Monday, March 20, 2017

Shirika la Amend na Taasisi za Puma na Fia zapania kuondoa ajali za barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi



Mkurugenzi wwa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Kazi, Injinia Julius Chambo akizungumza katika uzinduzi wa programu ya kuboresha miundombinu ya usalama wa Barabarani kwa shule za msingi iliyoanzishwa na  Shirika la Amend kwa kushirikiana naTaasisi za Puma Energy na Fia. Mpango huo uliozinduliwa katika shule ya msingi Mpakani, Manzese Tip Top  umeanzishwa kwa lengo la kuwakinga wanafunzi wa shule za msingi kupata ajali za barabarani. 
 Meneja Mkuu wa kampuni ya Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa program ya ujenzi na uboreshaji wa mindombinu ya usalama wa barabarani kwa shule za msingi. Corsaletti alianisha kuwa usalama barabarani ni ajenda namba moja kwa kampuni yao na mpaka sasa wamekwisha toa  mafunzo ya aina hayo kwa wanafunzi 39,000 kutoka shule 33 mbalimbali za mkoa wa Dar es Salaam na Geita.
 Mkurugenzi wa Mpango hu wa Shirika la Amend, Ayikai Poswayo kutoka Ghana akizungumza katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi wwa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Kazi, Injinia Julius Chambo akikata utepe kuzindua mpango wa kuwalinda wanafunzi wa shule za msingi kupatwa na ajali za Barabarani ulionzishwa na Shirika la Amend kwa msaada wa taasisi ya Puma Energy na Taasisi ya Fia kwenye shule ya msingi Mpakani ya Manzese Tip Top. Wengine katika picha ni Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti (wa tano kutoka kushoto), Mkurugenzi wa Amend, Ayikai Poswayo (wa kwanza kulia) na Diwani Kassim Lema ( wa kwanza kushoto).
 Washiriki katika uzinduzi huo wakiwa katika picha ya pamoja kwenye eneo ambalo limetengenezwa rasmi kwa ajili ya kutumiwa na wanafunzi wa shule ya msingi Mpakani kuvuka wakati wa kwenda na kutoka shuleni.
 Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi, Thabitha  Makaranga akizungumza katika hafla hiyo. Makaranga aliwamwakilisha Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama wa Barabarani, Naibu Kamishna, Mohamed Mpiga.
Wakufunzi wa masuala ya usalama barabarani kutoka shirika la Amend na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mpakani iliyopo Manzese Tip Top  wakionyesha kwa mfano njia sahihi ya kuvuka barabara.



Tanzania ni miongoni mwa nchi 10 zitakazofaidika na mpango wa kuwakinga wanafunzi wa shule za msingi kupata ajali za barabarani ulioanzishwa na shirika la kimataifa la Amend kwa msaada mkubwa wa taasisi ya FIA Foundation na Puma Energy Foundation. 


Mpango huo ulizinduliwa juzi kwenye shule ya msingi mpakani iliyopo Manzese Tip Top ambao lengo kubwa ni kujenga miundombinu itakyosaidia wanafunzi kuepuka ajali za barabarani waendapo, wakati wa kuvuka na kurejea kutoka shuleni.

Nchi nyingine ni Benin, Botswana, Ivory Coaste, Ghana, Malawi, Mozambique, Namibia, Senegal na Zambia.

Mkurugenzi wa mpango huo kutoka shirika la Amend, Ayikai Poswayo kutoka Ghana alisema kuwa takwimu si nzuri kwa Tanzania kuhusiana na ajali za barabarani ambapo inakadiliwa kuwa jumla ya watu 16,000 upoteza maisha kutokana na ajali hizo kila mwaka.

Poswayo alisema kuwa kutokana na taasisi yao kujishughulisha na masuala ya usalama wa barabarani katika bara la Afrika, waliamua kuzindua mpango huo hapa nchini kwa lengo la kuwalinda wanafunzi na watu wengine wanaotumia barabara wakati wa shughuli zao za kila siku.

Alifafanua kuwa mpango huo utahusisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ambayo itatumiwa na watembea kwa miguu, waendesha pikipiki, baiskeli na magari kuepuka ajali hizo ambazo nyingi zimeleta madhara kwa watu na wenginekubakia na ulemavu kama si kupoteza maisha.

“Huu ni mradi wa miaka miwili ambao malengo yake makubwa ni kuwakinga wanafunzi kwenye ajali za barabarani, takwimu siyo nzuri kwa Tanzania, hivyo tumeamua kuanzia hapa na baadaye unzinduzi kama huu kufanyika nchi nyingine, tutajenga miundombinu amayo itawafanya madereva wa vyombo vya moto kuendesha vyombo vyao kwa mwendo wa wastani, mradi huu utafanyika kwenye shule zote zilizopo karibu na barabara,” alisema Poswayo.

Meneja Mkuu wa kampuni ya Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti alisema kuwa wanawajibika katika mpango huo kwani ni sehemu ya shughuli zao za kijamii.

Corsaletti alisema kuwa usalama barabarani ni ajenda namba moja kwao na mpaka sasa wameweza kutoa mafunzo ya aina hayo kwa wanafunzi 39,000 kutoka shule 33 mbalimbali za mkoa wa Dar es Salaam na Geita.

Corsaletti alisema kuwa wanafunzi wengi wanakabiliwa na hatari ya kupoteza maisha au kupata ulemavu kutokana na ajali ambazo zinatokana na uendeshaji mbaya wa madereva au kukosekana kwa miundombinu ambayo sahihi kuwawezesha wanafunzi kuona kabla ya kuvuka barabara.

Mkurugenzi wwa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Kazi, Injinia Julius Chambo aliipongeza Shirika la Amend, Puma Energy na Taasisi ya Fia kwa kuanzisha mpango huo ili kuwakinga wanafunzi wa shule za msingi.

Injinia Chambo alisema kuwa takwimu za mwaka 2015 za ajali ya barabarani zinaonyesha kuwa zinaonyesha kuwa jumla ya wanafunzi 78 walipoteza maisha kwa mkoa wa Dar es Salaam kutokana na ajali za barabarani. Pia jumla ya watu wanafunzi 182 walijeruhiwa.

“Hali si nzuri, napongeza juhudi za wadau zinazolenga kupunguza ajali za barabarani, kuna makampuni mengi ambayo hayajihuishi na shughuli kama hizi, naziomba ziunge mkono sasa ili kuboresha miundombinu na kuepusha maisha ya wanafunzi,” alisema Chambo.

Alisema kuwa serikali inaiunga mkono juhudi za Puma Energy, taasisi ya Fia na Amend na ipo tayari kutoa ushirikiano ili kuondoa tatizo hili.

Mwisho…

No comments: