Wednesday, April 12, 2017

KUMBUKUMBU YA MIAKA 33 YA KIFO CHA HAYATI EDWARD MORINGE SOKOINE WILAYANI MONDULI

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye ibada ya kuadhimisha miaka 33 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Marehemu Edward Moringe Sokoine
 Wajane wa Marehemu Sokoine Mama Napono Katrika (kati) Mama Nekiteto (kulia), wakiwa na waziri wa maliasili na utalii Profesa Jumanne Maghembe nyumbani kwao Wilayani Monduli
 Msaidizi wa Askofu, Prosper Lyimo akihubiri wakati wa ibada ya kuadhimisha miaka 33 ya kifo cha Waziri Mkuu wa Zamani, Marehemu Edward Moringe Sokoine
 Binti wa Sokoine Namelok na Kaka yake, Balozi Joseph Sokoine wakiwa na wageni wengine walioshiriki ibada ya kumbukumbu ya baba yao wilayani Monduli.
 Wajane wa marehemu Sokoine wakiweka shada la maua katika kaburi la Hayati Edward Sokoine, wilayani Monduli.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe akiweka shada la maua katika kaburi la Hayati Edward Sokoine, wilayani Monduli wakati wa kumbukizi ya kifo cha kiongozi huyo kilichiotokea miaka 33 iliyopita  nyumbani kwa Sokoine
 Mwakilishi wa mkuu wa Majeshi Tanzania, Brigedia Jenerali Anderson Ghulila akiweka shada la maua katika kaburi la Hayati Edward Sokoine, wilayani Monduli katika ibada ya kumbukumbu ya kifo cha kiongozi huyo kilichotokea miaka 33 iliyopita 
 Wajukuu wa Hayati Edward Sokoine wakiwa katika ibada ya kumbukumbu ya kifo cha kiongozi huyo miaka 33 iliyopita, iliyofanyika nyumbani kwa Sokoine 
 Mtoto wa Hayati Sokoine, Balozi Joseph Sokoine akizungumza na wageni waalikwa katika misa maalum ya kumuenzi baba yake.
 Baadhi ya wageni kutoka sehemu mbalimbali waliohudhuria misa ya kumbukumbuku ya Sokoine.
 Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka akibadilishana mawazo na mwakilishi wa mkuu wa Majeshi Tanzania, Brigedia Jenerali, Anderson Ghulila pamoja aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha, Balozi Daniel Ole Njoolay
 Baadhi ya viongozi walioshiriki ibada ya kumbukumbu ya miaka 33 ya Sokoine, kutoka kushoto ni Askofu wa Dayosisi ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Mkoani Arusha, Solomon Masagwa, Mwakilishi wa Shehe Mkuu, Rajab Kiungiza, Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka na Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe
 Wanakwaya wakiandamana kuelekea eneo la ibada tayari kwa Misa Maalum
Msaidizi wa Askofu, jimbo kuu Katoliki Arusha, Prosper Lyimo akiweka shada la maua kwenye kaburi la Waziri Mkuu wa zamani, Hayati Edward Moringe Sokoine wakati wa ibada ya kumbukumbu ya kifo cha kiongozi huyo miaka 33 iliyopita, iliyofanyika nyumbani kwa Sokoine wilayani Monduli. Picha zaote na Pam Mollel wa Globu ya Jamii, Monduli

No comments: