Tuesday, February 21, 2017

Prof. Muhongo azindua Mafunzo ya taa, chaja za mionzi ya jua

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akionesha mfano wa Taa zinazotumia mionzi ya jua ambazo vijana 20 katika Kata ya Nyegina watafundishwa namna ya kuzitengeneza baada ya kuzindua mafunzo hayo. Kulia ni Balozi wa Korea Kusini nchini, Song Geumyoung na kushoto ni Mkufunzi wa mafunzo hayo Dkt. Hong- Kyu Choi.
Mkufunzi wa mafunzo ya kutengeneza Taa na Chaja zinazotumia mionzi ya jua, Dkt. Dkt. Hong- Kyu Choi, akiwaleza washiriki wa mafunzo namna mafunzo hayo yatakavyoendeshwa.
Mkuu wa Wilaya ya Musoma Vijijini, Dkt. Vicent Naano, (wa tatu kushoto) akiongea jambo mara baada ya uzinduzi wa mafunzo ya Kutengeneza taa na chaja zinazotumia mionzi ya jua. Wengine ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muongo (katikati), Balozi wa Korea Kusini nchini,Song Geumyoung Mkufunzi wa mafunzo hayo Dkt. Hong- Kyu Choi (wa pili kulia) na baadhi ya wawakilishi wa vijana wanaoshiriki mafunzo.
Mtaalam kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Emmanuel Yesaya, akizungumza jambo kuhusu utekelezaji wa REA awamu ya Pili na ya Tatu, katika Kata hiyo wakati wa Mkutano wa Waziri wa Nishati na Madini (hayupo pichani) na wananchi wa Kata ya Nyegina.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akikagua vitabu ambavyo baadhi alivigawa katika katika Kituo cha Sekondari ya Nyegina katika shule mbalimbali Mkoani Mara. Kulia ni Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Nyegina na Paroko wa Parokia hiyo, Padri Leo Kazeri.
Balozi wa Korea Kusini nchini,Song Geumyoung (wa tatu kulia) akiwa ameshika Taa za mfano ambazo vijana 20 kutoka Kata ya Nyegina watapewa mafunzo ya namna ya kuzitengeneza. Wengine wanaofuatilia ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Vijijini Dkt. Vicent Naano,(wa tatu kushoto) Mkufunzi wa Mafunzo hayo, Dkt. Hong-Kyu Choi (wa pili kushoto) na wawakilishi wa mafunzo hayo.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, akiweka tofali katika moja ya vyumba vya madarasa vinavyojengwa katika Shule ya Msingi Kata ya Bwasi, wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa shuleni hapo. Wengine ni Viongozi wa Vijiji, Halmashauri na wananchi wa Kijiji cha Kome.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (mwenye tisheti nyeusi) akiongea na wanafunzi wa shule ya msingi ya Kome mara baada ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuongea na wananchi wa Kijiji hicho.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, akimsikiliza mmoja wa wananchi aliyehudhuria katika mkutano wa Waziri na Wananchi wa Kijiji cha Kome. Wengine ni wanafunzi wa Shule ya Msingi wa Kome.

No comments: