Friday, April 14, 2017

CHUO CHA SHENYANG CHA CHINA CHATOA UFADHILI KWA AIR TANZANIA NA NIT

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Chuo kikuu cha shenyang kutoka nchini China kimeahidi kutoa ushirikiano na Shirika la ndege la Air  Tanzania kwa kutoa msaada wa kuwasomesha wafanyakazi wa kampuni hiyo,ili waweze kumudu ushindani wa soko la kimataifa.

Hayo yamesemwa na mwalimu wa malezi wa chuo cha Shenyang, Shi Guangda katika mkutano ulioandaliwa na Taasisi ya Global Education Link kwa wazazi ambao watoto wao wanasoma urubani na Masuala ya anga katika chuo hicho.

“Tangu Rais wetu wa China alipofika hapa tumekuwa na mahusiano makubwa na nchi hizi mbili, hivyo kwa kuanza kama chuo chetu tutatoa ufadhili kwa wafanyakazi wa shirika la ndege la Air Tanzania na kubadilishana mafunzo katika chuo cha usafirishaji cha NIT na Shenyang” Amesema Guangda .

Kwa upande wa Mkurugenzi mkuu wa shirika la ndege la Air Tanzania,Ladislaus Matindi ameishukuru tasisi ya Global Education Link kwa  kuwaunganisha na chuo hicho ambacho kwa sasa kimekuwa msaada mkubwa kwa kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa shirika hilo.

Matindi ametaja kuwa upatikanaji wa nafasi hiyo itasaidia kutoa motisha kwa vijana wetu ambao wanafanya kazi katika shirika hilo na wengine ambao wako nje kuwa na hamu ya kusoma masuala ya usafirishaji .

Kwa upande wake mkurugenzi wa Global Education link , AbduMalik Molell alitumia fursa hiyo kuzungumza na wazazi hao juu ya swala la bima ya wanafunzi amabo wanasoma chuo hicho katika swala zima la matibabu na majanga mengine ambayo yatawakuta wanafunzi.


Mkurugenzi wa Global Education Link, AbdulMalik Mollel akimkabidhi hati ya ufadhili wa masomo Mkurugenzi wa shirika la ndege nchini Air Tanzania,Ladislaus Matindi kwa ajili ya wafanyakazi wa shirika hilo watakotakiwa kwenda kusoma China
Mkurugenzi wa Shirika la Ndege la Air Tanzania Ladislaus Matindi akizungumza na wazazi ambao watoto wao wanasoma masuala ya Anga nchini China
Mkurugenzi wa Global Education Link, AbdulMalik Mollel akifafanua jambo kuhusu masuala ya bima ya matibabu kwa wazazi ambao wamefika katika mkutano huo
Mlezi wa wanafunzi kutoka chuo Shenyang, akizungumza juu ya mazingira na ufadhili walio utoa nchini kwa shirika la ndege
Afisa Biashara mkuu kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara upande wa Tantrade, Stephene Kobelo akizungumza na wazazi juu ya namna watoto wanavyotakiwa kuitangaza nchi 
Baadhi ya Wazazi ambao wamefika katika mkutano huo wakisikiliza kwa makini juu ya swala zima la bima ya matibabu kwa wanafunzi
Baadhi ya wakurugenzi  wenza wa Tasisi ya Global Education Link wakisikiliza 
Mmoja wa wazazi akichangia jambo juu ya kuboresha bima ya wanafunzi wanaosoma China
Wazazi na baadhi ya ndugu ambao watoto wao wanasoma nchini China wakifatilia mkutano.

No comments: