikamana.

“Naomba niwapongeze wote kwa ushirikiano mkubwa mnaounesha najua kuna changamoto ya kuwa na mapato kidogo kutokana na hali ya hewa na hivyo kuchangia kutopata pamba kwa wingi ambayo inaingiza mapato halmashauri,” alisema.

Mwenyekiti huyo ambaye pia ni diwani wa kata ya lagana aliishukuru ofisi ya mkuu wa wilaya kwa ushirikiano mkubwa kwa halmashauri na hivyo kuchangia mafanikio hayo.

Tayari miradi mbalilimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa, zahanati, barabara na maji imetekelezwa katika kata mbalimbali za halmashauri ya wilaya hiyo.

No comments: