Friday, June 9, 2017

SPIKA NDUGAI ATEMBELEWA NA BALOZI MDOGO WA MAREKANI NCHINI TANZANIA LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Balozi mdogo wa Marekani nchini Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Inmi Patterson, pale alipomtembelea leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akipokea zawadi ya saa kutoka kwa Balozi mdogo wa Marekani nchini Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Inmi Patterson, pale alipomtembelea  leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza jambo pale alipotembelewa na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini Tanzania, wakiongozwa na Balozi wa Uingereza nchini, Mheshimiwa Sarah Cooke(kulia kwake) katika kikao kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati)akimsikiliza Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mheshimiwa Sarah Cooke (wa pili kushoto) pale Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini Tanzania walipomtembelea leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akizungumza na Balozi kutoka Norway, Mheshimiwa Hanne Kaarstad (katikati) na Balozi kutoka Finland Mheshimiwa, Pekka Hukka (kulia) katika kikao kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mheshimiwa Hawa Ghasia (wa pili kulia) akiongoza kikao cha pamoja cha mashauriano kati ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti pamoja na Wadau wa Mashirika ya Maendeleo Duniani, kutoka Benki ya Dunia (World Bank) na Shirika la fedha la kimataifa (IMF) kilichofanyika leo ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma.
Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti na Wadau kutoka Mashirika ya Maendeleo Duniani wakiwa katika kikao cha Mashauriano ya pamoja kilichofanyika leo ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments: