Tuesday, May 30, 2017

TWIGA CEMENT KUENDELEA KUWA VINARA WA UZALISHAJI SARUJI LICHA YA KUIBUKA KWA MAKAMPUNI MENGINE NCHINI

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Kampuni ya Saruji nchini ya Tanzania Portland Cement inayozalisha Twiga Cement, imesema kuwa itaendelea kuwa kinara kwa mauzo ya Saruji hapa nchini, licha ya kuwepo wa viwanda vingi katika miaka ya hivi karibuni.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa kampuni hiyo Alfonso Velez, alipokuwa akitoa ripoti ya mauzo ya kampuni hiyo na changamoto inazokabiliana nazo katika mkutano wa wanahisa wa kampuni hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.

“licha ya makampuni mengine kuja na mpango wa ujanja wa kushusha gharama za saruji bado Twiga Cement imeendelea kuwa ndio saruji bora kwenye soko licha ya changamoto ya kupambana na bei ya soko”

Amesema wao wameshuhudia wakiona washindani wao wakihangaika juu ya upataji wa mali ghafi ambazo zitaweza kuwasaidia kuendelea kufanya bishara kwa bei ya chini lakini TPCC bado haijatetereka.

Amesema kuwa mshindani wake bado ana wakati mgumu kwani yuko mbali na soko na inamchukua muda mrefu kusafirisha mzigo mpaka sokoni hivyo wakati wowote atapandisha bei ya saruji na Twiga itabaki pale pale, kwani ameweza kufanya hivyo katika nchi zingine alizowekeza ambapo amepandisha bei kuwa juu hili kufidia gharama za uzalishaji.
Mwenyekiti wa bodi ya kampuni ya TPCC , Osward Urasa akizungumza katika mkutano huo juu ya wanahisa kutoa taharifa zitakazosidia kujenga kampuni kuzidi kuwa imara.
Mwenyekiti wa kampuni ya Tanzania Portland Cement, Alfonso Rodriguez akizungumza katika mkutano huo wa wanahisa wa kampuni hiyo uliofanyika leo katika hotel ya Ramada
Mkaguzi wa Mahesabu wa kampuni hiyo kutoka kampuni ya Ernist nd Young , Elibariki Fanuel akieleza juuya mehesabu ya mwaka ya kampuni hiyo
Mkurugenzi wa Twiga Cement Alfonso Velez akizungumza juuya mafanikio ya kampuni hiyo mara baada ya kuwepo wa ushindani wa makampuni mengine nchini
Sehemu ya Wanahisa katika mkutano huo wakiwa wanasikiliza kwa makini
Profesa akijadili jambo na wakurugenzina uongozi wa juu wa Twiga Cement
Katibu wa kampuni TPCC,Brain Kangeta akizungumza wakati wa mkutano huo wa wanahisa na wateja wa Twiga Cement
Mwanahisa Christopher Mvemo akichangia jambo juu ya kuboresha kampuni hiyo ili izidi kuwa kinara wa mauzo ya Saruji
Mwana hisa , Godfrey Marik akiuliza swali juu ya mipango ya kampuni katika kuhimili ushindani na makampuni mengine
sehemu ya wajumbe wa mkutano huo waliohudhuria

No comments: