Friday, March 31, 2017

DKT. KALEMANI ATAJA MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI KWA MWAKA 2016/17


Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani, Dkt. Medard Kalemani akiongea jambo wakati akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2016/17.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Dotto Biteko, akichangia Hoja baada ya Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa Mwaka 2016/17 kuwasilishwa kwa Kamati.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Susan Kiwango akichangia Hoja baada ya kuwasilishwa Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2016/17.
Mjumbe Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini, Mhe. Oscar Mkasa akichangia jambo wakati wakati wa kikao baina ya Kamati na Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake, ambapo Wizara na Taasisi ziliwasilisha Taarifa za Utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka 2016/17.
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gisima Nyamo- Hanga, akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya REA kwa mwaka 2016/17 kwa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Nishati na Madini.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Dkt. Tito Mwinuka akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka 2016/17 ya shirika hilo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.
Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Haji Janabi, akiwasilisha Taarifa ya Utekelzaji wa Wizara kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.
Baadhi ya Wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake wakifuatilia kikao baina ya Wizara ya Nishati na Madini na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.

…………………………………………………………………..

Wizara ya Nishati na Madini imekutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuanzia tarehe 27 Machi, 2017, ambapo Wizara na Taasisi zilizo chini yake zimewasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa Mwaka 2016/17.

Akielezea baadhi ya mafanikio ya Wizara kwa Kamati ya Bunge, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani, ametaja mafanikio hayo kuwa ni pamoja na;
 
Kukamilika kwa asilimia 100 kwa Mradi wa Kusafirisha Umeme kutoka Iringa hadi Shinyanga wenye msongo wa kilovoti (kV), 400.

Kukamilika kwa asilimia 98.5 ya Awamu ya Pili ya Mradi Kambambe wa Kupeleka umeme Vijijini unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini- REA.
Kuzinduliwa rasmi kwa Awamu ya Tatu ya Mradi Kabambe wa Kupeleka umeme Vijijjini unaolenga kusambaza umeme katika vijiji vyote visivyofikiwa na huduma hiyo.
 
Kukamilika kwa Kanuni za:
The Petroleum (Retail Operations in Townships and Villages) Rules,2016
The Petroleum (Natural Gas Pricing) Rules,2016
The Electricity (Supply Services) Rules, 2016

The Electricity (Market re- organization and competition) Rules,2016 na
The Mining (Minimum shareholding and Public Offering) Regulations 2016. Kanuni hizi zinasimamia utekelezaji wa Sheria zinazohusu Sekta za Nishati na Madini.

Kuanza kwa maandalizi ya utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Bandari ya Tanga, Tanzania.

Kuendeleza shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini ambapo hadi sasa jumla ya Futi za Ujazo Trilioni 57.25 za gesi asilia zimegunduliwa.
Kukamilisha utafiti wa jio-sayansi (jiolojia, jiokemia na jiofikizia katika mikoa ya Lindi na Mtwara na kuchora ramani za kuanisha kuwepo kwa madini mbalimbali ili kuhamasiaha uwekezaji kwenye maeneo ya Nachingwea, Ruangwa na Masasi.

Wizara kutenga maeneo 11 kwa ajili ya wachimbaji madini wadogo yaliyopo Msasa na Matabe Mkoani Geita, Biharamulo na Kyerwa yaliyopo Mkoani Kagera, Itigi, Mkoani Singida, D- Reef, Ibindi na Kapanda Mkoani Katavi, Ngapa Mkoani Songea, Nzega Mkoani Tabora na Kitowelo Mkoani Lindi. Maeneo hayo yana ukubwa wa takriban hekta 38.567
 

Kufanyika kwa minada miwili (2) ya madini ya vito hususan tanzanite jijini Arusha ambapo Serikali ilipata jumla ya shilingi milioni 793 ikiwa ni mrabaha uliolipwa Serikalini kutokana na minada hiyo.

No comments: