Thursday, March 2, 2017

KAIMU RC TANGA AGIZA WILAYA ZA MKOA HUO KUUNDA MAJUKWAA YA WANAWAKE

KAIMU Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhandisi Mwanasha Tumbo ameziagiza wilaya zote za mkoa huu kuunda majukwaa ya wanawake kwa kipindi cha miezi mitatu ijayo ili yaweze kuwa chachu ya kuwakomboa kimaendeleo na kiuchumi.

Mhandisi Mwanasha ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza aliyasema hayo hivi karibuni  wakati akizindua jukwaa la wanawake mkoani Tanga ambalo litakuwa na malengo makuu ya kuwainua na kuwawezesha wanawake kiiuchumi lililofanyika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Alisema uwepo wa majukwaa hayo itasaidia kutoa fursa kwa wanawake kuweza kushiriki kikamilifu kwenye masuala mbalimbali ikiwemo kuwepo na majukumu ya kuwawezesha wanawake kuweza kujiinua kiuchumi kutokana na shughuli wanazozifanya zikiwemo za ujasiriamali.
Aidha pia aliwataka wanawake kuwa mstari wa mbele kuzalisha bidhaa bora na wenye kiwango cha kimataifa ili waweze kupata nafasi ya kuziuza ndani na nje ya nchi ili kuwasaidia kuongeza pato lao na Taifa kwa ujumla.
“Wajasariamali warasimishe biashara zao ili ziweze kutambulika
kisheria ikiwemo kulipa kodi lakini pia muachane na suala la
kujiingiza kwenye biashara haramu ambazo zinaweza kukatisha ndoto zenu “Alisema.
“Kupitia Jukwaa hili mnaweza mnalitumia kusaidia wanawake kujikwamua kiuchumi na kuweza kufia sera ya asilimia 50 kwa 50 hivyo ili kufikia huko jukumu lenu kuonyesha uwezo lakini pia wekezeni kwenye elimu kupitia mkusanyiko huu “Alisema.
Awali akizungumza Mjasiriamali wa kampuni ya kutengeneza Fenicha, za majumbani na maofisini mkoani Tanga Edna Boimanda aliwashauri wanawake kuunganisha nguvu za pamoja ili kuona namna ya kuanzisha benki ya wanawake kwani hiyo ndio fursa ya kipekee wanayoweza kujikwamua kiuchumi.
Alisema kupitia benki hiyo itawawezesha waanawake kujiletea maendeleo kwa kupata mikopo itakayokuwa chachu ya kufikia malengo yao ya kupata mafanikio.

Mmmoja wa Wajasiriamali kushoto akimuonyesha Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tangaa,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza akiangalia moja kati ya bidhaa wanazozalisha wakati wa kongamano la wanawake wajasiriamali mkoani Tanga lililofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga hivi karibuni.

 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto aliyevaa hijabu ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake wajasiriamali wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi karibuni.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza kulia akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake wajasiriamali wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi karibuni.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza kulia akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake wajasiriamali wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi karibuni.

Picha na habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

No comments: