Tuesday, June 20, 2017

KAMPUNI YA MAWASILIANO YA ZANTEL YAJUMUIKA NA WAFANYAKAZI NA WADAU WAKE KWA FUTARI JIJINI DAR



Baadhi ya wafanyakazi wa Zantel wakijumuika katika tafrija ya futari maalumu kwa ajili yao katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam
Meneja Chapa na Mawasiliano wa Zantel, Rukia Mtingwa (kushoto) akitoa huduma ya chakula kwa baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni hiyo waliojumuika na wateja na wadau mbalimbali katika tafrija ya futari iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu Zantel, Joanitha Mrengo (wa pili kushoto) akitoa huduma ya chakula kwa Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Benoit Janin (wa kwanza kulia) katika tafrija ya futari iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Tafrija hiyo ilikuwa ni mahususi kwa ajili ya wafanyakazi na wadau wa kampuni hiyo. Anayeshuhudia (kushoto) ni Afisa wa Kitengo cha Rasilimali watu Zantel, Maryam Khatri.
Afisa wa Kitengo cha Rasilimali watu Zantel, Maryam Khatri (kushoto) akitoa huduma ya chakula kwa Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Benoit Janin (kulia) katika tafrija ya futari iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Tafrija hiyo ilikuwa ni mahususi kwa ajili ya wafanyakazi na wadau wa kampuni hiyo.
Afisa wa Kitengo cha Rasilimali watu Zantel, Maryam Khatri (kushoto) akitoa huduma ya chakula kwa wafanyakazi wa Zantel katika tafrija ya futari iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Tafrija hiyo ilikuwa ni mahususi kwa ajili ya wafanyakazi na wadau wa kampuni hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Zantel wakijumuika kupata futari katika tafrija iliyoandaliwa na Kampuni hiyo katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani ambayo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin akizungumza wakati wa tafrija ya futari maalumu iliyoandaliwa na Kampuni hiyo kwa ajili ya wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu Zantel Joanitha Mrengo akizungumza wakati wa tafrija ya futari maalumu iliyoandaliwa na Kampuni hiyo kwa ajili ya wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin (wa kwanza kushoto) akifurahia jambo na baadhi ya viongozi wa Kampuni hiyo wakati wa tafrija ya futari iliyoandaliwa na Zantel kwa ajili ya wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kipindi hiki cha mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Tafrija hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.

No comments: