Saturday, February 4, 2017

KINANA ATEMBELEA KUWAFARIKI YATIMA KATIKA KIJIJI CHA MATUMAINI, ENEO LA KISASA DODOMA, LEO

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwakabidhi msaada wa vyakula watoto wa Kijiji cha Matumaini, kilichopo eneo la Kisasa Dodoma mjini alipotembelea kituo hicho kuwafariki watoto yatima, leo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 40 ya CCM, ambayo kilele chake ni kesho. Kushoto ni mwanzilishi wa Kijiji hicho Padre Vincent Boseil
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na watoto wanaolelewa katika Kijiji cha Matumaini, kilichopo eneo la Kisasa Dodoma mjini alipotembelea kituo hicho kuwafariki watoto yatima, leo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 40 ya CCM, ambayo kilele chake ni kesho. Kulia ni mmoja wa waanzilishi wa kituo hicho Sista Roselie.

Kinana akionyeshwa eneo ambako hutunza watoto wachanga, ambao ni yatima, kwenye Kijiji hicho cha Matumaini

Kinana akimchukua mtoto mmoja kumfurahia, katika eneo hilo la kulea watoto wachanga
 Kinana akikaribishwa ndani na Mwanzilishi wa Kituo hicho, Padre  Vincent Boseili
 Kinana akisaini kitabu cha wageni alipowasili kwenye kituo hicho cha Kijiji cha Matumaini
 Padre Vincenti akionyesha wageni ramani ya Kijiji hicho cha Matumaini
 Sista Roselie akisoma risala
 Padre Vincent akitoa maelezo kuhusu kijiji hicho cha Matumaini
 Waziri Mavunde akizungumza alipokaribisha kuongea kwenye kijiji hicho cha Matumaini
 Mavunde akizungumza

Mavunde akipongezwa na Kinana baada ya kuzungumza neno la shukrani kwa mwanzilishi wa Kijiji hicho chenye kituo cha watoto yatima
Kinana akimpongeza Padre Vincent baada ya kuzungumza maneno ya shukrani
Kinana na ugeni wake wakienda kukagua sguhuli mbalimbali kwenye Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akiwasalimia watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho ambao pia wanasoma
Kinana akiwasalimia wanafunzi wa Sekondari wanalelewa na kusomeshwa na Kijiji hicho cha Matumaini. Kushoto ni Padre Vincent wa Kijiji hicho
Watoto ambao ni wanafunzi wanaolelewa na kusomeshwa kwenye Kijiji hicho wakiimba wimbo wa Taifa Kinana alipowasili
Wanafunzi wa Kijiji hicho wakipiga ala wakati wimbo wa Taifa la Tanzania ukiimbwa
Kinana akifurahia jambo kwa kupiga kofi huku mtoto wa Kijiji hicho aliyempakata naye akipiga kofi
Wanafunzi wa Sekondari wanaolelewa na kusomeshwa na Kijiji hicho cha Matumaini wakiimba wimbo wao maalum
Kinana akiwafurahia wanafunzi ambao alitambulishwa kwao na Padre Vincent
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimfurahia mtoto anayelelewa katika Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akikabidhi zawadi kwa watoto
Kinana akifurahia watoto wa Kijiji hicho baada ya kuwapa zawadi
Kinana akishiriki kuimba wimbo maalum pamoja na wanafunzi wanaolelewa na kusomeshwa katika Kijiji hicho
Kinana akionyeshwa eneo ambako kinamama hujifungulia bure kwenye Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akizungumzana wageni kutoka Italia ambao nao walifika kutembelea Kijiji hicho cha Matumaini
Kisha Kinana akamchumu mtoto huyo kwa upendo mkubwa
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini akimchukua mtoto kwa upendo
Watoto katika Kijiji hicho wakitazama kwa mshangao ugeni wa Kinana 
Katibu Mkuu Kinana akipewa maelezo kwenye mapokezi ya Hospitali ya Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akionyeshwa vifaa vya kupimia CD4 kwa wagonjwa wa Ukimwi
Kinana akimshukuru Padre Vincent baada ya kutembelea Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akiagana na Padre Vincnt kabla ya kuondoka
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini akiagana na Padre Vince pia kabla ya kuondoka. Picha zote na Bashir Nkoromo.  KINANA ASHIRIKI NA KUKAGUA SHUGHULI ZA MAENDELEO DODOMA LEO IKIWA NI SEHEMU YA MAADHIMISHO MIAKA 40 YA CCM
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Wilaya ya Dodoma mjini na mkoa huo, katika Ofisi ya CCM mkoa wa Dodoma, leo alipowasili kwenye ofisi hiyo, tayari kushiriki na kukagua shughuli za maendeleo ikiwa ni sehemu ya Madhimisho ya miaka 40 ya CCM ambayo kilele chake ni kesho. Akizungumza Kinana amesema, CCM imeamua kufanya Maadhimisho hayo mkoani Dodoma kwa kuwa imedhamiriwa kuisaidia Serikali katika kutekeleza ilani ya CCM, hivyo CCM imeamua kufanya hivyo ili kuunga mkono azma ya Serikali kuhamia Dodoma.
 Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana akitoa salamu za shukrani, baada ya Kinana kuzungumza katika mkutano huo wa ndani. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa huo, Adam Kimbisa.
 Katibu  Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwasalimia mafundi alipowasili kukagua na kupanda miti kwenye mradi wa Ujenzi wa Dampo la Kisasa katika eneo la Kata ya Matumbulu wilaya ya Dodoma Mjini, leo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 ya CCM ambayo kilele chake ni kesho.
 Katibu  Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akipanda miti kwenye mradi wa Ujenzi wa Dampo la Kisasa katika eneo la Kata ya Matumbulu wilaya ya Dodoma Mjini, leo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 ya CCM ambayo kilele chake ni kesho.
 Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Dodoma Mjini, akishiriki kupanda mji kwenye mradi huo
 Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini akishiriki kupanda mti kwenye eneo la mradi huo
 Mbunge wa Dodoma Mjini, Waziri Anthony Mavunde akishiriki kupanda mti katika eneo hilo
 Kinana akimpongeza kwa kupanda mti katika eneo hilo, Mzee Godfrey James
 Kinana akimsaidia kupanda mti mjumbe wa shina katika kata hiyo Ester Paschal
 Kinana na ujumbe wake wakiondoka katika upandaji mti na kwenda kukagua ujenzi wa dampo la kisasa katika eneo hilo. Kushoto ni Mavunde na kulia ni Kimbisa
 Mhandisi wa Manispaa ya Dodoma, Injinia John Nchilla akimpa Kinana maelezo kuhusu ujenzi wa dampo hilo la Kisasa katika Kata ya Matumbulu wilaya ya Dodoma Mjini
 Mwenyekiti wa CCM, Kata ya Nkuhungu, Dodoma Mjini, Pius Afa akimkaribisha Kinana kushiriki ujnezi na kupanda mti kwenye ujenzi wa Ofisi ya CCM ya Kata hiyo
 Wanachi wakimpokea Kinana kwa shamrashamra alipowasili katika Kata hiyo ya Nkuhungu
 Kinana akisalimia wananchi wa Nkuhungu
 Mwenyekiti wa CCM Kata ya Nkuhungu Pius Afa akimuonyesha Kinana ramani ya ujenzi wa Ofisi hiyo ya CCM ya Kata hiyo
 Kinana akipokea tofali alipokuwa akishiriki ujenzi wa Ofisi hiyo ya CCM Kata ya Nkuhungu
 Kinana akishiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Nkuhungu, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40ya CCM ambayo kilele chake ni kesho
 Kinana akishuka baada ya kushiriki ujenzi wa Ofisi hiyo kikamilifu
Kinana akizungumza na wananchi baada ya kushiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Mkuhungu, Dodoma leo. Picha zaidi  alipotembelea Kijiji cha Matumaini/>BOFYA HAPA

No comments: