Saturday, February 11, 2017

RC IRINGA MWALIMU AMINA MASENZA AONYA WATUMISHI WANAOKWEPA MAZOEZI


Na MatukiodaimaBlog
MKUU  wa  mkoa  wa  Iringa mwalimu  Amina Masenza amewaonya  watumishi  wa serikali ambao wanakwepa  kushiriki mazoezi ya  pamoja katika  uwanja  wa  Samora  na  kuwa kuanzia sasa mtumishi atakayekwepa kushiriki  kubanwa.

Alisema pamoja na kuwa mazoezi  hayo ni kwa ajili ya afya za kila mmoja kujikinga na maradhi  yanayosababishwa na  kutofanya mazoezi ila  bado mazoezi hiyo  ni  utekelezaji wa agizo la makamu  wa Rais kwa  kila mtanzania.

Hivyo  alisema kutokana na baadhi ya  watumishi hasa  wanawake  kukwepa mazoezi hayo anaandaa mkakati wa kuwabana  watumishi  wote  wanaokwepa mazoezi kwa  kuitisha mazoezi  siku ya kazi ili wale  ambao  watashindwa  kufika watawajibishwa .

"Naangalia  ni  siku gani  ambayo  itakuwa ni  siku ya kazi kama ijumaa ama siku  nyingine  yeyote  ambayo  nitaitisha mazoezi kuanzia ofisi  yangu  hadi  Samora kwa  kila mtumishi kushiriki na siku hiyo hata ofisini  watumishi  wakichelewa ni  sawa lengo  kuweza  kufanya mazoezi na kutekeleza agizo la  serikali ......nashangazwa  sana  awali  wanawake  ndio  ambao  walikuwa  wakifika kwa  wingi mazoezini  ila leo  hii idadi ya  wanawake  imepungua ukilinganisha na  wanaume ....nawashangaa sana wanawake  wanaokwepa mazoezi  wakati  ndio ambao  wanakula vitu  vyenye mafuta "
Hivyo  alisema  kuanza sasa  kila mtumishi  wa serikali  lazima  kufika katika mazoezi na  utawekwa  utaratibu  wa  kuorodhesha majina kila idara  ya  watu  wanaoshiriki mazoezi .


Mkuu  wa  mkoa  wa  Iringa  mwalimu  Amina Masenza (wa tatu kushoto) akiongoza  mazoezi ya viungo katika  uwanja wa  samora  Leo wa  pili kushoto ni katibu  tawala wa mkoa  wa Iringa wamoja Ayubu

DC  Iringa  Richard  Kasesela wa kwanza  kulia  akishiriki mazoezi ya  riadha kutoka  uwanja  wa Samora

Washiriki wa  mazoezi  wakiwasili  ufisi ya  RC Iringa wakitokea  uwanja  wa  Samora


Afisa  michezo mkoa wa Iringa Kenedy Komba  akiorodhesha  majina  ya wakuu wa Idara  walioshiriki mazoezi leo ni  kuwabana wamnaokwepa mazoezi


Wanamazoezi  wakitoka  uwanja wa  samora


Mkazi  wa Iringa  akiwa amebeba  pombe aina ya  komoni asubuhi ya  leo pombe  hii inatengenezwa kwa mahindi jambo  ambalo  serikali  ya  mkoa imepigamarufuku matumizi mabaya ya  chakula

Mkazi  wa Iringa  akipishana na washiriki wa mazoezi huku  akiwa amebeba pombe ya  komoni inayotengenezwa  kwa mahindi

RAS  Iringa na RC Masenza kulia  wakiwa katika mazoezi

RC Iringa Amina Masenza  kulia  akiongoza mazoezi saa 12 asubuhi ya  leo

Afisa  habari Manispaa ya  Iringa  Sima Bingilengi kushoto  akiwajibika

Mwanahabari Manispaa ya  Iringa Janeth Matondo kulia pia  akishiriki mazoezi


DC  Kasesela katikati wa  pili  kulia akiwa na wadau  wa  kwanza  kulia ni Geofrey  Mungai
Mzee Vitus Mushi  akiwajibika mazoezini

DC  Iringa  Richard Kasesela  wa  tatu katikati  kulia akiwa na mkurugenzi Manispaa ya  Iringa Dr  Wiliam na mwanasheria  wa  Iringa wa  pili kulia



No comments: