Tuesday, March 7, 2017

NMB yamwahidi Rais Magufuli kuendelea kutumia mfumo wa kieletroniki

Benki ya NMB imemwakikishia Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kuwa itaendelea kutumia mifumo ya kiteknolojia ili kuwawezesha wateja wa benki hiyo kutumia Zaidi mifumo ya kietroniki kuliko unaotumika Zaidi kwa sasa wa malipo kwa kutumia pesa taslim.

Hayo ya mesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa NMB, Ineke Bussemaker wakati wa ufunguzi wa Kituo cha Kibiashara cha Mtwara na kueleza kuwa nia ya benki ni kuendelea kukua Zaidi huku ikitoa suluhu ya vipau mbele vya serikali na kujikita katika ukusanyaji wa mapato ya serikali kwa njia zakielektroniki.

“Kwa kutumia teknolijia mbalimbali, NMB tumewekeza Zaidi kwenye kutatua changamoto mbalimbali za wateja wetu na hivyo kutoa fursa za kutumia Zaidi njia za benki kuliko kutumia njia za malipo kwa kutumia pesa taslim,” alisema Ineke.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NMB, Prof. Joseph Semboja alisema kuwa NMB imefanya maboresho makubwa na hivyo kuwa na uwezo mkubwa wa kutoa huduma za kifedha kwa kila kada ya watanzania na serikali kwa ujumla.

Prof. Semboja alisema kuwaSerikali kwa sasa inamiliki hisa asilimia 32 ndani ya benki ya NMB zenye thamani ya Zaidi ya Bilioni 430 hivyo kuiwezesha serikali kupata gawio la Zaidi ya bilioni 75 ndani ya miaka mitano.

“Kwa mwaka huu mheshimiwa raisi, kama mkutano mkuu wa wanahisa utakaokaa mwezi wa sita mwaka huu, utabariki Kiwango cha gawio, serikali itapata gawio la shilingi Bilioni 16.5 zinazotokana na faida iliyopatikana mwaka 2016,” alisema Prof. Semboja.

Nae Rais Magufuli aliwapongeza NMB kwa huduma wanazotoa na kutoa wito kwa viongozi wa serikali na wakuu wa wilaya na viongozi waliopo ndani ya serikali kufanya biashara na NMB kwani serikali ina hisa kwenye benki hiyo na hupata faida kutoka NMB.

“Nikuombe Waziri, toa maelekezo kwa sababu wewe ndo unasimamia pesa, pesa ya serikali ipitie NMB ili nipate gawio kubwa zaidi, wale wengine wanaofanya biashara bila kuifaidisha serikali na kugawana gawio wao kwa wao huku serikali haipati faida yoyote, hatutafanya biashara nao,” alisemaRaisiMagufuli.

Rais Magufuli pia aliiomba NMB kushiriki katika kuunga mkono ajenda ya serikali katika kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.

Rais Magufuli alisema kuwa,“Naomba NMB mshiriki katika kukopesha viwanda hasa viwanda vidogovidogo na hivyo kuunga Mkono juhudi za serikali katika kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.”
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NMB Ineke Bussemaker mara baada kukifungua rasmi kituo cha Biashara cha NMB mjini Mtwara kijulikanac ho kama Mtwara Business Centre. Pamoja na mambo mengine, rais magufuli alimuagiza Waziri wa fedha Dr Philip Mpango kuhakikisha kuwa fedha zote za serikali zinapita NMB.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mkurgenzi wa NMB – Ineke Bussemaker wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa kituo cha kibiashara cha NMB – NMB Business Centre mjini Mtwara juzi. Kutoka kulia niAfisa Mkuu wa wateja wadogo na wa kati – Abdulmajid Nsekela, Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi – Prof Joseph Semboja na kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara – Halima Dendegu na Waziri wa Fedha na Uchumi – Dr Philip Mpango.

No comments: