Monday, May 22, 2017

BODI YA (AQRB) YAWAPA ELIMU WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MAJANI YA CHAI JUU YA FANI YA UBUNIFU MAJENGO.


  Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadriaji Majenzi (AQRB) , Dkt Geraldine Kikwasi akizungumza na Wanafunzi wa kidato cha pili wa shule ya Sekondari Majani ya Chai iliyoko wilayani Ilala, jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya kuwahamasisha Wanafunzi wa kidato cha pili wa shule hiyo kuwapa elimu kuhusiana na fani mbili za ubunifu majengo na Wakadriaji Majenzi kwa masomo ya sayansi.
ARCH. Daniel Matondo kutoka Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadriaji Majenzi akiwaelezea Wanafunzi wa kidato cha pili wa shule ya Sekondari Majani ya Chai shughuli mbalimbali zinazofanywa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadriaji Majenzi katika sekta ya ujenzi.
Mwalimu wa shule ya Sekondari Majani ya Chai akiwasisitizia wanafunzi kusoma zaidi masomo ya sayansi wakati wakati wa ziara ya kuwahamasisha Wanafunzi wa kidato cha pili wa shule hiyo.

Wanafunzi kutoka chuo cha ardhi. wanayesomea fani ya Wabunifu Majengo wakiwapa elimu wanafunzi kuhusiana wasomo ya fani ya wabunifu majenge.
Afisa Uhusiano kutoka Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadriaji Majenzi (AQRB) Bw.Hamis Sungura. akiwatambulisha viongozi wa Bodi.
Wanafunzi wa kidato cha pili wa shule ya Sekondari Majani ya Chai iliyoko wilayani Ilala, jijini Dar es Salaam wakifuatilia elimu ya fani mbili ya ubunifu majengo na Wakadriaji Majenzi kwa masomo ya sayansi.
Viongozi wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadriaji Majenzi (AQRB) , wakiwasili katika Shule ya Sekondari Majani ya Chai iliyoko wilayani Ilala, jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya kuhawamasisha Wanafunzi wa kidato cha pili wa shule hiyo kuwapa elimu kusomea fani mbili za ubunifu majengo na Wakadriaji Majenzi kwa masomo ya sayansi (mbele kulia) Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadriaji Majenzi, Dkt Geraldine Kikwasi, katikati ARCH Daniel Matondo na Kushoto Afisa Uhusiano wa Bodi Bw.Hamis Sungura.

No comments: