Saturday, May 6, 2017

YANGA YAJIKITA KILELENI YAIPIGA TANZANIA PRISONS 2-0

Mshambuliaji wa Yanga, Geofrey Mashiuya (kulia), akichuana na beki wa Tanzania Prisons, Michael Ismail. (Picha na Francis Dande). 

 Kipa wa Tanzania Prisons, Aron Kalambo, akipata huduma ya kwanza baada ya kuumia katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya Yanga uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga ilishinda 2-0. 


Mshambuliaji wa Yanga, Geofrey Mashiuya (kulia), akichuana na beki wa Tanzania Prisons, Nurdin Chona katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga ilishinda 2-0. 
Beki wa Yanga, Vincent Bossou akimtoka kipa wa Tanzania Prisons, Aron Kalambo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya Yanga uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao lililofungwa na Obrey Chirwa.
 Mashabiki wa Yanga wakishangilia.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia.

No comments: