Thursday, March 16, 2017

Wanawake wa Tanga Cement waadhimisha Siku ya Wanawake kwa kufanya mazoezi na kupima afya.


Meneja Rasilimali Watu wa Kampuni ya Saruji Tanga (TCPLC), Diana Malambugi (wa pili kulia), Meneja Mawasiliano na Mahusiano ya Nje wa Kampuni hiyo, Mtanga Noor (kulia), pamoja na baadhi ya wanawawake wafanyakazi wa Kampuni ya Saruji Tanga pamoja na wake wa wafanyakazi,  wakishiriki mbio za pole pole kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani zilizoanza eneo la Kange na kumalizikia katika kiwanda cha kampuni hiyo, Pongwe, nje kidogo ya mji wa Tanga juzi. 
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk. Amina Mchalaganya (wa pili kulia), baadhi ya wanawawake wafanyakazi wa Kampuni ya Saruji Tanga pamoja na wake wa wafanyakazi, wakishiriki mbio za pole pole (jogging), kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani zilizoanza eneo la Kange na kumalizikia katika kiwanda cha kampuni hiyo, Pongwe nje kidogo ya mji wa Tanga. 
Meneja Rasilimali Watu wa Kampuni ya Saruji Tanga (TCPLC), Diana Malambugi (wa pili kulia), Meneja Mawasiliano na Mahusiano ya Nje wa Kampuni hiyo, Mtanga Noor (kushoto), Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk. Amina Mchalaganya (wa pili kushoto), pamoja na baadhi ya wanawawake wafanyakazi wa Kampuni ya Saruji Tanga pamoja na wake wa wafanyakazi, wakishiriki mbio za pole pole kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani zilizoanza eneo la Kange na kumalizikia katika kiwanda cha kampuni hiyo, Pongwe, nje kidogo ya mji wa Tanga.
Meneja Mawasiliano na Mahusiano ya Nje wa Tanga Cement, Bi. Mtanga Noor (kulia), akitoa zawadi kwa baadhi ya wanawake waliohudhuria maadhimisho hayo. 
Baadhi ya washiriki katika hafla hiyo wakiselebuka mara baada ya kumaliza mbio na tukio la kupima afya zao ambapo wanawake hao walipimwa na kupewa elimu kuhusu ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi. 
Baadhi ya wanawake wafanyakazi wa Kampuni ya Saruji Tanga wakipiga picha ya kumbukumbu katika hafla hiyo. 
Baadhi ya washiriki wakifanya vitu vyao katika sherehe za maadhinisho ya Siku ya Wanawake Dunia ambayo kwa mwaka 2017 Kampuni ya Tanga Cement waliadhimisha kwa kufanya mazoezi, kupima afya na kupata mafundisho kuhusu masuala ya ujasiriamali.

No comments: