Tuesday, April 18, 2017

TTCL YAKUTANA NA MAWAKALA ZAIDI YA 50 WILAYA YA TEMEKE

 Meneja Msaidizi wa wa mkoa wa Dar es Salaam Kusini wa mtandao wa simu ya Mkononi ya TTCL, Mwanaisha Semboko  akizungumza na Mawakala wa kuuza laini za Mtandao wa TTCL na kuwaeleza namna ya kuwafikia wananchi ambao hawajapata kuwa na laini za mtandao huo ili waweze kupata kutumia .

Semboko amesema kuwa Mtandao wa TTCL ni mtandao wa bei rahisi na wakizalendo, kwani fedha ambayo watapata kuchangia watanzania ni fedha ambayo inarudi katika maisha yao ya kila siku kwa kuendelea kujenga miundombinu ya mawasiliano ya Taifa hili .
 Baadhi ya Mawakala wakimsikiliza, Semboko wakati wakitoa mada ya faida za kuwa wakala wa mtandao huo
 Mratibu wa mkutano huo kutoka Makangarawe Youth , Ismail Mnikite  akizungumza na Mawakala waliofika katika mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam
 Afisa Mauzo wa mkoa wa Dar es Salaam Kusini , Amina Salum  akizungumza na mawakala hao juu ya uzwaaji wa laini za TTCL na faida zake na kutaja kuwa ni mtandao wa gharama nafuu katika data kuliko yote
 Mmoja wa mawakala walioshiriki mkutano huo , Monica Harry akiuliza swali juu ya huduma zinazotolewa na matandao wa simu za mkononi wa TTCL
 Baadhi ya mawakala wakisikiliza kwa makini namna ya kuwaunganisha watu katika mtandao wa TTCL

No comments: