Monday, May 29, 2017

TACAIDS YATOA SEMINA KWA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI JUU YA MAAMBUKIZI YA UKIMWI -MJINI DODOMA

Semina ya wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari kuhusu VVU na Ukwimu iliyoandaliwa na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania TACAIDS,mjini Dodoma.

Miongoni mwa masuala yaliyozungumzwa katika semina hiyo ni changamoto mbalimbali zinazoikabili Tanzania katika mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi.

Changamoto hizo ni pamoja na Sheria ya Magereza, adhabu ndogo kwa wanaoambukiza watu wengine VVU kwa makusudi zilizoanishwa katika Sheria ya Ukimwi, mila na desturi zilizopitwa na wakati (ukiwamo ukeketaji) na unyanyasaji wa kijinsia.

Mzungumzaji mkuu katika semina alikuwa ni Mkuu wa Kitengo cha Sheria Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania TACAIDS,  Elizabeth Kaganda. 
 Mkuu wa Kitengo cha Sheria wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania TACAIDS,  Elizabeth Kaganda akitoa elimu ya sheria ya maambukizi ya ukimwi wakati wa semina ya wahariri wa vyombo  vya habari na waandishi wa habari kuhusu VVU na Ukwimu iliyoandaliwa na Tacaids mjini Dodoma.
  Mkutumbi (LIBRARIAN) Bwana Elisha Mngale kutoka Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania TACAIDS, akifafanua tafiti za maambukizi ya Ukimwi zinazofanywa na Tume hiyo.
 Waandishi wakitoa taarifa mbalimbali na changamoto zinazohusiana na maambukizi ya ukimwi wakati wa semina ya wahariri wa vyombo  vya habari na waandishi wa habari kuhusu VVU na Ukwimu iliyoandaliwa na Tacaids iliyofanyika mjini Dodoma.
Waandishi wa habari pamoja na wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali wakifuatilia mada katika semina hiyo.

Picha zote na Philemon Solomon.

No comments: